Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,483
- 30,155
Nimekuwa nikimsikiliza Mara kwa Mara Rais wangu Magufuli, katika hotuba zake mbalimbali, anazotoa kwenye majukwaa ya kisiasa na Mara kwa Mara amekuwa akirudia kauli yake ya kulalamika na kusema kuwa kazi ya Urais ni ngumu sana na kama yeye angelijua hilo kabla, basi hata fomu ya Urais mwaka ule wa 2015 asingeenda kuchukua!
Nimekuwa nikatafakari sana kauli hii na kujiuliza hivi ni nini tafsiri ya kauli hii ya Rais?
Amekuwa pia akisema kuwa Mara kwa Mara amekuwa akienda na mafaili ya kazi hiyo ya urais, kwenye chumba chake cha kulala na amekuwa akikesha akifanya kazi hiyo ya urais
Nilichogundua ni kuwa kazi ya Urais siyo ngumu kivile kama ambavyo anavyodai Mheshimiwa Rais, lakini ni yeye mwenyewe anayeifanya kazi hiyo ya Urais iwe ngumu sana, kutokana na "hulka" wake wa kutaka kuifanya kazi hiyo ionekane kuwa ya "one man show" ndiyo tatizo kubwa
Hivi utawezaje kuona kazi ya Urais ngumu, wakati una taasisi nyingi zinazokusaidia kazi na hivyo kukurahisishia kazi yako?
Hivi katika nchi ambayo inaongoizwa na utawala bora, ambapo mihimili mitatu, ambayo ni Serikali, Mahakama na Bunge, ikiwa kila mhimili unafanya kazi yake kwa Uhuru bila kuingiliwa kati na mhimili wa serikali, utawezaje kuiona kazi ya Urais ngumu??
Nimsihi Rais wangu Magufuli ili ajiepushe na kuzeeka haraka, aruhusu kila aliyempa jukumu la kiutendaji, basi afanye kazi yake akiwa huru na yeye aingilie kati pale tu atakapothibitisha kuwa mteule wake "ameboronga" katika utumishi wake, lakini itakaootokea kuwa wewe mwenyewe Rais, una-wish You could be IGP, una-wish pia you could be CJ na pia una-wish You could be Speaker!
Huo si utawala bora na ni lazima "at the end of the day" utakwama na hutapata mtu wa kuja kukukwamua!
Nimekuwa nikatafakari sana kauli hii na kujiuliza hivi ni nini tafsiri ya kauli hii ya Rais?
Amekuwa pia akisema kuwa Mara kwa Mara amekuwa akienda na mafaili ya kazi hiyo ya urais, kwenye chumba chake cha kulala na amekuwa akikesha akifanya kazi hiyo ya urais
Nilichogundua ni kuwa kazi ya Urais siyo ngumu kivile kama ambavyo anavyodai Mheshimiwa Rais, lakini ni yeye mwenyewe anayeifanya kazi hiyo ya Urais iwe ngumu sana, kutokana na "hulka" wake wa kutaka kuifanya kazi hiyo ionekane kuwa ya "one man show" ndiyo tatizo kubwa
Hivi utawezaje kuona kazi ya Urais ngumu, wakati una taasisi nyingi zinazokusaidia kazi na hivyo kukurahisishia kazi yako?
Hivi katika nchi ambayo inaongoizwa na utawala bora, ambapo mihimili mitatu, ambayo ni Serikali, Mahakama na Bunge, ikiwa kila mhimili unafanya kazi yake kwa Uhuru bila kuingiliwa kati na mhimili wa serikali, utawezaje kuiona kazi ya Urais ngumu??
Nimsihi Rais wangu Magufuli ili ajiepushe na kuzeeka haraka, aruhusu kila aliyempa jukumu la kiutendaji, basi afanye kazi yake akiwa huru na yeye aingilie kati pale tu atakapothibitisha kuwa mteule wake "ameboronga" katika utumishi wake, lakini itakaootokea kuwa wewe mwenyewe Rais, una-wish You could be IGP, una-wish pia you could be CJ na pia una-wish You could be Speaker!
Huo si utawala bora na ni lazima "at the end of the day" utakwama na hutapata mtu wa kuja kukukwamua!