Rais Magufuli: Mtu akitaka kukiona cha moto ajaribu kumshambulia Mwana-CCM aliyevaa kijani

technically

JF-Expert Member
Jul 3, 2016
11,975
48,842
Rais Magufuli anasema kama mtu anataka kukiona cha moto ajaribu kumshambulia Mwana-CCM yeyote aliyevaa kijani.

--
MAONI YANGU

Mimi najiuliza, je wananchi wanaovaa kaki hawana haki ya kulindwa?

Tuna Rais mbaguzi sijawai kuona yaani wakina Mawazo mpaka waliuawa na watu kibao wanashambuliwa kisa wamevaa kaki hakuna hatua zinazochukuliwa.

Tuna Rais mbaguzi sana.
 
Magufuli ni Rais mzuri sana ila vitu vinavyomshushia hadhi ni vidogo vidogo sana

Anakosa utashi sio kama tu kiongozi bali kama gentleman

Lakini namkubali kwa kuwa ana uthubutu kwa mambo makubwa mapungufu yake ni hayo ya kugawa watu.
 
Magufuli ni rais mzuri sana ila vitu vinavyomshushia hadhi ni vidogo vidogo sana

Anakosa utashi sio kama tu kiongozi bali kama gentleman

lakini namkubali kwa kuwa ana uthubutu kwa mambo makubwa mapungufu yake ni hayo ya kugawa watu

Haya unaweza kuyaona ni madogo lakini madhara yake ni makubwa due tutafika stage tuanze ulizana makabila kama ilivyo kwa kenya ko umoja wetu hautakuwepo kwa ss hivi ni uhasama unajengwe tu miongoni mwa watu kwa kuona kuwa kundi moja linabebwa zaid kwao wataona kila wanachofanya ni sahihi hata kama ni kinyume na utaratibu
 
Magufuli ni rais mzuri sana ila vitu vinavyomshushia hadhi ni vidogo vidogo sana

Anakosa utashi sio kama tu kiongozi bali kama gentleman

lakini namkubali kwa kuwa ana uthubutu kwa mambo makubwa mapungufu yake ni hayo ya kugawa watu
Yaani mtu anayeongoza nchi yenye watu takiriban 60ml halafu hahubiri umoja wa watu wake uzuri wake unaona wapi mkuu! Kauli anazotoa haziendani kabisa na umoja walioasisi viongozi wetu.

Hivi leo hii watu wa Dodoma wawe na chuki na watu wa Mwanza hayo unayoyaona mazuri yanafaa nini?. Wanaosema ana upendo na huruma sijui wanaonaje

UPENDO hauna ubaguzi, hauna chuki, hauna husuda, hauna ubabe, hauna kiburi, hauna kisingizo, haujifanyi mtakatifu. Upendo humsikiliza kila mtu kwa unyenyekevu na upole
 
Huyu mzee sijui hua anafikiria nini kabla ya kuongea, juzi kaombwa msaada wa maji alieomba akaambiwa akamuombe mume wake, au diwani wake (upinzani) au mbunge wake (upinzani).

Leo anasema viongozi wawatumikie wananchi wote bila kubagua chama, itikadi, wala dini kwani manendeleo hayana vyama.

Leo tena anatoa KINGA kwa wanaovaa kijani (wanachama wa CCM).

#Hizi kampeni za uchaguzi wa urais #2020 zitasababisha tafrani kuelekea uchaguzi mkuu, tusubiri upinzani waanzishe amsha amsha kwenye uchaguzi mkuu kwa KUTUMIA KAULI ZA MKULU.
 
Kabla ya kuuliza hilo inabidi ujiulize ulishawahi kuona mtu kavaa kaki au gwanda akizomewa au kupigwa kwa ajili ya vazi?


Kama yupo mtaje tuanzie hapo, na kuhusu kupigana hilo ni suala lingine walishapiwa wa chadema na pia hivyo hivyo wa CCM walishapigwa ajili ya siasa hilo lipo., nadhani tatizo lipo mtu akivaa nguo ya kijani watu wanaanza kumtukana bila sababu hilo ndo nadhani anakemea.
 
Rais Magufuli anasema kama mtu anataka kukiona cha moto ajaribu kumshambulia Mwana-CCM yeyote aliyevaa kijani.

Mimi najiuliza, je wananchi wanaovaa kaki hawana haki ya kulindwa?

Tuna rais mbaguzi sijawai kuona yaani wakina mawazo mpaka waliuawa na watu kibao wanashambuliwa kisa wamevaa kaki hakuna hatua zinazochukuliwa.

Tuna Rais mbaguzi sana.
Tuna Rais mshamba sana!
 
Rais Magufuli anasema kama mtu anataka kukiona cha moto ajaribu kumshambulia Mwana-CCM yeyote aliyevaa kijani.

Mimi najiuliza, je wananchi wanaovaa kaki hawana haki ya kulindwa?

Tuna rais mbaguzi sijawai kuona yaani wakina mawazo mpaka waliuawa na watu kibao wanashambuliwa kisa wamevaa kaki hakuna hatua zinazochukuliwa.

Tuna Rais mbaguzi sana.
na muda huo-huo Lissu alishambuliwa kwa risasi 38 kwenye nyumba za serikali na hadi leo serikali imeficha kichwa kwenye mchanga kama mbuni jike.
 
Rais Magufuli anasema kama mtu anataka kukiona cha moto ajaribu kumshambulia Mwana-CCM yeyote aliyevaa kijani.

Mimi najiuliza, je wananchi wanaovaa kaki hawana haki ya kulindwa?

Tuna rais mbaguzi sijawai kuona yaani wakina mawazo mpaka waliuawa na watu kibao wanashambuliwa kisa wamevaa kaki hakuna hatua zinazochukuliwa.

Tuna Rais mbaguzi sana.

Aache kujiona kamungu kadogo.

Sasa kama mimi ni simba namzomea wa yanga nitakiona cha mtema kuni!?

Mbona tunatishana sana.

Hivi nchi hii kuna wengine wana haki na wengine hawana!?
 
Rais Magufuli anasema kama mtu anataka kukiona cha moto ajaribu kumshambulia Mwana-CCM yeyote aliyevaa kijani.

Mimi najiuliza, je wananchi wanaovaa kaki hawana haki ya kulindwa?

Tuna rais mbaguzi sijawai kuona yaani wakina mawazo mpaka waliuawa na watu kibao wanashambuliwa kisa wamevaa kaki hakuna hatua zinazochukuliwa.

Tuna Rais mbaguzi sana.
Harafu utashangaa anaalika viongozi wa dini kubadirishana nae ideas. Sijawahi kuacha kumuunga mkono Lowassa pamoja na mapungufu yake kibao
 
Magufuli ni rais mzuri sana ila vitu vinavyomshushia hadhi ni vidogo vidogo sana

Anakosa utashi sio kama tu kiongozi bali kama gentleman

lakini namkubali kwa kuwa ana uthubutu kwa mambo makubwa mapungufu yake ni hayo ya kugawa watu
Unajua ukweli ulio wazi kabisa huyu jamaa ana roho mbaya haijalishi natoka nae kanda moja. Mungu saidia tu atoke madarakani kabla hajatugawa na kuwa kama nchi jirani kwa tofauti zetu za kisiasa. Kinachonishangaza ni kwanini anaeneza chuki huku akifahamu hakuna upinzani na mpinzani wake mkuu yuko nje ya nchi baada ya kunusurika kifo
 
Back
Top Bottom