Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Mh rais wewe ni mkuu wa taifa letu, na taifa letu linaendesha kwa misingi ya kuilinda na kuiheshimu katiba ya JMT.
Ibara ya 13 (6)(b) ya katiba ya JMT imetamka wazi kuwa hakuna mtu atakutwa na hatia ya jinai mpaka mahakama ithibitishe na kumtia hatiani.
Kumpa amri IGP awe anawalazimisha watuhumiwa kuacha ujambazi inaleta wasiwasi kwa sisi ambao tunaona kama hukutumia lugha ya wazi. Je, walazimishwe kuacha ujambazi kwa namna gani?
Ni wazi kuwa hakuna mtanzania anayependa uhalifu, lakini nini maana ya kuwepo kwa haki jinai kama mtuhiwa amekamatwa bila kukaidi?
Je, watanzania waanze kusikia habari kama kipindi kile cha msitu wa Mabwepande? Kwamba watu wanakamatwa tena wanatii bila shuruti alafu tunasikia walimiminiwa risasi?
Ilikuwa ni jambo jema umpatie Igp Sirro hiyo amri lakini umpe tahadhari juu ya kutokuathiri uhai wa watu ambao watajikuta wanaingia kwenye madhara ya askari ambao watafanya kama yale tuliyosikia kipindi cha akina Zombe.
Ni wazi kuwa amri uliyoitoa leo inatakiwa itekelezwe kwa umakini sana, la sivyo utasikia malalamiko mengi juu ya uovu wa askari polisi. Maana hata kabla ya akina Zombe kutiwa hatiani kila mtu aliamini anayeuawawa na polisi alikuwa ni jambazi.
Ibara ya 13 (6)(b) ya katiba ya JMT imetamka wazi kuwa hakuna mtu atakutwa na hatia ya jinai mpaka mahakama ithibitishe na kumtia hatiani.
Kumpa amri IGP awe anawalazimisha watuhumiwa kuacha ujambazi inaleta wasiwasi kwa sisi ambao tunaona kama hukutumia lugha ya wazi. Je, walazimishwe kuacha ujambazi kwa namna gani?
Ni wazi kuwa hakuna mtanzania anayependa uhalifu, lakini nini maana ya kuwepo kwa haki jinai kama mtuhiwa amekamatwa bila kukaidi?
Je, watanzania waanze kusikia habari kama kipindi kile cha msitu wa Mabwepande? Kwamba watu wanakamatwa tena wanatii bila shuruti alafu tunasikia walimiminiwa risasi?
Ilikuwa ni jambo jema umpatie Igp Sirro hiyo amri lakini umpe tahadhari juu ya kutokuathiri uhai wa watu ambao watajikuta wanaingia kwenye madhara ya askari ambao watafanya kama yale tuliyosikia kipindi cha akina Zombe.
Ni wazi kuwa amri uliyoitoa leo inatakiwa itekelezwe kwa umakini sana, la sivyo utasikia malalamiko mengi juu ya uovu wa askari polisi. Maana hata kabla ya akina Zombe kutiwa hatiani kila mtu aliamini anayeuawawa na polisi alikuwa ni jambazi.