MIKOPO YA WANAFUNZI ELIMU YA JUU
Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli imezidi kuonyesha namna inavyowajali Waafunzi wa elimu ya juu kwa kutoa mikopo zaidi kwa Wanafunzi waliokata rufaa na kuonekana wanastahili kupewa mikopo. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetangaza jumla ya wanafunzi 2679 waliofanikiwa kupata mkopo katika maombi yao ya rufaa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo, Abdul-RAzaq Badru, ameeleza kuwa kati ya wanafuzi 4200 waliokata rufaa, wanafunzi 2679 wamefanikiwa kupata mikopo yao katika mwaka wa masomo 2017/18.
Mkurugenzi Badru ameeleza kuwa kati ya wanafunzi hao 2769 waliopata mikopo, wanafunzi 1847 ni wa mwaka wa kwanza ambao mkopo wao umegharimu kiasi cha shilingi 6.84 bilioni na wanafunzi 832 waliobakia ni wa naoendelea (mwaka wa 2,3 na 4) ambao mkopo wao umegharimu shilingi 2.75 bilioni.
Ikumbukwe kwa mwaka huu wa 2017/18 Serikali ilianza kutoa mikopo ya elimu ya juu kwa Wanafunzi wa mwaka wa kwanza mnamo Oktoba 26, 2017. Kiasi cha shilingi bilioni 72.2 mpaka sasa kimetolewa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu wapatao 21,677 kati ya wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza waliopangwa kupatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 108.8 kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Abdul-Razaq Badru imesema kuwa idadi ya wanafunzi waliobaki wapatao 8,323watapangiwa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 36.6 katika awamu inayofuata ili kukamilisha idadi iliyopangwa.
Idadi ya wanafunzi 21,677 waliokwishapangiwa mikopo na ambao wamedahiliwa katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu vinavyotambulika; ni asilimia 72.2 ya wanafunzi 30,000wanaotarajiwa kunufaika na mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Awamu hii ya Dk. Magufuli ni awamu ya vitendo zaidi, ni awamu ya kazi tu. HAPA KAZI TU
Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli imezidi kuonyesha namna inavyowajali Waafunzi wa elimu ya juu kwa kutoa mikopo zaidi kwa Wanafunzi waliokata rufaa na kuonekana wanastahili kupewa mikopo. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetangaza jumla ya wanafunzi 2679 waliofanikiwa kupata mkopo katika maombi yao ya rufaa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo, Abdul-RAzaq Badru, ameeleza kuwa kati ya wanafuzi 4200 waliokata rufaa, wanafunzi 2679 wamefanikiwa kupata mikopo yao katika mwaka wa masomo 2017/18.
Mkurugenzi Badru ameeleza kuwa kati ya wanafunzi hao 2769 waliopata mikopo, wanafunzi 1847 ni wa mwaka wa kwanza ambao mkopo wao umegharimu kiasi cha shilingi 6.84 bilioni na wanafunzi 832 waliobakia ni wa naoendelea (mwaka wa 2,3 na 4) ambao mkopo wao umegharimu shilingi 2.75 bilioni.
Ikumbukwe kwa mwaka huu wa 2017/18 Serikali ilianza kutoa mikopo ya elimu ya juu kwa Wanafunzi wa mwaka wa kwanza mnamo Oktoba 26, 2017. Kiasi cha shilingi bilioni 72.2 mpaka sasa kimetolewa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu wapatao 21,677 kati ya wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza waliopangwa kupatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 108.8 kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Abdul-Razaq Badru imesema kuwa idadi ya wanafunzi waliobaki wapatao 8,323watapangiwa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 36.6 katika awamu inayofuata ili kukamilisha idadi iliyopangwa.
Idadi ya wanafunzi 21,677 waliokwishapangiwa mikopo na ambao wamedahiliwa katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu vinavyotambulika; ni asilimia 72.2 ya wanafunzi 30,000wanaotarajiwa kunufaika na mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Awamu hii ya Dk. Magufuli ni awamu ya vitendo zaidi, ni awamu ya kazi tu. HAPA KAZI TU