Rais Magufuli tusaidie sisi vijana wasomi kwenye mradi wa SGR

kikoozi

JF-Expert Member
Jun 24, 2015
2,030
2,923
Habari Mh rais Dr John Pombe Joseph Magufuli, Pole kwa majukumu mazito ya nchi kwa maana ya kitaifa na kimataifa kwa ujumla.

Awali ya yote tunatoa pongezi za dhati kabisa kwa serikali yako ya awamu ya tano, chini ya uongozi wako kwa kazi nzuri ulizozifanya na unazoendelea kuzifanya katika kuliletea maendeleo taifa letu, tunaona miradi mikubwa ya kimaendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo usafirishaji na uchukuzi kama vile ufufuaji wa shirika letu la ndege ATCL ikiambatana na ununuzi wa ndege mpya kabisa.

Ujenzi wa reli mpya kabisa ya umeme (SGR), uboreshaji wa miundo mbinu ya barabara kuunganisha mkoa na mkoa na kurahisisha mawasiliano,ujenzi wa barabara za juu (flyovers), Upitiaji upya wa mikataba na uboreshwaji wa sheria za madini hii ni kuhakikisha tunalinda rasilimali zetu na kunufaika kama nchi, mradi wa usambazaji wa umeme vijijini REA kupitia wizara ya nishati, haya ni machache tu katika yale mengi unayoyafanya.

Dhamira yako ya dhati na hulka ya kujitoa bila kujali hali hii inadhihirisha kua wewe ni mzalendo wa kweli.

Dhumuni kuu la andishi langu hapa JamiiForums ni kukuomba Mh rais sisi vijana ambao wengi wetu ni wasomi wa vyuo vikuu hapa nchini mabao tupo kwenye mradi huu wa SGR tunaomba usitusahau Mh rais tunakuomba sana sana utusaidie kupata ajira endapo mradi huu utakamilika, mradi huu umebeba vijana wadogo wenye taaluma mbalimbali, kuna ma engineer, wataalam wa technolojia (IT), Telecommunication, Electrical etc.. etc..

Siku yoyote ile utakapotembelea mradi huu au kuja kuuzindua baada ya kukamilika tunaomba utoe neno lolote jema ambalo litaenda kutuponya sisi vijana tuliopo kwenye mradi huu

Tuna kutakia kazi njema na afya njema baba yetu kipenzi na raisi wetu mpendwa Dr John Pombe Joseph Magufuli

Mungu ibariki Tanzania.
 
Uzuri umeshamuelewa vzr,unaanza kwa kusifia sana/kuunga mkono juhudi then unamalizia kwa kueleza shida yako.

Kwa style hio amesikia malalamiko yako.
ayo ni yako, tunachoamini ni kuwa rais wetu ni mtu makini, na msikivu sana ndio maana tupo nae bega kwa bega
 
ayo ni yako, tunachoamini ni kuwa rais wetu ni mtu makini, na msikivu sana ndio maana tupo nae bega kwa bega
Uko naye bega kwa bega? Ungeacha kulialia basi ukamuunge mkono kwa kuanzisha kiwanda... Msomi hata kiwanda cha kati cha kubrashi viatu huna... dah!
 
Kikoozi,
by Kikoozi, ... Dhumuni kuu la andishi langu hapa JamiiForums ni kukuomba Mh rais sisi vijana ambao wengi wetu ni wasomi wa vyuo vikuu hapa nchini mabao tupo kwenye mradi huu wa SGR tunaomba usitusahau Mh rais tunakuomba sana sana utusaidie kupata ajira endapo mradi huu utakamilika, mradi huu umebeba vijana wadogo wenye taaluma mbalimbali, kuna ma engineer, wataalam wa technolojia (IT), Telecommunication, Electrical etc.. etc..
Mhandisi: Reli ya SGR mpya kuchukua miaka 15 kumalizika
February 5, 2020 Kilosa, Tanzania Wahandisi : Reli ya kati ihamishwe toka eneo la mafuriko na pia SGR kuchukua miaka 15 kukamilisha Wakati wa ukaguzi wa uharibifu wa njia ya reli ya kati sehemu za Gulwe na Kilosa, wataalamu wa ujenzi wa reli wamebainisha kuwa Tanzania itaendelea
Source: Mhandisi: Reli ya SGR mpya kuchukua miaka 15 kumalizika
 
Habari Mh rais Dr John Pombe Joseph Magufuli, Pole kwa majukumu mazito ya nchi kwa maana ya kitaifa na kimataifa kwa ujumla.

Awali ya yote tunatoa pongezi za dhati kabisa kwa serikali yako ya awamu ya tano, chini ya uongozi wako kwa kazi nzuri ulizozifanya na unazoendelea kuzifanya katika kuliletea maendeleo taifa letu, tunaona miradi mikubwa ya kimaendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo usafirishaji na uchukuzi kama vile ufufuaji wa shirika letu la ndege ATCL ikiambatana na ununuzi wa ndege mpya kabisa.

Ujenzi wa reli mpya kabisa ya umeme (SGR), uboreshaji wa miundo mbinu ya barabara kuunganisha mkoa na mkoa na kurahisisha mawasiliano,ujenzi wa barabara za juu (flyovers), Upitiaji upya wa mikataba na uboreshwaji wa sheria za madini hii ni kuhakikisha tunalinda rasilimali zetu na kunufaika kama nchi, mradi wa usambazaji wa umeme vijijini REA kupitia wizara ya nishati, haya ni machache tu katika yale mengi unayoyafanya.

Dhamira yako ya dhati na hulka ya kujitoa bila kujali hali hii inadhihirisha kua wewe ni mzalendo wa kweli.

Dhumuni kuu la andishi langu hapa JamiiForums ni kukuomba Mh rais sisi vijana ambao wengi wetu ni wasomi wa vyuo vikuu hapa nchini mabao tupo kwenye mradi huu wa SGR tunaomba usitusahau Mh rais tunakuomba sana sana utusaidie kupata ajira endapo mradi huu utakamilika, mradi huu umebeba vijana wadogo wenye taaluma mbalimbali, kuna ma engineer, wataalam wa technolojia (IT), Telecommunication, Electrical etc.. etc..

Siku yoyote ile utakapotembelea mradi huu au kuja kuuzindua baada ya kukamilika tunaomba utoe neno lolote jema ambalo litaenda kutuponya sisi vijana tuliopo kwenye mradi huu

Tuna kutakia kazi njema na afya njema baba yetu kipenzi na raisi wetu mpendwa Dr John Pombe Joseph Magufuli

Mungu ibariki Tanzania.
Wewe ni miongoni mwa wasomi mafala
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom