Rais Magufuli sitisha mambo yote wekeza kwenye Elimu bora kwanza

herikipaji

JF-Expert Member
Aug 23, 2016
1,198
1,345
Naomba rais Magufuli katika mambo yote unayofanya au unayotaka kufanya utoe kipaumbele kwanza katika sekta ya elimu, Elimu ni dira kuu na msingi mkuu katika ustawi wa jamii na taifa lolote lile ndio maana hata Mwalimu Nyerere alitumia akili na nguvu zake zote kuwasomesha Watanzania kwa hali na mali hata kuwapeleka nje ya nchi mfano China, Urusi nk.

Mwalimu Nyerere aliamini katika Elimu bora kwanza na sio kitu kingine na alitarajia Watanzania kupata Elimu kwanza ili watumie kujenga taifa na kuushinda umaskini. Mwalimu Nyerere leo na hata kesho ataendelea kukumbukwa kwa hili la kupigania Elimu bora.
Hakuna viwanda, hakuna. Hakuna uchumi wa kati, hakuna. Hakuna chochote kitakachofanikiwa pasipo elimu, hakuna.
Mataifa yote yalio dunia ya kwanza hii leo yanatoa misaada kwenye nchi maskini Tanzania ikiwemo lakini waliwekeza katika elimu. Nenda China, Urusi, Sweden, USA, Israel nk wamewekeza kwenye elimu bora kwanza sio kingine.

Nakuomba rais Magufuli sitisha mambo mengine yote ufanye uwekezaji katika elimu bora, elimu bora italeta viwanda, elimu bora italeta uchumi wa kati, Tanzania itaondokana na umaskini tukifanikiwa kupata elimu bora na wewe rais Magufuli utakumbukwa kwa hilo kama tunavyomkumbuka Mwalimu Nyerere.

Pesa inayotumika kulipa madeni aliyosema Makamu wa rais Mama Samia Suluhu kiasi cha shilingi bilioni 900 itumike kwenye kutoa mikopo ya elimu ya juu kwanza hayo madeni sitisheni kulipa kwanza.
Jamii ya Watanzania inalia na kusaga meno sababu watoto wetu wanakosa mikopo ya elimu ya juu na kushindwa kusoma sifa na vigezo vyote wanavyo.

USISAHAU HAKUNA TAIFA LILILOENDELEA KWA KUIPUUZA ELIMU, HAKUNA.
ITAKUWA NI MAAJABU YA DUNIA TANZANIA IWE TAIFA LINALOPUUZA ELIMU NA LIPATE MAENDELEO.

herikipaji.
MDAU WA ELIMU TANZANIA.
 
Kwani JK alivyomfyatua Ndalichako mlifikiri alikuwa zuzu?
Matokea yake ndio hayo elimu bora kwa kila kijana M-TZ imekuwa ndoto
Walianza kidato cha sita 21000 kukosa nafasi, sasa wanafunzi wa vyuo vikuu wanakosa mikopo.Kisa wanalewa sana pombe.
 
Kwani JK alivyomfyatua Ndalichako mlifikiri alikuwa zuzu?
Matokea yake ndio hayo elimu bora kwa kila kijana M-TZ imekuwa ndoto
Walianza kidato cha sita 21000 kukosa nafasi, sasa wanafunzi wa vyuo vikuu wanakosa mikopo.Kisa wanalewa sana pombe.
.....na kununua Tv
 
Magu Alishasema Muache Kuandikaa Weeeeeeee......


Lowassa.. alisema Mara Tatu(ELIMU ...ELIMU....ELIMU) Hakumsikiliza
 
bongo ajabu sana Mzazi msomi anashauriwa kusomesha mtoto wake angekua unaemshauri hajasoma ningesema hajui faida ya Elimu..Wazazi waliuza ng'ombe tena wa maziwa ili mpate Elimu ninyi mnanunua Ndege ili watu wakose Elimu...kwa maamuzi hayo wenye vyeti Feki na halari wote sawa hamjavitendea haki vyeti vyenu..
 
bongo ajabu sana Mzazi msomi anashauriwa kusomesha mtoto wake angekua unaemshauri hajasoma ningesema hajui faida ya Elimu..Wazazi waliuza ng'ombe tena wa maziwa ili mpate Elimu ninyi mnanunua Ndege ili watu wakose Elimu...kwa maamuzi hayo wenye vyeti Feki na halari wote sawa hamjavitendea haki vyeti vyenu..
 
Kwani JK alivyomfyatua Ndalichako mlifikiri alikuwa zuzu?
Matokea yake ndio hayo elimu bora kwa kila kijana M-TZ imekuwa ndoto
Walianza kidato cha sita 21000 kukosa nafasi, sasa wanafunzi wa vyuo vikuu wanakosa mikopo.Kisa wanalewa sana pombe.
Halafu kweli anaskia hivi vilio?
 
Mh. Rais anatakiwa aache wizara ya fedha watekeleze bajeti ya 2016/17 proffesionally. Inawezekana ana nia ya kutoa mikopo kwa wote, lakini kwakuwa alitapanya fedha unprofessionally sasa anakosa hela za kuwapa. Mh. Rais akubali kufuata mipango kazi....na sio vya moyoni
 
RAIS WETU MAGUFULI KILA KITU NI MUHIMU KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU,GAWA BAJETI KOTE KOTE KWANI HAKUNA LISILO LA MUHIMU
***
barabara ni muhimu.
Maji ni muhimu.
Kilimo ni muhimu.
madarasa ni muhimu.
umeme ni muhimu.
elimu ya Juu ni muhimu.
elimu ya msingi ni muhimu.
•NAOMBA RAIS WETU MAGUFULI ASOME HAPA.
 
Kupanga ni kuchagua,ila busara na hekima yatakiwa itumike ili kuepuka kuumiza RAIA
 
Hivi mustakabali wa nchi unaamliwa na rais au bunge. Ni hatari kwa nchi kuongozwa na mtu mmoja, madhara yake yataumiza taifa hili na litaangamia na watu wake
 
Watoto wa masikini wakisoma nchi hii aitatawalika kama una bisha uliza nyerere kilicho taka mkuta baada ya kutaka kuwapa watoto wa masikini.!!!!!!

Kwa kifupi hawa watu awataki kutupa elimu wakijua awata tu tawala vizuri. Fikiri
 
RAIS WETU MAGUFULI KILA KITU NI MUHIMU KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU,GAWA BAJETI KOTE KOTE KWANI HAKUNA LISILO LA MUHIMU
***
barabara ni muhimu.
Maji ni muhimu.
Kilimo ni muhimu.
madarasa ni muhimu.
umeme ni muhimu.
elimu ya Juu ni muhimu.
elimu ya msingi ni muhimu.
•NAOMBA RAIS WETU MAGUFULI ASOME HAPA.
Chanzo cha umaskini unafikiri ni nini?
 
Back
Top Bottom