Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,239
- 9,527
Utu wa mtu ni jambo la msingi ambalo kwa ubinadamu wetu, bila kujali itikadi ya vyama vyetu au jinsi tunavyoonekana, wote tumezaliwa sawa na hakuna kigezo kwa yeyote kati yetu kuishi kwa manyanyaso.
Samahani ila, Kwa pamoja kama watanzania tumefanikisha mambo mengi kwa umoja ulioshikiliwa na heshima yetu kwa utu wa mtu. Tumeyafanikisha hayo kabla, ya uhuru, wakati wa uhuru na baada ya uhuru kwa lengo la kuhakikisha utu wa mtu unalindwa.
Tumepambana na magonjwa wakati wote huu bila kujali itikadi zetu kisiasa, tumechangia nchi nyingi kupata uhuru, na leo pamoja na mapungufu, bado tunapiga hatua kwenye elimu, tuna piga hatua watu watoke kwenye umasikini. Ila kazi yetu bado haijakamilika, na haitakamilika Kama tutarudi nyuma sana kwenye jambo lililompa Nyerere jina kimataifa. Jambo linayoyapa maisha ya binadamu wote maana, UTU WA MTU.
Leo watumishi wa umma wanaonekana hawana umuhimu, Mungu anipunguzie hasira maana baba na mama yangu ni watumishi na ningekuwa kinondoni wakati ule Makonda anawadhalilisha watumishi wa ardhi ningemkata mabanzi straight away!
Kuna mambo mengi ambayo bila umoja wetu kama watanzania hatuwezi kufanikisha kama tutaona hakuna uzito kwa mmoja kati yetu kudharauliwa na kudhalilishwa. Yupo kijana mmoja -Bouzine, ambaye alijiwasha kwenye historia ya majuzi kwaajili ya manyanyaso tu ya mgambo na nchi ikawaka, rais akaondoka madarakani.
Kitendo cha Makonda kuwadhalilisha watumishi wa ardhi kinondoni ni kitendo kinachoumiza dhamira za wengi, ni haki na usawa na utu wa mtu vilivyokanyagwa bila kipimo.
Magufuli turudishe pamoja kama taifa ili kutambua mabadiliko tunayoyataka. Sio kila mabadiliko ni maendeleo.
Leo tukitaka viwango vikubwa vya utendaji kwa kila mtu katika taifa tuanze na viongozi, tuanze na midomo yao. Mheshimiwa rais, tuanze na Makonda.
Ili mabadiliko yatokee, kila mtu afanye nafasi yake. Kwa hili mimi nimefanya yakwangu. Bado wewe!
Samahani ila, Kwa pamoja kama watanzania tumefanikisha mambo mengi kwa umoja ulioshikiliwa na heshima yetu kwa utu wa mtu. Tumeyafanikisha hayo kabla, ya uhuru, wakati wa uhuru na baada ya uhuru kwa lengo la kuhakikisha utu wa mtu unalindwa.
Tumepambana na magonjwa wakati wote huu bila kujali itikadi zetu kisiasa, tumechangia nchi nyingi kupata uhuru, na leo pamoja na mapungufu, bado tunapiga hatua kwenye elimu, tuna piga hatua watu watoke kwenye umasikini. Ila kazi yetu bado haijakamilika, na haitakamilika Kama tutarudi nyuma sana kwenye jambo lililompa Nyerere jina kimataifa. Jambo linayoyapa maisha ya binadamu wote maana, UTU WA MTU.
Leo watumishi wa umma wanaonekana hawana umuhimu, Mungu anipunguzie hasira maana baba na mama yangu ni watumishi na ningekuwa kinondoni wakati ule Makonda anawadhalilisha watumishi wa ardhi ningemkata mabanzi straight away!
Kuna mambo mengi ambayo bila umoja wetu kama watanzania hatuwezi kufanikisha kama tutaona hakuna uzito kwa mmoja kati yetu kudharauliwa na kudhalilishwa. Yupo kijana mmoja -Bouzine, ambaye alijiwasha kwenye historia ya majuzi kwaajili ya manyanyaso tu ya mgambo na nchi ikawaka, rais akaondoka madarakani.
Kitendo cha Makonda kuwadhalilisha watumishi wa ardhi kinondoni ni kitendo kinachoumiza dhamira za wengi, ni haki na usawa na utu wa mtu vilivyokanyagwa bila kipimo.
Magufuli turudishe pamoja kama taifa ili kutambua mabadiliko tunayoyataka. Sio kila mabadiliko ni maendeleo.
Leo tukitaka viwango vikubwa vya utendaji kwa kila mtu katika taifa tuanze na viongozi, tuanze na midomo yao. Mheshimiwa rais, tuanze na Makonda.
Ili mabadiliko yatokee, kila mtu afanye nafasi yake. Kwa hili mimi nimefanya yakwangu. Bado wewe!