Rais Magufuli umedanganywa mengi kuhusu Mkurugenzi wa Wilaya ya Ileje, Undugu na Waziri Mkuu unampa jeuri na huambiwi ukweli na wasaidizi wako

Habari wanaJamvi,

Kwanza nianze kukupongeza kwa kututembelea katika mkoa wetu mpya wa Songwe kwa Mara ya kwanza tangu umekuwa mkuu wa nchi.Ni jambo jema kwa ustawi wa mkoa wetu

Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu,leo wakati unaweka jiwe la msingi katika barabara ya Mpemba-Isongole kuna mambo kadhaa yaliibuka hasa baada ya Mh.Mbunge wa jimbo la Ileje Janeth Mbene kusema kwamba mkurugenzi anakwamisha mengi Ileje na utusaidie kumuondoa

Mheshimiwa Mbunge alikuwa anatoa sauti ya wanaIleje wasio na sauti ya kukufikia,na sikama ulivyodanganywa kwamba yeye ni mchapakazi hadi anafundisha,watume vijana wako wakafanye utafiti wakwambie kama kweli anafundisha na ni shule gani? maana sikweli.

Huyu mkurugenzi anaundugu na waziri mkuu,mh. Kasimu Majaliwa na ndiyo fimbo yake tangu akiwa afisa elimu pale manispaa ya iringa na ndiyo maana anaogopwa na haguswi na hata mawaziri wako(Jafo),na RC anajua

Kwanza anatuhumiwa kwa ufisadi wa pesa ya ujenzi wa hospital ya wilaya pale Itumba,amekuwa akidai rushwa kwa wakandarasi akihitaji ten percent, haya mkuu wa wilaya anajua hata mkuu wa mkoa anajua na RC alishamuundia hata tume kumchunguza,ila hata RC hajakwambia ukweli.Maana kuna waliohusika pamoja na mkurugenzi waliwekwa mahabusu kwa amri yake.

Hawapi posho madiwani ni zaidi ya miaka kadhaa sasa,Uhusiano wake pia haupo vizuri na watumishi wa halmashauri,na mwenyekiti wa halmashauri ameshaandika barua nyingi tu kuhusu huyu mheshimiwa ila kwasababu anangao ya PM hachukuliwi hatua yoyote.

Sauti ya Mbunge Mbene Si yakinafiki kama ulivyomtafsiri ila uliamua kujitoa muhanga ili upate picha ya hali halisi ya wilaya ya ileje,maana hakuna mshikamano wa viongozi hata DC anamuogopa na maendeleo unayohubiri utakuwa unampigia mbuzi gitaa tu,maana saizi anatamba kuwa wameumbuka na genge lake,eti hawamuwezi kwasababu umemtetea mbele ya umma.

Kama unataka kuupata ukweli tuma vijana wako,utapata ukweli usiyo na shaka,ili utuondolee hili jipu maana anakwamisha maendeleo kwenye wilaya iliyonyuma sana hasa kwenye miundombinu ya barabara.

Ukweli utabainika tu bila shaka

Tatizo la wabongo tunapenda kukariri, kwa hiyo mlitaka atumbuliwe jukwaani..!
Rais amesema anasubiri uchunguzi ulio chini ya Waziri-Tamisemi..
Halafu ataona ukweli wa malalamiko hayo.
Ndipo achukue hatua..
 
"Hawapi posho madiwani ni zaidi ya miaka kadhaa sasa,Uhusiano wake pia haupo vizuri na watumishi wa halmashauri,na mwenyekiti wa halmashauri ameshaandika barua nyingi tu kuhusu huyu mheshimiwa ila kwasababu anangao ya PM hachukuliwi hatua yoyote."

Hapa ndipo kilipo chanzo cha mgogoro! njaa njaa! mnakaa kikao cha siku mbili mnadai posho za wiki moja, mkurugenzi akigoma nongwa!
 
"Hawapi posho madiwani ni zaidi ya miaka kadhaa sasa,Uhusiano wake pia haupo vizuri na watumishi wa halmashauri,na mwenyekiti wa halmashauri ameshaandika barua nyingi tu kuhusu huyu mheshimiwa ila kwasababu anangao ya PM hachukuliwi hatua yoyote."

Hapa ndipo kilipo chanzo cha mgogoro! njaa njaa! mnakaa kikao cha siku mbili mnadai posho za wiki moja, mkurugenzi akigoma nongwa!
Kwahiyo hilo pekee ndiyo umeliona? Kula pesa za hospital ya wilaya ni ruksa? Acha mawazo mgando
 
Tatizo la wabongo tunapenda kukariri, kwa hiyo mlitaka atumbuliwe jukwaani..!
Rais amesema anasubiri uchunguzi ulio chini ya Waziri-Tamisemi..
Halafu ataona ukweli wa malalamiko hayo.
Ndipo achukue hatua..
Upo sahihi,ila ni shida ya muda mrefu kina Jafo wanajua ila hawasemi ukweli
 
Nimesomaaaaaa. Nimesimaaaa
Kuna kauli kwenye post ina ukakasi
"Hana ushirikiano na madiwani"
Hapa ndipo panafanya DED awe salama kwangu, madiwani ni wapenda posho kama mtoa mada alivyodai hawapewi, wapige kazi kama wanaona posho hakuna waacha kazi waligombea kwa lengo la kutumikia watu kama ajira ipo tume ya ajira waende

Huenda ni zengwe tu ila kama upo ukweli huyu DED hakuchukui round
DSO na timu yake huwa hawaripoti umbea cheka nao kunywa nao ila wataripoti uhalisia wako, maana kila mmoja anaripoti kivyake
Hilo la posho za madiwani ni eneo dogo sana,Mpaka mkuu wa mkoa alimuundia tume ya ubadhilifu wa fedha na kazi huyu jamaa washirika wake pekee ndiyo wkapelekwa mahabusu.Ila ukweli huwa haujifichi ni suala la muda tu
 
Tupime kidogo tu,maelezo ya mtoa post,shutuma dhidi ya ded zimetolewa jana,sasa hayo majivuno ya kutamba kayatoa saa ngapi? Vema kumkumbuka hata mungu
 
Tukiwaambia serikali hii hakuna itakapofanikiwa mnatuita vibaraka wa mabeberu, wasaliti, sio wazalendo n.k, n.k, n.k lakini ukweli ni huu:
Kuna kikundi cha watu ndani ya serikali wanaojua kabisa udhaifu wa jiwe wa kupenda majungu na maamuzi ya mtu mmoja na ya kukurupuka.

Kwa mantiki hiyo wanahakikisha wanampa taarifa zisizo sahihi ili aendelee kuwa kituko huku wao wakinufaika binafsi. Muamini msiamini; nchi inaelekea kwenye machafuko na sababu itakuwa pamoja na maelezo yaliyomo kwenye huu uzi. Wanaofanya kazi kwa uadilifu (sina maana kuwa huyo mkurugenzi ni muadilifu au la - sina ushahidi either way) wanakuwa frustrated huku waharibifu wakipeta.
Kuharibu mfumo wa utawala ni kazi rahisi sana, ila kuujenga ukishabomoka ni shughuli pevu na ya muda mrefu.

Kwa heri Tanzania ya Nyerere.
Upo sahihi kuna watu wanafanya mambo ya ovyo ila bado hawaguswi,wakati jambo lilelile akifanya mwingine anatimuliwa faster
 
Nilijua tu....Ile ilikuwa Ni sauti ya madiwani.

Mkulu HAWEZI KUMTUMBUA mtu ambaye ana maslahi naye. Ushafikiria kuwa Kuna maslahi mkulu anapata kupitia kwa huyo DED??
Tamisemi ipo chini ya Pm na dogo anatambia hilo wazi wazi maana hata DC anamuogopa
 
Basi kuna changamoto kubwa katika nchi yetu
Atume vijana toka wapi wakati vijana wake mnao kila siku mnakunywa nao kahawa na pombe. Mkuu wa Nchi ana habari za nchi nzima na kabla hajaenda mahali anapata taarifa za kina za watendaji wake wa huko anakuja akiwa very well informed. Kabla hajaja kuna vijana wake wanakuja hata wiki mbili kabla ili kunusa na kuona hali ikoje ili wampe habari na hao vijana wala hawafungamani na yeyote hata PM.
 
Mungu anakazi nyingi achana naye,kama jambo hulijui ningumu kusadiki
Tupime kidogo tu,maelezo ya mtoa post,shutuma dhidi ya ded zimetolewa jana,sasa hayo majivuno ya kutamba kayatoa saa ngapi? Vema kumkumbuka hata mungu
 
Watanzania tuache kushabikia majungu, tuchape kazi , mbunge na madiwani walizoea kula kifisadi fedha za halmashauri, huyu DED hapendeki kwa vile anafuata kanuni na taratibu za mapato na matumizi ya raslimali fedha. Mbunge kakalia kuti kavu mwakani Harudi, hivyo anatafuta wa kuchomoka naye
Ileje unaijua vizuri ha ha ha ha,Mbunge anamapungufu mengi kweli na nikweli hawezi kupita tena,ila kuhusu DED aisee ngoja niishie hapo tu
 
Ndumbula anajaribu kudanganya ili kumtetea dadako.
Mbene ni mtu wa kuzusha hasa kwa sababu ya hofu yake kisiasa. Kazi yake huyo bibi ni kufukuza kila anayemuona hayuko naye vizuri. Labda nikukumbushe tu kuwa mwaka 2014 alimfukuza DED Siliwa kisa aliomba uwanja wa kujenga akamegewa kidogo wakati yeye alitaka chote. Yeye kupitia kwa kijana wake Ndabila walishinikiza madiwani wamuundie zengwe na akafukuzwa.
Mwaka 2015 kulikuwa na DED Otieno alisema yupo karibu na CDM na wakamfukuza wiki tatu Kabila ya uchaguzi akaenda Kakwembe. Mwaka 2016 alianza kumuomba Kakwembe mafuta alipoanza kunyimwa akawaita madiwani nyumbani kwake ili wamjengee hoja kuwa hanaushirikiano na madiwani na anakiburi. Mkurugenzi akahamishiwa Momba. Alivyokuja huyu amepambana kumtoa mara nyingi. Na wanashirikiana na madiwani watatu. Kwenye CCM nako amefukuza makatibu 4. Huyu mama anaishi Dar Ukimuona akaja Ileje ujue anashida na mtu. Akija lazima atengeneze mgogoro. Ni mtu wa visasi. Lengo lao ni kumuondoa mkurugenzi ili baada ya hapo wamuondoe na mwenyekiti wa Halmashauri. Unataka kuniambia Mbene anayeishi dar anajua mambo ya DED kuliko DSO na RCO? Ninajua unamtetea kwa kuwa ni dadako, lakini mwambie akauguze miguu.
Mkuu Najua Mbene anamapungufu mengi sana sana na hawezi kupita tena na nimama asiyeshaurika na mtu,mpaka kijana wake alidisco Dodoma university kwaajili ya kumpigania jimboni alishakosana naye na dogo akaenda kwa naibu spika ndiye anayemsomesha Pale mzumbe mbeya.

DED aisee,kwanza wakati anafika ileje alikuwa hana uzoefu na kazi aliyumba sana akapewa back up sikati kulisema hili,ila kama unajua issue ya itumba hospital, tume aliyounda RC na mengine,Mwenyekiti wa halmashauri ameshaandika barua kadhaa kuhusu DED ila hasikilizwi.Basi kama anasingiziwa ukweli utabainika tu
 
Ndumbula anajaribu kudanganya ili kumtetea dadako.
Mbene ni mtu wa kuzusha hasa kwa sababu ya hofu yake kisiasa. Kazi yake huyo bibi ni kufukuza kila anayemuona hayuko naye vizuri. Labda nikukumbushe tu kuwa mwaka 2014 alimfukuza DED Siliwa kisa aliomba uwanja wa kujenga akamegewa kidogo wakati yeye alitaka chote. Yeye kupitia kwa kijana wake Ndabila walishinikiza madiwani wamuundie zengwe na akafukuzwa.
Mwaka 2015 kulikuwa na DED Otieno alisema yupo karibu na CDM na wakamfukuza wiki tatu Kabila ya uchaguzi akaenda Kakwembe. Mwaka 2016 alianza kumuomba Kakwembe mafuta alipoanza kunyimwa akawaita madiwani nyumbani kwake ili wamjengee hoja kuwa hanaushirikiano na madiwani na anakiburi. Mkurugenzi akahamishiwa Momba. Alivyokuja huyu amepambana kumtoa mara nyingi. Na wanashirikiana na madiwani watatu. Kwenye CCM nako amefukuza makatibu 4. Huyu mama anaishi Dar Ukimuona akaja Ileje ujue anashida na mtu. Akija lazima atengeneze mgogoro. Ni mtu wa visasi. Lengo lao ni kumuondoa mkurugenzi ili baada ya hapo wamuondoe na mwenyekiti wa Halmashauri. Unataka kuniambia Mbene anayeishi dar anajua mambo ya DED kuliko DSO na RCO? Ninajua unamtetea kwa kuwa ni dadako, lakini mwambie akauguze miguu.
Mkuu Najua Mbene anamapungufu mengi sana sana na hawezi kupita tena na nimama asiyeshaurika na mtu,mpaka kijana wake alidisco Dodoma university kwaajili ya kumpigania jimboni alishakosana naye na dogo akaenda kwa naibu spika ndiye anayemsomesha Pale mzumbe mbeya.

DED aisee,kwanza wakati anafika ileje alikuwa hana uzoefu na kazi aliyumba sana akapewa back up sikati kulisema hili,ila kama unajua issue ya itumba hospital, tume aliyounda RC na mengine,Mwenyekiti wa halmashauri ameshaandika barua kadhaa kuhusu DED ila hasikilizwi.Basi kama anasingiziwa ukweli utabainika
 
Acha wivu ndugu, kuchongeana hakuna maana! Mwenzio akiharibikiwa ww utapata nn? Kama kuumbuka mshaumbuka chapeni kazi, kwa taarifa yako huyo Ded hana undugu wa aina yoyote na PM.
wakati PM anatokea Ruangwa mkoa wa Lindi, huyo Ded anatokea Newala mkoa wa Mtwara!
Narudia kwa sauti kubwa " Acha wivu nawe subiri wakati wako wa kuwa Ded, piga Kazi, majungu unafki, uzandiki na fitna ndizo zilituchelewesha maendeleo kwa miaka mingi"
Mkuu ninachokisema sijakurupuka,na Mara nyingi unafiki wa watz ni kusema ukweli, unadhani kutoka mikoa tofauti ndiyo sababu ya kutokuwa ndugu (This is fallacy)
 
Ngoja niende Isongole,Itumba nikapate ukweli Wa hayo yote nami nije nitoe ushuhuda wangu yupi ni kero kwa wana Wana Ileje
 
Back
Top Bottom