Rais Magufuli na CCM waliwaahidi watanzania Katiba Mpya kabla ya 2020

Say no to actors

JF-Expert Member
Aug 9, 2016
637
640
Wadau ni matunaini yangu kuwa wazima wa buheri.


Leo napenda nidadavue juu ya majibu ya mkuu wetu wa nchi siku amekutana Na wahariri wa vyombo vya habari. Rais aliulizwa suala la katiba mpya lakini yeye majibu aliyotoa hayakuwa yenye uhalisia na wataalam wanasema yalikuwa ya uongo.

Kwanza nikili kuwa suala la katiba mpya liko kwenye ilani ya chama cha Mapinduzi, angalia ilani ya chama cha mapinduzi page 164 kipengele cha 145(g) inasema "Kukamilisha mchakato wa kutunga Katiba Mpya na kuanza kuitekeleza kwa mjibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba".

Screenshot 2018-11-02 at 20.07.39.png


Pia hili suala la kukamilisha mchakato cha katiba na kuanza kuitumia ndani ya 2015/2020 ni mojawapo ya maazimio ya mkutano mkuu wa CCM na ambayo yamewekwa pia kwenye ilani yao ya uchaguzi page 185 kipengele cha 183a kudumisha muungano ambapo CCM inaamini ndani ya katiba hii inayopendekezwa kero nyingi za muungano zimepatiwa majawabu ya kuridhisha.

Na ninakumbuka kipindi huyu ndugu amepitishwa na mkutano mkuu wa chama kama mgombea urais aliulizwa na waandishi wa habari juu ya kipaumbele chake na alisema ni ILANI YA CCM ya uchaguzi lakini leo hii anaisimanga na kusema si kipaumbele.

Na jambo la kushangaza chama nacho kimeshindwa kutekeleza wajibu wake kwa serikali. Kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi pg 188 Jukumu la CCM kipengele 187 "chama kina jukumu la kufuatilia utekelezaji wa ilani hii".

Chama leo kinacheza ngoma ya Rais Magufuli akisema leo hakuna kuvaa nguo za chama wote wananywea na hakuna wa kukohoa. Hakuna hata press conference ya CCM ya kujitokeza na kurekebisha kauli ya mtu wako. Au kumuita na kumwambia hapa unaenda kinyume na ilani.

Watanzania walidanganywa kupindi cha campaign kuwa mtuchague tutakamirisha katiba mpya nao wakawapatia kura na leo wanaambiwa ngoja kwanza tuwanyooshe ilani baadaye, na wao wasijiulize

- Je, tulikuwa tumepinda?
- Je kama tulikuwa tumepinda?
- Je, ukitunyoosha hatutovunjika?

NI GARI BOVU NA DREVA MLEVI HUKU KONDAKTA NI TEJA, Safari si salama.

Nawasilisha.
 
Wewe sio Mtanzania.

Nashangaa Wakenya kila kukicha kujifanya Watanzania na kushadadia mambo ya Tanzania.

Lugha inakusuta na kukuanika kua wewe sio Mtumiaji halisia wa lugha hii bali unalazimisha.

Mambo ya katiba waachie Watanzania, wewe tulia enjoy sukumawiki na kimbo.
 
Wewe sio Mtanzania.

Nashangaa Wakenya kila kukicha kujifanya Watanzania na kushadadia mambo ya Tanzania.

Lugha inakusuta na kukuanika kua wewe sio Mtumiaji halisia wa lugha hii bali unalazimisha.

Mambo ya katiba waachie Watanzania, wewe tulia enjoy sukumawiki na kimbo.


Haya tufanye yeye siyo Mtanzania, je mada aliyoleta ni kweli au si kweli? Tuanzie hapo kwanza...
 
Sawa katika ILANI ipo... Je 2020 na Ishirini imeshafika.. Miaka miwili inatumika kunyoosha nchi alafu 2020 kabla ya julai katiba mpya inatoka kabatini
 
Watu wagumu kuelewa Rais kasema, "lini katika kampeni mlimsikia akizungumzia katiba mpya?" Kwa maneno mengine pamoja na kuwa katiba mpya iko kwenye ilani ya ccm, haipo katika vipaumbele vyake. Kipaumbele ni kuiweka nchi kwenye mstari na katiba itakuja kwa wakati wake maana imetajwa kwenye ilani. Juzi tu hapa mmesahau kuna Rais alituambia mambo mengine ya ilani ya chama chake haya tekelezeki.

Na washawsha!
 
Wewe sio Mtanzania.

Nashangaa Wakenya kujifanya Watanzania na kushadadia mambo ya Tanzania.

Lugha uliotumia kufikisha ujumbe I


Wewe sio Mtanzania.

Nashangaa Wakenya kila kukicha kujifanya Watanzania na kushadadia mambo ya Tanzania.

Lugha inakusuta na kukuanika kua wewe sio Mtumiaji halisia wa lugha hii bali unalazimisha.

Mambo ya katiba waachie Watanzania, wewe tulia enjoy sukumawiki na kimbo.
Were ambae no mtanzania mbona huna lolote. Na ukubwa elimu Na kila mungu alichokupa bado huoni umuhimu was katiba ama kweli Tanzania tunahitaji elimu ya kujitambua kama bado watu hawajui umuhimu was katiba inayotokana Na maoni ya wao wenyewe no tatizo kubwa. Uliekosoa jamaa alichosema jitazame upya au unatatizo la kiundani zaidi ambalo huenda lonakuondolea uelewa was kawaida tu
 
Watu wagumu kuelewa Rais kasema, "lini katika kampeni mlimsikia akizungumzia katiba mpya?" Kwa maneno mengine pamoja na kuwa katiba mpya iko kwenye ilani ya ccm, haipo katika vipaumbele vyake. Kipaumbele ni kuiweka nchi kwenye msatari na katiba itakuja kwa wakati wake maana imetajwa kwenye ilani. Juzi tu hapa mmesahau kuna Rais alituambia mambo mengine ya ilani ya chama chake haya tekelezeki.

Na washawsha!
Kasikilize hutuba zake kwenye kampain utasikia. Usitetetee vibovu. Lakini jiuloze inamaana ukinyoosha inch vitu vingine vinasimama mana kama no hivo mawaziri Na watendaji was Nazi gani. Mana maendeleo yamesimama kabisa Na he anaowanyoosha anawapeleka wap mana tunaona anafagia lakn hatuoni taka anatupa wapi Na pia hatuoni akinunua vitu vipya sasa kazi kwa anaowafagia zinafanywa Na nan. Haya Sikh moja using ingize njia ya kutafuta eneo katika kutafuta mzingo japo zote no hesabu lakini matokeo yake mabovu. Kiukweli kama halii itaenda hivi had I 2018 tusianze kuuwa watoto kupunguza majukumu mana sion dalili yoyote ya kuweka uchumi vizur nyie tu shabikie tu but finally cc watu wa kawida kabisa ndio tutapata cha moto wabunge sio wenzetu mil10 zinawaelekea
 
Watu wagumu kuelewa Rais kasema, "lini katika kampeni mlimsikia akizungumzia katiba mpya?" Kwa maneno mengine pamoja na kuwa katiba mpya iko kwenye ilani ya ccm, haipo katika vipaumbele vyake. Kipaumbele ni kuiweka nchi kwenye msatari na katiba itakuja kwa wakati wake maana imetajwa kwenye ilani. Juzi tu hapa mmesahau kuna Rais alituambia mambo mengine ya ilani ya chama chake haya tekelezeki.

Na washawsha!
Hivi una akili sawasawa? Kila kitu mnataka kutetea tu? Hili alishalisema na sio mara moja.Tafuta hotuba zake yzisikilize usilete ukurupukaji humu.
 
Hivi una akili sawasawa? Kila kitu mnataka kutetea tu? Hili alishalisema na sio mara moja.Tafuta hotuba zake yzisikilize usilete ukurupukaji humu.

Hatutetei tuna sema Rais alichokisema basi, kwa nini unahangaika kumquote mtu asiye na akili sawasawa (mwehu) lakini?

Na washawasha!
 
Sawa katika ILANI ipo... Je 2020 na Ishirini imeshafika.. Miaka miwili inatumika kunyoosha nchi alafu 2020 kabla ya julai katiba mpya inatoka kabatini
Kauli ya mwenyekiti wako katiba baadae na inathibitishwa na waziri wake wa sheria mwakyembe kuwa katiba si kipaumbele cha magu
 
Hakuna ubaguzi wa fikra. Wenzetu wenye dola hawapendi kuhojiwa wala hawapendi fikra mbadala. Big up mleta mada. Hicho ni kiashiria kuwa uchwara si uchwara tu bali hamnazo.
 
Wewe sio Mtanzania.

Nashangaa Wakenya kujifanya Watanzania na kushadadia mambo ya Tanzania.

Lugha uliotumia kufikisha ujumbe I


Wewe sio Mtanzania.

Nashangaa Wakenya kila kukicha kujifanya Watanzania na kushadadia mambo ya Tanzania.

Lugha inakusuta na kukuanika kua wewe sio Mtumiaji halisia wa lugha hii bali unalazimisha.

Mambo ya katiba waachie Watanzania, wewe tulia enjoy sukumawiki na kimbo.
Wacha udwanzi wewe, hapa hoja sio rangi, kabila wala uraia wa mtu! Tunajuaje kwamba wewe sio mrundi hohehahe?! Hoja ya mleta mada ni
katiba mpya, kwamba swala hilo limo kwenye ilani ya ccm ambacho JPM ndio mwenyekiti wake na ni azimio muhimu kutoka vikao mahsusi vya ccm, sasa iweje Rais aliambie taifa kwamba hilo sio kipaumbele chake?! Inashangaza sana kuwa na kiongozi mkuu wa nchi asiyethamini katiba! Jikite kwenye mada, sio mihemuko yako ya kiitikadi; bs
 
Ukawa naona mambo yanawawia ugumu mnaweweseka itafikiri ng'ombe anayepelekwa mnadani huku kashikwa mkia
 
Back
Top Bottom