Duh! Mkuu katema cheche za maana. Kwa namna yoyote ile kama kuna mtoto alishaanza kufurahi kudonolewa amenywea. Safi!Ameyasema hayo leo akiwa Bagamoyo kwenye uzinduzi wa barabara.
"Kwenye utawala wangu siko tayari kuruhusu ujinga kama huu, kama wanaona inafaa basi wafungue shule za wazazi ili huku wakiendelea na masomo waendelee kunyonyesha watoto wao."
Ameongeza kuwa hizo NGOs ndio zimeleta mambo ya ajabu ajabu hadi wanaume kwa wanaume kuingiliana, wanawake kwa wanawake kuingiliana.
"Hata wanyama hawafanyi hivyo mbuzi Ng'ombe huwezi kuwaona wakikosea ile sehemu...Wachungaji si mpo hapa mmewahi kuwaona mbuzi wakikosea au ng'ombe wakikosea"....aliongeza Magufuli.