Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,571
Wanabodi,
Salaam.
Moja ya vipindi vipindi bora kabisa vya TV vya mazungumzo (TV Talk Show) hapa nchini kwetu Tanzania ni kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari kinachorushwa live na Star TV, kila siku za Jumamosi asubuhi, kikiendeshwa na mtangazaji nguli na mahiri Dotto Emmanuel Bulendu (ambaye pia ni mhadhiri mwandamizi wa SAUT), kwa upande wa Mwanza, na mkongwe nguli Angalieni Mpendu kwa upande wa Dar es Salaam kikijikita kwa yanayojiri kwenye tasnia ya Habari kwa wiki nzima ambapo waandishi mbalimbali wa habari hukaribishwa kuchangia.
Kwenye kipindi cha leo, hoja kuu ilitojadiliwa ni jukumu la vyombo vya habari, kama jicho la jamii, kumkosoa rais Magufuli na kuikosoa serikali pale ambapo inafanya makosa kwa lengo la kuisaidia kujirekebisha.
Jee ukosoaji huu ufanyike namna gani?.
Wachangia mada wameshauri media kama media inatakiwa kuwa impartial kwa kutoegemea upande wowote hivyo rais Magufuli na serikali yake, wakifanya mazuri wapongezwe na wakifanya makosa tumkosoe Magufuli na serikali yake kwa hoja na sio kwa viroja au vijembe. Ukosoaji ufanyike with objectivity na kwa lugha ya heshima na staha na sio kwa lugha ya machukizo, maudhi au kutukana, na ukosoaji huo pia ufanyike constructively kwa nia ya kujenga na sio kubomoa, yaani "contructive criticism".
Mwendeshaji Dotto Bulendu amenigusa sana aliposema huku kwenye mitandao ya kijamii wengi wameegemea upande fulani, wale wa kusifu kazi yao ni kusifu tuu hata madhaifu ya wazi wao watasifu tuu, na wale wa kukosoa kazi yao ni kukosoa na kubeza tuu kila kitu, hata Magufuli afanye mazuri vipi au serikali ifanye mazuri gani wao watabeza tuu.
Sasa wanapojitokeza watu objective na impartial ambao kwenye mazuri watasifu na kwenye mabaya watakosoa, siku wakisifu, wale wakosoaji watawanyooshea vidole kuwa ni upande wa CCM na serikali na siku wakikosoa wale wasifuji tuu watawanyooshea kidole kuwa wao ni wapinzani.
Kiukweli hili alilolisema Dotto Bulendu lipo sana humu jf, kuna watu kazi yao ni kumkosoa tuu na kupinga kila kitu kinachofanywa na Awamu ya Tano, hata kiwe kizuri vipi. Na kuna wengine kazi yao kusifu tuu hata serikali iboronge vipi wao watasifu tuu.
Hali hii impelekea sisi tunaochangia kwa kusifia mazuri na kwenye mabaya tunakosoa huwa tunashutumiwa kwa kunyooshewa vidole kuwa hatueleweki, siku tukisifu tunaitwa CCM, siku tukikosoa tunaitwa wapinzani.
Jee hatuwezi sisi wana jf wote tukawa more objective kwenye kumsifu au kumkosoa Magufuli na serikali yake kwa hoja na sio kwa viroja bila kunyoosheana vidole?.
Paskali
Rejea
Mwito Kwa Wana JamiiForums Kuhusu Ukosoaji wa Rais Magufuli
Salaam.
Moja ya vipindi vipindi bora kabisa vya TV vya mazungumzo (TV Talk Show) hapa nchini kwetu Tanzania ni kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari kinachorushwa live na Star TV, kila siku za Jumamosi asubuhi, kikiendeshwa na mtangazaji nguli na mahiri Dotto Emmanuel Bulendu (ambaye pia ni mhadhiri mwandamizi wa SAUT), kwa upande wa Mwanza, na mkongwe nguli Angalieni Mpendu kwa upande wa Dar es Salaam kikijikita kwa yanayojiri kwenye tasnia ya Habari kwa wiki nzima ambapo waandishi mbalimbali wa habari hukaribishwa kuchangia.
Kwenye kipindi cha leo, hoja kuu ilitojadiliwa ni jukumu la vyombo vya habari, kama jicho la jamii, kumkosoa rais Magufuli na kuikosoa serikali pale ambapo inafanya makosa kwa lengo la kuisaidia kujirekebisha.
Jee ukosoaji huu ufanyike namna gani?.
Wachangia mada wameshauri media kama media inatakiwa kuwa impartial kwa kutoegemea upande wowote hivyo rais Magufuli na serikali yake, wakifanya mazuri wapongezwe na wakifanya makosa tumkosoe Magufuli na serikali yake kwa hoja na sio kwa viroja au vijembe. Ukosoaji ufanyike with objectivity na kwa lugha ya heshima na staha na sio kwa lugha ya machukizo, maudhi au kutukana, na ukosoaji huo pia ufanyike constructively kwa nia ya kujenga na sio kubomoa, yaani "contructive criticism".
Mwendeshaji Dotto Bulendu amenigusa sana aliposema huku kwenye mitandao ya kijamii wengi wameegemea upande fulani, wale wa kusifu kazi yao ni kusifu tuu hata madhaifu ya wazi wao watasifu tuu, na wale wa kukosoa kazi yao ni kukosoa na kubeza tuu kila kitu, hata Magufuli afanye mazuri vipi au serikali ifanye mazuri gani wao watabeza tuu.
Sasa wanapojitokeza watu objective na impartial ambao kwenye mazuri watasifu na kwenye mabaya watakosoa, siku wakisifu, wale wakosoaji watawanyooshea vidole kuwa ni upande wa CCM na serikali na siku wakikosoa wale wasifuji tuu watawanyooshea kidole kuwa wao ni wapinzani.
Kiukweli hili alilolisema Dotto Bulendu lipo sana humu jf, kuna watu kazi yao ni kumkosoa tuu na kupinga kila kitu kinachofanywa na Awamu ya Tano, hata kiwe kizuri vipi. Na kuna wengine kazi yao kusifu tuu hata serikali iboronge vipi wao watasifu tuu.
Hali hii impelekea sisi tunaochangia kwa kusifia mazuri na kwenye mabaya tunakosoa huwa tunashutumiwa kwa kunyooshewa vidole kuwa hatueleweki, siku tukisifu tunaitwa CCM, siku tukikosoa tunaitwa wapinzani.
Jee hatuwezi sisi wana jf wote tukawa more objective kwenye kumsifu au kumkosoa Magufuli na serikali yake kwa hoja na sio kwa viroja bila kunyoosheana vidole?.
Paskali
Rejea
Mwito Kwa Wana JamiiForums Kuhusu Ukosoaji wa Rais Magufuli