G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Rais wangu, hivi unajua kuwa pamoja na kukupinga sana ila ni miongoni mwa watendaji wako wasaidizi wakuu ndani ya serikali? Kwa taarifa yako ninasimamia moja ya taasisi ambazo kwa siku za hivi karibuni umeelekeza macho yako yote pale. Nipo na vijana wako unaowatuma kila siku na mambo yanaenda vizuri sana kwao chini ya usimamizi wangu usiofuata mkumbo wala ulambaji viatu. Pale ofisi ya msajili mkuu wa Hazina ni nyumbani kwangu na tunafanya vikao kila mara.
Twende kwenye mada.
Unajua kuwa mimi ni mwenyeji mkubwa pale Hazina? Unajua kuwa naelewa madudu yote uliyofanya dhidi ya sekta binafsi kuanzia mwaka 2016 mpaka jana? Unajua kuwa ninazo taarifa za uhakika kuwa kwa utaifishaji holela na uvurugaji wa mipango uliofanya nchi nzima umegharimu ajira za watu siyo chini ya elfu 50?
Naomba nikueleze kuwa siyo kila msaidizi wako anafurahishwa na jinsi unavyoendesha nchi! Naomba kwa leo niishie hapo ila nyongo ikizidi itatoka!
Tukutane Dodoma kesho kwenye ripoti muhimu uliyotutuma kuifanyia kazi Dar!
Twende kwenye mada.
Unajua kuwa mimi ni mwenyeji mkubwa pale Hazina? Unajua kuwa naelewa madudu yote uliyofanya dhidi ya sekta binafsi kuanzia mwaka 2016 mpaka jana? Unajua kuwa ninazo taarifa za uhakika kuwa kwa utaifishaji holela na uvurugaji wa mipango uliofanya nchi nzima umegharimu ajira za watu siyo chini ya elfu 50?
Naomba nikueleze kuwa siyo kila msaidizi wako anafurahishwa na jinsi unavyoendesha nchi! Naomba kwa leo niishie hapo ila nyongo ikizidi itatoka!
Tukutane Dodoma kesho kwenye ripoti muhimu uliyotutuma kuifanyia kazi Dar!