Rais Magufuli na Waziri Kamwelwe fanyeni haya juu ya zuio la ndege za Tanzania kwenda Kenya

Ngokongosha

JF-Expert Member
Feb 9, 2011
3,402
7,567
Nawapongeza kwa hatua zilizochukuliwa za kuzuia ndege za Kenya kutua nchini. Sitaki kuwachosha na maneno mengi, ila nimeona mazungumzo yameanza kurejesha safari, mimi nina wazo hili.

Kwa kuwa kenya wameanzisha utaratibu wa kutubeep, tukiwapigia wanaomba tuongee tuyamalize, mimi nashauri ili kuwapa funzo tusiruhusu mazungumzo yoyote mpaka ile deadline iliowekwa na TCAA itapofika, yaani Oktoba.

Hii itawapa funzo siku nyingine waache kutubeep au kuchukua maamuzi ya hovyo. Tukiendelea kuwa tunakubali kukaa mezani wataendelea na hii tabia na kuna siku watafanya jambo ambalo litatuathiri na hata kama tukikaa mezani bado litatuacha sisi na madhara.
 
Ni wakati sasa Dodoma ije na kauli ya kidiplomasia yenye mrengo wa kuionya Nairobi dhidhi ya hii tabia ambayo imekuwa ikijirudia rudia.
 
Back
Top Bottom