Rais Magufuli na utawala uliojaa uadilifu na mapenzi ya hali ya juu kwa raia wako

Tunkamanin

JF-Expert Member
Feb 27, 2015
951
865
Kupenda uadilifu na kuchukia ufisadi, kupenda haki na kuchukia unyanyasaji, ni mambo ambayo kiongozi wetu wa nchi anayo na nani basi asiyelifahamu jambo hilo kwa Mh. wetu? Lakini je kupenda peke yake, au kuchukia peke yake ndio lengo lake? jibu hapana......

Najua Rais wangu anaumiza kichwa, halali usingizi ukanoga, hali chakula kikaingia vizuri tumboni, anatafuta namna ya kufikia uadilifu wa kiwango cha juu, anatafuta namna ya kuweka hisia zake katika vitendo ili kuwasaidia wananchi wa Tanzania.

Naam hapo ndipo ulipo ugumu, unachukia ufisadi, je unauondoaje? unataka watoto wa tanzania wasome bila Bughudha, je unafanyaje ili wafikie hapo? Unataka kueneza uadilifu katika jamii, wanyonge wawe daraja sawa na watawala, hayo yote ni mambo tunayoyataka.

Amini hakuna jipya katika dunia ambalo waliopita kabla yetu hawajafanya, wapo viongozi waadilifu mno walipita katika ulimwengu huu, wakaeneza haki, usawa , uadilifu, neema na baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu zikaenea katika ardhi zao.

Hazina kubwa ipo kwenye vitabu, mimi naweka historia hapa ya Sayidnaa Umar, huyu alifanikiwa kueneza uadilifu na kupambana na ufisadi angalia namna alivyoongoza, utajifunza kitu.

Siku moja alishawahi kusema baada ya tumbo lake kutoa sauti kwa ajili ya njaa " Alisema wewe tumbo, nakuapia kuwa hutakaa uonje nyama mpaka watoto wa nchi hii watakapo shiba" speech yake wakati anapokea madaraka ilikua hivi.

Tukumbuke kuwa huyu alikua kiongozi wa nchi ya kiislamu kipindi hicho lakini yako mengi ya kujifunza hata kama ni wa dini nyingine.

upload_2016-11-20_0-51-0.jpeg
upload_2016-11-20_0-52-9.jpeg
 

Attachments

  • Umar-Ibn-Al-khattab-Volume-1.pdf
    13.9 MB · Views: 151
Uadilifu gani kuweka wakuu wa mikoa tisa wote kabila lake la wasukuma na wengine tisa Makabila ya kanda ya ziwa halafu watanzania wengine makabila 120 yanagombea nafasi 12. Huoni kama huo ni ukabila
 
Kupenda uadilifu na kuchukia ufisadi, kupenda haki na kuchukia unyanyasaji, ni mambo ambayo kiongozi wetu wa nchi anayo na nani basi asiyelifahamu jambo hilo kwa Mh. wetu? Lakini je kupenda peke yake, au kuchukia peke yake ndio lengo lake? jibu hapana......Najua Rais wangu anaumiza kichwa, halali usingizi ukanoga, hali chakula kikaingia vizuri tumboni, anatafuta namna ya kufikia uadilifu wa kiwango cha juu, anatafuta namna ya kuweka hisia zake katika vitendo ili kuwasaidia wananchi wa Tanzania. Naam hapo ndipo ulipo ugumu, unachukia ufisadi, je unauondoaje? unataka watoto wa tanzania wasome bila Bughudha, je unafanyaje ili wafikie hapo? unataka kueneza uadilifu katika jamii, wanyonge wawe daraja sawa na watawala, hayo yote ni mambo tunayoyataka.

...
Hii ni fyokofyoko au maono?
Ujumbe umeshamfikia.

Maisha ya "kimalaika" kwa mwendo kasi. Hapana kazi tu.
 
Hivi sijajua hiyo haki gani anafanya huyo rais wako watu wanalala nje wako katika shida baada ya tetemeko la ardhi na watu na mashirika mbalinbali yamechanga hajali shida za wananchi wake atajali nini tena haki gani aliyonayo zaidi ya ubabe ngoja ninyamaze nazidi pata hasira
 
Tatizo la watanzania wenzangu hasa wa karne hizi hatujui kushauri, ndio maana hata ushauri wetu mzuri hauchukuliwi, hatujui kukosoa kwa sababu hata kosoa yetu haina maadili. Hakuna binaadamu anapenda maneno ya karaha, dharau, kejeli, hata kama binaadamu huyo anapnda kukosolewa seuze Rais wa nchi, viongozi wana namna zao za kuwafikishia ujumbe na si hivyo ambavyo mmezoea, mkiweza kutegua kitendawili hicho na mkabadilika nadhani mtazungumza lugha moja.

Angalia zaidi mazuri yake hata kama mabaya anayo.........mshukuru na mpongeze kwa alipoweza kisha weka lako unalotaka kumshauri aongezee, hapo utakuwa unamtia moyo na humkatishi tamaa.

Angalia heshma yake kwa jamii, kama kiongozi wa nchi, kama si hivyo basi stahi zile nywele zake zilizoanza kupata weupe.

Onesha ari na nia nzuri ya kurekebisha au kukosoa kwa lengo la kumsaidia kujenga sio kumkosoa kwa kumbomoa.

HEKMA NI KUWEKA MANENO SAHIHI KWA WAKATI SAHIHI KATIKA SEHEMU SAHIHI.

"Aliyepewa hekma miongoni mwenu basi amepewa kitu kikubwa." Qur-anil kareem.
 
Kupenda uadilifu na kuchukia ufisadi, kupenda haki na kuchukia unyanyasaji, ni mambo ambayo kiongozi wetu wa nchi anayo na nani basi asiyelifahamu jambo hilo kwa Mh. wetu? Lakini je kupenda peke yake, au kuchukia peke yake ndio lengo lake? jibu hapana......

Najua Rais wangu anaumiza kichwa, halali usingizi ukanoga, hali chakula kikaingia vizuri tumboni, anatafuta namna ya kufikia uadilifu wa kiwango cha juu, anatafuta namna ya kuweka hisia zake katika vitendo ili kuwasaidia wananchi wa Tanzania.

Naam hapo ndipo ulipo ugumu, unachukia ufisadi, je unauondoaje? unataka watoto wa tanzania wasome bila Bughudha, je unafanyaje ili wafikie hapo? Unataka kueneza uadilifu katika jamii, wanyonge wawe daraja sawa na watawala, hayo yote ni mambo tunayoyataka.

Amini hakuna jipya katika dunia ambalo waliopita kabla yetu hawajafanya, wapo viongozi waadilifu mno walipita katika ulimwengu huu, wakaeneza haki, usawa , uadilifu, neema na baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu zikaenea katika ardhi zao.

Hazina kubwa ipo kwenye vitabu, mimi naweka historia hapa ya Sayidnaa Umar, huyu alifanikiwa kueneza uadilifu na kupambana na ufisadi angalia namna alivyoongoza, utajifunza kitu.

Siku moja alishawahi kusema baada ya tumbo lake kutoa sauti kwa ajili ya njaa " Alisema wewe tumbo, nakuapia kuwa hutakaa uonje nyama mpaka watoto wa nchi hii watakapo shiba" speech yake wakati anapokea madaraka ilikua hivi.

Tukumbuke kuwa huyu alikua kiongozi wa nchi ya kiislamu kipindi hicho lakini yako mengi ya kujifunza hata kama ni wa dini nyingine.

View attachment 436632View attachment 436634
Nitakuwa mtu wa Mwisho kukuunga Mkono.... Kwakuwa hiyo dhamira sijaona bado. Hata dhamira butu sijaiona!
 
Nitakuwa mtu wa Mwisho kukuunga Mkono.... Kwakuwa hiyo dhamira sijaona bado. Hata dhamira butu sijaiona!
Kwa kweli kwa matendo na maneno yanayodhihiri kila uchao ni vigumu kuamini kuwa kuna mapenzi mema na wanyonge! Hata hivyo ni woga wetu wenye unaotufanya tuendelee kuvumilia maumivu.
 
Kwa kweli kwa matendo na maneno yanayodhihiri kila uchao ni vigumu kuamini kuwa kuna mapenzi mema na wanyonge! Hata hivyo ni woga wetu wenye unaotufanya tuendelee kuvumilia maumivu.
Nchi imejaa wanafiki wa Kila Aina,ni ngumu mkiendelea sisi. Tumerudishwa kwenye mfumo wa Zidumu fikra za mwenyekiti...
 
Back
Top Bottom