Rais Magufuli: Mtu akipotea, marufuku kuhusisha vyombo vya Dola, utakamatwa na utoe ushahidi

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
RAIS MAGUFULI "HUYO ANA USHAHIDI, MSHIKENI MPAKA ATOE USHAHIDI"

Siku hizi kumekuwa na tabia ya hovyo imejitokeza kwa baadhi ya Watanzania wachache. Kila kitu kinachofanywa ni Usalama wa Taifa, mtu akipotea siku mbili hata kama hajapotea yupo kwa mpenzi wake ni Usalama wa Taifa.

Niviombe vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama likiwemo Jeshi la Polisi ambao huwa mnashughulikia wahalifu, msiwaache wahalifu waanze kuchafua vyombo vya Ulinzi na Usalama. Mtu akizungumza amempotea huyu ana ushahidi mshikeni mpaka atoe ushahidi.

Mawazo yangu:

Kama hawahusiki waliopotea nani kawachukua? Wasiojulikana ni kina nani?

Crediti to Vitalis

Simple questions to ask yourself

Kwanini ni Usalama wa Taifa, kwanini tusiseme ni maharamia wa Kisomali, kwanini sio Al Shabab, Kwanini sio watu wengine wowote? Kwanini TISS?

Kama sio TISS kwanini sio hao niliotaja hapo juu ambao wangekwisha kamatwa?

Ni kwanini wanaitwa wasiojulikana?

Je, hayo majeshi ya vyombo vya ulinzi na usalama wamefeli kiasi hicho cha kutokamata hata mmoja?

Tujiulize majeshi yetu ni ya kukaa kambini tuu na kubaini wale wanaotaka kujinyonga siku za karibuni?

Majeshi yetu ni ya kubaini kuwa kutokana na intelijensia kwenye kikao au mkutano wa chama fulani kunategemewa kuwa na vurugu na badala yake kuzuia Kikao au mkutano?

USHAURI.

Majeshi ya Ulinzi na Usalama wao ndio wanatakiwa kutuhakikishia kuwa sio TISS kwa kukamata wale wote wasiojulikana ili jamii itokane na dhana hiyo.
 
Waliopo karibu ya Rais wanisaidie kuniulizia, hivi kazi ya police siku hizi ni nini? Yaani hata mimi nisipoonekana for two days, niwe nimefungiwa ndani na jimama au nguo zangu zimelowekwa na mchepuko, mama atakwenda police au popote anapoona anaweza kupata msaada kuriport kuwa nimepotea then ni jukumu la police kufanya uchunguzi na kutoa taarifa kama ni kweli nilikuwa nimepotea, nimetekwa au nilikuwa kwa hawara. shame on him
 
Ni sawa kabisa,tena itungwe sheria Kali dhidi ya vyombo vya habari vinavyohusika kutoa taarifa za uzushi kama hizi ili Iwe mwisho wa upuuzi huu,mtu amekamatwa let's say na polisi mijitu inasema ametekwa,mtu yuko offline kwa matatizo ya mtandao wanadai ametekwa,hatuwezi kufika kwa kuendekeza upuuzi kama huu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom