Rais Magufuli na Waziri Mkuu wafanya ziara ya kushtukiza kwa Makamu wa Rais

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Haifahamiki kwa nje (officially) kilichokuwa kinaongewa na viongozi wetu wakuu wa nchi lakini duru za kisiasa za ndani zinasema, Suala la Baraza la Mawaziri lilikuwa kwenye ajenda!

Ikumbukwe kuwa, siku moja kabla ya Waziri Mkuu, Majaliwa hajafanya ziara ya kushtukiza bandarini Dar es Salaam na kuwaita maofisa wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kikaoni kujadili changamoto kuhusu ufanisi na mapato alikutana na Rais Magufuli kwenye ofisi yake.

Tusishangae kesho kama tutasikia serikali ya Rais Magufuli ikiwashangaza tena watanzania kwa tukio lingine la kihistoria.

The man is on mission!

2%2B%25281%2529.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, (kushoto) akizungumza na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, wakati Rais na Waziri Mkuu walipomtembelea Makamu Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015 kwa mazungumzo.
3.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (kushoto) akiagana na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa (kulia) baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015. Wa pili (kulia) ni Naibu Katibu wa Makamu wa Rais, Mohamed Khamis.
 
katibu mkuu kiongozi ampeiga ''marufuku matumizi ya gharama kama kununua card na calendar''
Hayo maua mezani yanaangukia eneo gani!
 
katibu mkuu kiongozi ampeiga ''marufuku matumizi ya gharama kama kununua card na calendar''
Hayo maua mezani yanaangukia eneo gani!

Maua huwa ni ya mama mwenye ofisi kama vile uyakutayo mezani nyumbani kwako yanewekwa na mama wa nyumba bunch kama lile buku tano tu na linakaa hata siku 4
karibu namanga kama upo pande za dar ujipatie ya kuweka ofisini kwako.
 
katibu mkuu kiongozi ampeiga ''marufuku matumizi ya gharama kama kununua card na calendar''
Hayo maua mezani yanaangukia eneo gani!

Hahahahaa daah mzee kwa nini unauliza maswali ya kichokozi namna hiyo?

Hahahahaa....
 
katibu mkuu kiongozi ampeiga ''marufuku matumizi ya gharama kama kununua card na calendar''
Hayo maua mezani yanaangukia eneo gani!
Kwa hiyo wewe unadhani kama aliyakuta baada ya kuingia ofisini basi ayatupe kwa sababu Katibu Mkuu amepiga marufuku ununuzi wa kadi na kalendar.

Hivi hizi fikra mnazitoa wapi?

Nadhani ungetumia hata fikra kidogo na kujiuliza kwanza kama hayo maua ameyanunua yeye au ameyakuta baada ya kuwa Makamu wa Rais.

Tatizo ni kwamba, kwa sasa serikali ya Rais Magufuli is walking the talk. Nafasi za uanaharakati kama zako hazina nafasi kwa sasa.

Mtamkumbuka sana Rais Kikwete aliyewawezesha wanaharakati kama wewe kupata hoja kutokana na utendaji wa serikali yake.
 
Maua huwa ni ya mama mwenye ofisi kama vile uyakutayo mezani nyumbani kwako yanewekwa na mama wa nyumba bunch kama lile buku tano tu na linakaa hata siku 4
karibu namanga kama upo pande za dar ujipatie ya kuweka ofisini kwako.
Thanks, nitakuja
 
Kwa hiyo wewe unadhani kama aliyakuta baada ya kuingia ofisini basi ayatupe kwa sababu Katibu Mkuu amepiga marufuku ununuzi wa kadi na kalendar.

Hivi hizi fikra mnazitoa wapi?

Nadhani ungetumia hata fikra kidogo na kujiuliza kwanza kama hayo maua ameyanunua yeye au ameyakuta baada ya kuwa Makamu wa Rais.

Tatizo ni kwamba, kwa sasa serikali ya Rais Magufuli is walking the talk. Nafasi za uanaharakati kama zako hazina nafasi kwa sasa.

Mtamkumbuka sana Rais Kikwete aliyewawezesha wanaharakati kama wewe kupata hoja kutokana na utendaji wa serikali yake.
Jamani hasira za nini? Nimeuliza tu maana kwa elimu yangu inaweza kuwa sikujua mambo ya ofisi

Ahsante kunifahamisha, wala hakuna tatizo. Mbona mnakuwa mbogo, tuulize akina nani kama si wana jamvi

'Walk the talk'
 
Jamani hasira za nini? Nimeuliza tu maana kwa elimu yangu inaweza kuwa sikujua mambo ya ofisi

Ahsante kunifahamisha, wala hakuna tatizo. Mbona mnakuwa mbogo, tuulize akina nani kama si wana jamvi

'Walk the talk'
Siyo suala la kuuliza tu bali anauliza kwa kutumia logic gani?

'Talk sense'
 
Hahahahaa daah mzee kwa nini unauliza maswali ya kichokozi namna hiyo?

Hahahahaa....
Bwana weeee! ninashambuliwa utadhani nimekwepa kodi

Nilikuwa nafikiria tu jinsi ya kubana matumizi. Nikakumbuka 'walk the talk'

Nashambuliwa sana, sijui niombe radhi kwa kuuliza kaswali hako ka kipuuzi au
 
Kwa hiyo wewe unadhani kama aliyakuta baada ya kuingia ofisini basi ayatupe kwa sababu Katibu Mkuu amepiga marufuku ununuzi wa kadi na kalendar.

Hivi hizi fikra mnazitoa wapi?

Nadhani ungetumia hata fikra kidogo na kujiuliza kwanza kama hayo maua ameyanunua yeye au ameyakuta baada ya kuwa Makamu wa Rais.

Tatizo ni kwamba, kwa sasa serikali ya Rais Magufuli is walking the talk. Nafasi za uanaharakati kama zako hazina nafasi kwa sasa.

Mtamkumbuka sana Rais Kikwete aliyewawezesha wanaharakati kama wewe kupata hoja kutokana na utendaji wa serikali yake.

Umenisaidia kumjibu maana nlikuwa nafikiria kitu kibaya cha kumjibu
 
Back
Top Bottom