Rais Magufuli: Sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani (Covid19), tutaendelea kuchukua tahadhari zingine za kiafya. Akemea Chanjo

John Magufuli: A science teacher who decries science in fighting Coronavirus. What has gone wrong?​

11a66b6f0dc328e4c1a564900f0df301

Rehema Ibrahim 28th January 20210 Comments

DETRIMENTAL? Devastating? Disastrous? Careless? Bullying? Narcissistic? Sadistic? Which word exactly fits the description of the character and statements of Tanzania’s President John Magufuli in his handling of the COVID-19 pandemic?
No one really knows what has befallen President Magufuli, a PhD holder in Chemistry and a former science teacher, who does not seem to believe in science any more when it comes to protecting his people against the adverse effects of the Coronavirus infections.
IMG-20210128-WA0317.jpg

A complete Corona denialist and a skeptic of globally-renowned WHO, Magufuli has resorted to unscientifically proven methods of countering the pandemic – at the detriment of his people’s lives.
Taking advantage of a highly religious society he is ruling, he has severally told his people to rely more on prayers and traditional herb concoctions than on scientific and medical solutions.
On many occasions, he keeps on reiterating that “Tanzania is a corona free country,” citing prayers as the solution.
With a bit of a nationalistic-cum-racist tone, he has publicly voiced out his doubts on the foreign-made medical solutions, including the vaccines made and distributed by what he calls “wazungu,” that is, “white people.”
But his stance is no surprise. In 2011, Magufuli was one of senior politicians in the country who gulped a local herb from the famous “Babu wa Loliondo” in Northern Tanzania, retired church leader Rev. Ambilikile Mwaisapile, who claimed to have been “directed” by God to prescribe a multi-diseases cure herb that was administered by drinking from a special cup – in a one-dose-fits-all-diseases fashion.
President Magufuli’s handling of the COVID-19 pandemic, his repeated public dismissals of scientific expertise, and his contempt for evidence have prompted some researchers to tag him the most anti-science president in Africa.
Early this week, probably after getting tired of Tanzania government’s position on the pandemic in the obviously frequent deaths due to the new wave of Coronavirus infections in the country, bishops from the Tanzania Episcopal Conference (TEC) spoke up through an official statement to its believers and the nation calling on them to take responsible decisions and protect themselves from the pandemic.
Magufuli ordered the government to stop releasing data on the pandemic since 29th April 2020.
This week alone, Magufuli has spoken more than once claiming that the vaccines against COVID-19 are dangerous. Instead, he advised his citizens to rely on local herbs.
“These vaccines are dangerous. If the white people were able to come up with vaccines, they should have found a vaccine for tuberculosis, and they could have eliminated AIDS by now. A vaccine for cancer would have been found by now,” he said.
In analysing President Magufuli’s irresponsible remarks on record regarding this pandemic, including the denial and embracing misinformation, the leader of the Zanzibar centred ACT-Wazalendo party, Zitto Kabwe, has strongly criticised President Magufuli for neglecting science.
Magufuli’s approach, he says, poses a serious threat to the citizens who have almost completely abandoned most of WHO guidelines in combating Coronavirus.
Dr Matshidiso Moeti, Africa Director for the World Health Organization (WHO), today urged Tanzania to abide by science.
On her Twitter account, she says: “Urging #Tanzania to ramp up public health measures such as wearing masks to fight #COVID19, science shows that #VaccinesWork and I encourage the government to prepare for a COVID vaccination campaign.”
The WHO Director General, Dr Tedros Ghebreyesus, echoed what Dr Matshidiso said on Tanzania. He called on Tanzania to support the global efforts in fighting the pandemic.
Robert Amsterdam’s tweet on Magufuli’s position was more punchy: “This man is a stain on humanity!”
President Magufuli is surrounded by many, and they know a lot. By the way, are those vaccines that he said never existed, really do not exist, or has he lied? Was that which caused His Excelency to say that oil and papaya tested positive for the corona virus not Science? President Magufuli uses scientific research to criticize or reject other scientific research. You never know the said vaccine may have been already available for days and then worked in a laboratory. Like on the issue of papayas and oil, people worked first in the laboratory, and without knowing that they were working on oil or papayas, and after the results were confirmed, he appeared on stage. I'm worried even this time he has emerged on stage having already done extensive research or scientific enquiry. The president of the country can't just suddenly appear uttering words on stage that he has no research with, completely impossible




Rais Magufuli amezungukwa na wengi, na wananajua mengi. By the way, hizo chanjo alizosema kuwa hazijawahi kuwepo, ni kweli hazipo, au amedanganya? Kilichosababisha Mh. Rais akasema kuwa oil na mapapai yali-test positive kwa corona virus haikuwa Sayansi? rais Magufuli anatumia utafiti wa Sayansi ku-criticize au kukataa utafiti mwingine wa ki-Sayansi. Huwezi kujua pengine hiyo chanjo alishaipata siku nyingi na ikafanyiwa kazi kwenye maabara. Kwenye issue ya mapapai na oil, watu walifanya kazi kwanza kwenye maabara, na pasipo kujua kuwa wamepewa oil au mapapai, halafu matokeo yalipotoka ndiyo akaibuka jukwaani. Nina wasiwasi hata safari hii ameibuka jukwaani akiwa tayari ameshafanya utafiti wa kina. Rais wa nchi hawezi akaibuka tu ghafla kutamka maneno jukwaani ambayo hana utafiti nao, completely impossible
 
Kwa sasa kinachoendelea ni utambulisho wa viongozi ikiwemo wizara na idara za serikali. Waliokuwepo kwa uchache ni Dkt. Damass Ndumbaro, Medadi Kalemani ambae ni mbunge mwenyeji na waziri wa nishati, Dotto Biteko ambae ni waziri wa madini, Elias Kwandikwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Waziri wa maji, Jumaa Aweso na Marry Masanja Naibu waziri wa Utalii. Pia yupo Mwita Waitara naibu wa Mazingira.

Pia upo uongozi wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii, wapo wakurugenzi, wakuu wa taasisi ikiwemo Tawa, Tafori na DTI. Upo pia ungozi wa mkoa wa Geita ukiongozwa na mkuu wa mkoa, makatibu tawala na manaibu wao, wakurugenzi wa halmashauri za wilaya, kamati ya usalama wilaya ya Chato, viongozi wa chama cha Mapinduzi Geita, viongozi wa dini mkoa na wilaya pia wabunge wa mkoa wa Geita.

=========

Medard Kalemani: Mheshimiwa Rais wetu, sisi wananzengo na wananchi wa Chato kwa siku ya Leo ni siku ya furaha kubwa na kwetu sisi ni siku ya kihistoria, nichukue nafasi hii kwa niaba ya wananzengo na wananchi wa Jimbo letu na wilaya yetu ya Chato, kwanza kabisa kuwakaribisheni Chato.

Chato ndugu zangu ni nchi yetu sote, naomba wananchi wa Chato tuwapigie makofi wageni wote waliofika hapa.

Nimesikia huu ni msitu wa pili kwa ukubwa nchini kwetu, hongereni sana. Pia msitu ni wa kwanza kwa aina ya misitu mchanganyiko, misitu ya kupanda na misitu asili. Eneo hili limetoa ajira na watumishi na wafanyakazi ni wanaozunguka maeneo haya.

Mheshimiwa Rais na ndugu wananchi, kwa heshma ya pekee napenda nitoe shukrani ya moyoni, hawa wananchi walioko hapa kama kawaida ya misitu mmetupatia chakula, nawaomba wananchi tushangilie sana. Kitendo cha kutupatia ng'ombe wanne wakubwa madume yaliyonona kwa ajili ya wananchi hawa kula walau leo mchana na kilo 1,500 kwa ajili ya chakula cha mchana tunawashukuruni sana, wananchi tupige makofi na vigerere kwa ushirikiano huu mzuri. Mheshimiwa Rais na Waziri baada ya kusema hayo, niwashukuruni sana kwa kunisikiliza.

10:20 Asubuhi: Rais John Magufuli amewasili eneo la tukio na kupokewa na viongozi kadhaa kisha kuimbwa wimbo wa Taifa na wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Baada yahapo zimefata Dua na Sala kutoka kwa viongozi wa dini.

RAIS MAGUFULI: Nimeanzisha mashamba mengine manne ya misitu. Nina historia na eneo hili, wakati nikiwa mbunge ukifanya mkutano tu kwenye maeneo kutoka hapa Buseresere mpaka Bwanga.

Sikutegemea kama siku moja tutakuta miti mizuri shamba hili, mmefanya kazi kubwa sana, hongereni sana. Mimi nafikiri kwa kazi kubwa iliyofanywa na wizara ya maliasili na utalii lakini kwa kazi kubwa iliyofanywa na kamishna anaehusika na hifadhi ya misitu lakini kwa kumbukumbu kubwa ya vijana hawa maaskari wameendelea kulinda rasilimali hii

Katika kipindi hiki ambako kuna magonjwa gonjwa yanayojitokeza yasiyojulikana kama Korona, nchi nyingi wananchi wake watakuwa wamejifungia ndani, sisi Watanzania hatujajifungia ndani na hatutegemei kujifungia ndani na wala sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani kwa sababu Mungu wetu yuko hai na ataendelea kutulinda Watanzania lakini pia tutaendelea kuchukua tahadhari zingine za kiafya ikiwa ni pamoja na kujifukizia. Unajifukizia huku unamuomba Mungu, unaswali huku unapiga zoezi la kufanya kazi la kulima mahindi, viazi ili ule vizuri ushibe Corona ishindwe kuingia kwenye mwili wako.

Mtatishwa sana ndugu zangu Watanzania lakini simameni imara, ninajua wapo baadhi ya Watanzania wameondoka ndani ya nchi na kukimbilia maeneo mengine na kwenda kuchanjwa na walipochanjwa huko, wamekuja huku wametuletea Corona ambayo ni ya ajabu ajabu, simameni imara.

Chanjo hazifai, kama wazungu wangekuwa na uwezo wa kuleta chanjo, hata chanjo ya Ukimwi ingekuwa imeshaletwa, hata chanjo ya kifua kikuu, kifua kingekuwa kimeshaondoka, hata chanjo ya maleria ingekuwa imeshapatikana, hata chanjo ya kansa ingekuwa imeshapatikana.

Ni lazma Watanzania tuwe waangalifu kwa mambo ya kuletewa letewa, msije mkafikiria mnapendwa sana. Taifa hili ni tajiri, Afrika ni tajiri, kila mmoja anaitamani, tuwe waangalifu na niiombe wizara ya afya isiwe inakimbilia mambo ya machanjo chanjo bila yenyewe kujiridhisha.

Ipo nchi fulani watoto wake walichanjwa wa kike umri wa miaka 14, wanaambiwa ni kwa ajili ya kuzuia kansa ya kizazi, imekuja kugundulika ile chanjo ni kwa ajili ya kuwazuia wasizae, kwa hiyo niiombe sana Wizara ya Afya, sio kila chanjo ni ya maana kwa Taifa letu.

Sio kila chanjo ina faida kwetu, ni lazima Watanzania tuwe macho, ni lazima watanzania tuwe waangalifu, tutafanyiziwa majaribio ya ajabu ambayo yataleta madhara makubwa, ninaomba tuendelee kusimama na kumuomba Mungu wetu, tuendelee kumtanguliza Mungu wetu huku tukichukua tahadhari za kiafya kadri tutakavyokuwa tunaambiwa na wataalam wetu lakini tujihadhari sana.

Tumeweza kukaa zaidi ya mwaka mzima na kitu, Tanzania tukiwa hatuna Corona hata hapa hakuna alievaa barakoa, Mungu wetu yuko mbele ya shetani.

Kwa hiyo niwaombe ndugu zangu Watanzania na hasa Wizara wa Afya ambae ni kiongozi wetu ijitahidi sana kuangalia afya za Watanzania bila kuingia kwenye papara za kuletewa kila jaribio linalofanyika linaletwa hapa, hii ni tahadhari na mimi naamini tutafanikiwa.
Mmmh
 
Back
Top Bottom