Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,498
- 51,092
Nyerere alisifiwa sana lakini hakupenda misifa ya kijinga. Na alikuwa anajua sana kuwasoma wanaotafuta vyeo kwa kumsifusifu akawa hawapi au anatafuta namna ya kuwanyamazisha kwa vijembe vya hali ya juu.
Mheshimiwa Rais, stuka sasa hawa wanakusifusifu hovyo hawakutakii mema, wanakung'ong'a, wanakupaka mafuta kwa. mgongo wa chupa!
Wamekusoma, wamekuelewa kuwa unapenda ujiko na wao sasa kila mmoja anatafuta ujiko mkuubwa ili akupatie.
Na kimsingi hawa wanaosifu bila haya wanatafuta nini? Wanataka uwape nafasi tu washibishe matumbo yao.
Mheshimiwa these people are embarrassing you, yaani wanakupamba ili kukupanga, wakataze la sivyo watakufanya kituko ndani ya Taifa na huko nje kwenye Mataifa.
1. Kuna yule aliyedai ni mnyonge katoka huko kavaa barakoa lakini alipofika mbele yako mnyonge yeye kaamua kuivua.
2. Kuna yule anayedai utake usitake utalazimishwa Uraisi, Yaani upende usipende Katiba itabadrishwa kwa ajili yako.
3. Kuna yule aliyesema kuwa kuna sehemu ndani ya jiji la Dodoma sharti iitwe Magufuli city.
4. Kuna huyu anakuita YESU, kwamba ulipomtengua nafasi ni sawa na bwana Yesu anatwaa kilicho chake.
5. Kuna hawa kila baada ya sentensi moja wanataja jina lako
6. Bahati mbaya hata viongozi wa dini nao wameingia kwenye mkumbo, kuna yule sheikh aliyesema kuwa wewe ni kichwa sana na asiyekubaliane na wewe afe huku akiharisha akataka watu waseme Amen
7. Kuna hao wa makanisa ya kupiga hela, nao ndo kutwa kucha kuimba sifa kwako
Mheshimiwa ngoja nikwambie kitu, Mwenyezi Mungu anakataza kutukuza tukuza watu kupita kiasi kwa muktadha huu inabidi ukataze wanaokutukuza namna hii japo kiukweli kabisa wanakucheza shere, hawakutakii mema, sisi wananchi tunaona ni vituko kabisa maana tunawaangalia tunaona kabisa they don't mean it!
Mheshimiwa umebakiza miezi michache madarakani, baada ya muda itategemea kama Mungu ataamua kukurudisha kwenye hiyo nafasi au la, basi kaa chini ufikiri, je kipindi utakapokuwa nje ya hicho kiti hao wanaokutukuza tukuza wataendelea kukutukuza au sasa watatafuta "Bwana" mpya?
Mheshimiwa rais kuwa makini sana na malaya wa kisiasa, wao watatukuza yeyote atakayewapa madaraka, vyeo au pesa na hao malaya wa kisiasa pindi wakipata "Bwana" mpya ndo watakuwa wa kwanza kukuponda!
Mheshimiwa rais stuka! watu wanataka usiwakate kwenye kugombea ubunge!
Mheshimiwa Rais, stuka sasa hawa wanakusifusifu hovyo hawakutakii mema, wanakung'ong'a, wanakupaka mafuta kwa. mgongo wa chupa!
Wamekusoma, wamekuelewa kuwa unapenda ujiko na wao sasa kila mmoja anatafuta ujiko mkuubwa ili akupatie.
Na kimsingi hawa wanaosifu bila haya wanatafuta nini? Wanataka uwape nafasi tu washibishe matumbo yao.
Mheshimiwa these people are embarrassing you, yaani wanakupamba ili kukupanga, wakataze la sivyo watakufanya kituko ndani ya Taifa na huko nje kwenye Mataifa.
1. Kuna yule aliyedai ni mnyonge katoka huko kavaa barakoa lakini alipofika mbele yako mnyonge yeye kaamua kuivua.
2. Kuna yule anayedai utake usitake utalazimishwa Uraisi, Yaani upende usipende Katiba itabadrishwa kwa ajili yako.
3. Kuna yule aliyesema kuwa kuna sehemu ndani ya jiji la Dodoma sharti iitwe Magufuli city.
4. Kuna huyu anakuita YESU, kwamba ulipomtengua nafasi ni sawa na bwana Yesu anatwaa kilicho chake.
5. Kuna hawa kila baada ya sentensi moja wanataja jina lako
6. Bahati mbaya hata viongozi wa dini nao wameingia kwenye mkumbo, kuna yule sheikh aliyesema kuwa wewe ni kichwa sana na asiyekubaliane na wewe afe huku akiharisha akataka watu waseme Amen
7. Kuna hao wa makanisa ya kupiga hela, nao ndo kutwa kucha kuimba sifa kwako
Mheshimiwa ngoja nikwambie kitu, Mwenyezi Mungu anakataza kutukuza tukuza watu kupita kiasi kwa muktadha huu inabidi ukataze wanaokutukuza namna hii japo kiukweli kabisa wanakucheza shere, hawakutakii mema, sisi wananchi tunaona ni vituko kabisa maana tunawaangalia tunaona kabisa they don't mean it!
Mheshimiwa umebakiza miezi michache madarakani, baada ya muda itategemea kama Mungu ataamua kukurudisha kwenye hiyo nafasi au la, basi kaa chini ufikiri, je kipindi utakapokuwa nje ya hicho kiti hao wanaokutukuza tukuza wataendelea kukutukuza au sasa watatafuta "Bwana" mpya?
Mheshimiwa rais kuwa makini sana na malaya wa kisiasa, wao watatukuza yeyote atakayewapa madaraka, vyeo au pesa na hao malaya wa kisiasa pindi wakipata "Bwana" mpya ndo watakuwa wa kwanza kukuponda!
Mheshimiwa rais stuka! watu wanataka usiwakate kwenye kugombea ubunge!