Rais Magufuli shtuka nchi ipo kwenye vita kali sana ya Coronavirus

Mr pianoman

JF-Expert Member
May 22, 2019
2,548
6,102
Kabla ya yote mtanisamehe katika uandishi wangu, lakini huu ndio ujumbe wangu kwa Mheshimiwa Magufuli.

Mheshimiwa Rais, popote usomapo ujumbe huu nakusihi chukua hatua stahiki kwani siku zote neno la Rais ni sheria.

Mheshimiwa Rais, corona sio tena kaugonjwa kama ulivyo uita hapo awali kwani mpaka saivi tayari imesha kuonyesha rangi yake halisi.

Mheshimiwa Rais, jitokeza sasa utoe japo tamko dogo tu la watu kuvaa japo barakoa (facemask) kwa nchi nzima, kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kupunguza maambukizi ya virusi hivi. Acha kuwaachia wakuu wa mikoa kwani kuna wakuu wa mikoa tayari wamesha poteza muelekeo hawajui cha kufanya.

Mheshimiwa Rais, nchi saivi haina tena amani kama ulivyo zoea kulitamka hili neno kwenye mikutano yako kwani tumevamiwa na adui asiye onekana hivyo inahitaji akili kubwa kumshinda.

Mheshimiwa Rais, najua zoezi la kuwaweka wananchi wote ndani ( lockdown) ni ngumu kwako kutokana na maswala ya kiuchumi (na mimi kwa hili nakuunga mkono kwa asilimia mia). Ila jaribu kuweka mazingira salama ya wananchi wako huko wanapo jitafutia liziki zao ili tusiendelee kuongeza tatizo juu ya tatizo.

Mheshimiwa Rais, ni vitu vidogo tu vya kuwekea mkazo kupambana na ugonjwa huu kama:

- Uvaaji wa barakoa (facemask) kwa kila mwananchi.

- Vyombo vya usafiri kuzingatia sheria za usafi na kupunguza mibanano ndani ya gari. Hii izingatiwe nchi nzima hata kule vijijini

- Kuwe na timu za unyunyiziaji dawa kila sehemu inayo kaliwa na watu wengi kama stendi za mabasi na sehemu nyingine kama hizo (hapa nahisi lile jeshi lako pendwa la JKT litafaa zaidi katika operesheni hii kwani halijawahi kushindwa katika operesheni zake )

- Weka muda wa mwisho wa watu kufanya kazi ili kupisha operesheni hii ya kupiga dawa sehemu husika ili lifanikiwe zaidi.

- Panapo wezekana watu kunawa mikono naomba hilo suala lifanyike kwa usimamizi mkali sana. Sehemu kama kuingia masoko makuu na stendi kubwa kubwa inawezekana kabisa zoezi hili kufanyika kwani sehemu hizi huwa na sehemu zake maalum za kuingia na kutoka.

Mheshimiwa Rais, huu ndio muda muafaka sasa wa kutumia jeshi la polisi kulinda raia wake. Inawezekana polisi wakawa wachache katika kusimamia hili jukumu kutokana na nchi yetu ilivyo kubwa Lakini hili sisi wananchi halituhusu sana maana jukumu la kuajiri polisi kila mwaka ni lako kama ulifanya uzembe ndio ujifunze sasa kuwa nchi inahitaji polisi wa kutosha.

Mheshimiwa Rais, nimekueleza hayo kwani ukitamka wewe litatekelezwa kwa asilimia kubwa kuliko kuwaachia hao watendaji wako ambao matamko yao yanapishana kila kukicha.

Kwa kukukumbusha tu mheshimiwa Rais usijiaminishe sana na amani iliyopo kwenye nchi kwani siku zote kutoka kwenye amani kuja kwenye vita huwa ni kasi ya 5G. Na kutoka kwenye vita kurudi kwenye Aman huwa ni spidi ya kobe.

CHUKUA HATUA MAPEMA.
 
Ushauri mzuri kabisa, ila umesahau point moja ya kupiga marufuku mikusanyiko isiyo ya ulazima ikkwezeka shughuli za Bar na ibada zote zipigwe marufuku hii itasaidia sana...

Ama anaweza kwenda mbali zaidi akapiga marufuku ya vyombo vya usafiri hasa madalala maana siti kutoka mtu mmoja kwenda mwingine sidhani kama inafika mita moja...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ndio kashindwa maana wengi wamemshauri, nahisi ndio vitu anavyo hisi vikifanyika uchumi utayumba zaidi. Hivyo nimeona nimshauri hivi vidogo vidogo Lakin vitaleta matokeo chanya.
Ushauri mzuri kabisa, ila umesahau point moja ya kupiga marufuku mikusanyiko isiyo ya ulazima ikkwezeka shughuli za Bar na ibada zote zipigwe marufuku hii itasaidia sana...

Ama anaweza kwenda mbali zaidi akapiga marufuku ya vyombo vya usafiri hasa madalala maana siti kutoka mtu mmoja kwenda mwingine sidhani kama inafika mita moja...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee wa watu mtamlalamikia Bure tu. Kila kitu ulichokisema mtoa Mada ameshakisema Waziri Ummy na hata Ukigoogle unapata njia jinsi ya kujikinga au hata redioni kote elimu inatolewa. Ni utekelezaji tu. Sidhani kama akisema Rais anything will change au wagonjwa watapungua. Kujilinda ni jukumu lako binafsi.


Kuhusu mikusanyiko ni akili kumkichwa mkuu. Kama unaona Hali inazidi kuzorota kaa ndani km huwezi Toka lakini uwe makini. Sasa hadi Hilo kweli Rais atoke Chato aje kukwambia? Au Raha yako umsikie mtu mzee baba anazungumza.

Anyway Be Safe.
 
Enyi watanzania muacheni Jiwe apumzike zake juu ya Mawe huko aliko, kila mtu apambane kivyake.
 
Jiwe ni muoga haijapata kutokea. Hafai kuwa amirijeshi. Ikitokea nchi iko vitani atakimbia nchi atuache tunateketea.
 
Mzee wa watu mtamlalamikia Bure tu. Kila kitu ulichokisema mtoa Mada ameshakisema Waziri Ummy na hata Ukigoogle unapata njia jinsi ya kujikinga au hata redioni kote elimu inatolewa. Ni utekelezaji tu. Sidhani kama akisema Rais anything will change au wagonjwa watapungua. Kujilinda ni jukumu lako binafsi.


Kuhusu mikusanyiko ni akili kumkichwa mkuu. Kama unaona Hali inazidi kuzorota kaa ndani km huwezi Toka lakini uwe makini. Sasa hadi Hilo kweli Rais atoke Chato aje kukwambia? Au Raha yako umsikie mtu mzee baba anazungumza.

Anyway Be Safe.
L



Kama hayo yote yamesemwa na Wasaidizi wake,

Yeye atoke na aseme kuwa " CORONA SIYO KAUGONJWA KADOGO TENA, LIMEKUWA GONJWA BALAA, HATARI NA LINATISHA PIA ASEME NINI KIFANYIKE ILI WATANZANIA WAPONE
 
Amesema tusali
Pay attention to what you’re dwelling on. Don’t just think of anything that comes to mind. If it’s negative, discouraging, fearful, don’t give it the time of day. Turn it around and dwell on what God says about you .Joel Osteen
 
nashauri latra watoe vibali vya muda kwa magari binafsi na yale ya shule kubeba abiria kipindi hiki hasa jijini daresalaam maana kuna uhaba wa usafiri hasa asubuhi na.jioni, hivyo kufanya abiria kupandia gari njiani kwa kugombania bila kunawa mikono wala kupaka sanitizer..kipindi hiki ingefaa sana abiria wote kupandia gari vituo husika tena kwa foleni baada ya.kunawa mikono ama kupaka sanitizer...muhimu usimamizi.uwe mkali maana hali sio nzuri..
 
Kabla ya yote mtanisamehe katika uandishi wangu, lakini huu ndio ujumbe wangu kwa Mheshimiwa Magufuli.

Mheshimiwa Rais, popote usomapo ujumbe huu nakusihi chukua hatua stahiki kwani siku zote neno la Rais ni sheria.

Mheshimiwa Rais, corona sio tena kaugonjwa kama ulivyo uita hapo awali kwani mpaka saivi tayari imesha kuonyesha rangi yake halisi.

Mheshimiwa Rais, jitokeza sasa utoe japo tamko dogo tu la watu kuvaa japo barakoa (facemask) kwa nchi nzima, kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kupunguza maambukizi ya virusi hivi. Acha kuwaachia wakuu wa mikoa kwani kuna wakuu wa mikoa tayari wamesha poteza muelekeo hawajui cha kufanya.

Mheshimiwa Rais, nchi saivi haina tena amani kama ulivyo zoea kulitamka hili neno kwenye mikutano yako kwani tumevamiwa na adui asiye onekana hivyo inahitaji akili kubwa kumshinda.

Mheshimiwa Rais, najua zoezi la kuwaweka wananchi wote ndani ( lockdown) ni ngumu kwako kutokana na maswala ya kiuchumi (na mimi kwa hili nakuunga mkono kwa asilimia mia). Ila jaribu kuweka mazingira salama ya wananchi wako huko wanapo jitafutia liziki zao ili tusiendelee kuongeza tatizo juu ya tatizo.

Mheshimiwa Rais, ni vitu vidogo tu vya kuwekea mkazo kupambana na ugonjwa huu kama:

==uvaaji wa barakoa (facemask) kwa kila mwananchi.

==vyombo vya usafiri kuzingatia sheria za usafi na kupunguza mibanano ndani ya gari. Hii izingatiwe nchi nzima hata kule vijijini

==kuwe na timu za unyunyiziaji dawa kila sehemu inayo kaliwa na watu wengi kama stendi za mabasi na sehemu nyingine kama hizo (hapa nahisi lile jeshi lako pendwa la JKT litafaa zaidi katika operesheni hii kwani halijawahi kushindwa katika operesheni zake )

== Weka muda wa mwisho wa watu kufanya kazi ili kupisha operesheni hii ya kupiga dawa sehemu husika ili lifanikiwe zaidi.

== Panapo wezekana watu kunawa mikono naomba hilo suala lifanyike kwa usimamizi mkali sana. Sehemu kama kuingia masoko makuu na stendi kubwa kubwa inawezekana kabisa zoezi hili kufanyika kwani sehemu hizi huwa na sehemu zake maalum za kuingia na kutoka.

Mheshimiwa Rais, huu ndio muda muafaka sasa wa kutumia jeshi la polisi kulinda raia wake. Inawezekana polisi wakawa wachache katika kusimamia hili jukumu kutokana na nchi yetu ilivyo kubwa Lakini hili sisi wananchi halituhusu sana maana jukumu la kuajiri polisi kila mwaka ni lako kama ulifanya uzembe ndio ujifunze sasa kuwa nchi inahitaji polisi wa kutosha.

Mheshimiwa Rais, nimekueleza hayo kwani ukitamka wewe litatekelezwa kwa asilimia kubwa kuliko kuwaachia hao watendaji wako ambao matamko yao yanapishana kila kukicha.

Kwa kukukumbusha tu mheshimiwa Rais usijiaminishe sana na amani iliyopo kwenye nchi kwani siku zote kutoka kwenye amani kuja kwenye vita huwa ni kasi ya 5G. Na kutoka kwenye vita kurudi kwenye Aman huwa ni spidi ya kobe.

CHUKUA HATUA MAPEMA.
Mwezi mzima yuko kijjijini, ni vema kila mtu ajichukulie hatua
 
Back
Top Bottom