Rais Magufuli; Masikini hawa hawana haki, ingilia kati uwasaidie

bopwe

JF-Expert Member
Oct 1, 2013
1,768
1,445
Moja ya malengo yako ni kuona Raia Masikini wakifaidi uhuru, fursa na nafasi za maisha zilizopo nchini.
Fursa hizi ni nyingi na zipo katika shughuli tofauti ikitegemea kiwango cha
elimu
mtaji
na maeneo
kuna fursa za kazi za serikali
kuna fursa za kazi kwenye secta binafsi kama kuajiriwa au kuanzisha biashara mbali
kuna fursa za kilimo , kama ni kilimo cha biashara au cha kujikimu mtu na familia yake
kuna fursa za wavuvi ..kupata fursa za kuvua na kuuza samaki kama pale Ferry
kuna fursa za vibarua mbali mbali wakiwamo
wajenzi na vibarua
wafagia barabara
boda boda
hawa wote wanatumia fursa zilizopo na kwa kiwango fulani wanalindwa lindwa na vijisheria ..angalau wanafanya kazi zao bila bughudha ..wanatambuliwa.
kuna kundi moja la wananchi wako hawana fursa za kuwa huru nchini mwao. Wao biashara zao kila siku haramu , kila siku wana chezea virungu vya mgambo , nakumbuka uliwahi kusema mgambo wa jiji kupiga masikini hawa itakua mwishio...hawa ni pamoja na

  • wauza Madafu na Baiskeli zao hawa mtaji wao ni elfu 40...hawa masikini wa mungu wana watoto , wanataka kuwapeleka watoto wao shule nao wanataka kula nao wanataka kufaidi fursa lakini Mgambo wanawanyima fursa hio, kila siku ya mungu wanafukuzana nao, wanawanyanganya baskeli zao na kuchukua madafu (mtaji) . wauza madafu sio wahalifu...wanafanya kazi halali...na madafu ni bidhaa muhimu ni kiburudisho na dawa kwa wagonjwa. .. hawa wanatembeza na baiskeli zao hawachafui mji ..sioni sababu ya kuwanyima fursa masikini hawa kutoa huduma hii...mgambo wanawapiga kila siku inakua kama wanauza unga...ni dhulma kwa masikini hawa...sioni sababu yao kwa nini wasiuze madafu ...sioni sababu yao kuwa wahalifu kuuza madafu ndani ya nchi yao...ni uonevu
  • Pili kuna mama ntilie...hawa nao bado wanasumbuliwa hasa maeneo ya upanga , mjini , kariakoo, ilala nk. Mgambo bado wamekua wakipita kila siku kumwaga na kuwapiga na kuwadhalilisha kina mama hawa masikini wa mungu...sioni dhambi ya huduma hiii , kazi yao sio haramu nao pia wanatumia fursa ya kuwa huru na ukweli watanzania wengi wanatumia chakula cha kina mama hawa..chakula chao ni rahisi na kitamu pia..lakini inasikitisha kuona mgambo wanapita kila siku kuwapiga marungu na kumwaga chakula na mitaji yao..kuwarejesha katika ufukara...tunapiga vita ukahaba...lakini biashara hizi za kina mama wasio na mitaji mikubwa nayo tunaipiga vita ..hii sio haki hii ni dhulma
  • tatu kuna wauza matunda..nimeona mara kadhaa Mawaziri wengi husima njiaani kununua matunda kutoka vijana hawa ambao wamebeba matunda yao kwenye Carts au Baiskeli , wakiwa wameketi pembeni ya baadhi ya mitaa ya mjini , upanga , masaki, nk nk....hawa nao wanatumia fursa za kuwa huru ndani ya nchii yao. Biashara ya matunda sio Haramu, ni halali na wanasaidia wana nchi wengi kuwasogezea huduma hii....wengi hawachafui mazingira wanajitahidi kufanya kwa usafi ...lakini hakki hio ina pondwa na mgambo na jiji ..kila siku wanapondwa pondwa na mgambo hakika inatia uchungu , sio haki ni dhulma kuwafanyia wananchi mambo haya.
naelewa haya mambo huyajui kama yana tendeka ndani ya utawala wako, bila ya shaka haya huambiwi lakini yanatendeka na yanahitaji neno lako kuyaingilia..masikini hawa nao wana familia na hizi kazi sio haramu ni halali..Mimi sio muuza madafu...lakini ninapoona wanavo dhulumia hawa vijana inaniuma sana..sio haki Mr President tafadhali ingilia kati ...
kama ni suala la usafi au utaratibi...basi jiji ...lije na ubunifu...waweke utaratibu wanaotaka . madafu yanatakiwa na yanapendwa waje na wazo la vipi wauza madafu wafanye biashara zao..waweke utaratibu..sio kuwapiga marufuku bila ya solution ya kuwasaidia
wauza matunda nao waagize jiji waje na solution ..lakini sio kukataza
na mama ntilie nao jiji waje na utaratibu...huduma yao inapendwa kuifuta kwa kumwaga chakula chao sio haki
Naamini utasikiliza kilio hichi na kupiga marufuku uonevu huu..kwa kuwataka Jiji waache maonevu haya na badala yake waje na utaratibu wanao utaka...lakini kabla ya kutoa muuongozo tunakuomba usimamishe uonevu huu kwa masikini hawa...ambao ndio nguzo yako
ahsante
 
Moja ya malengo yako ni kuona Raia Masikini wakifaidi uhuru, fursa na nafasi za maisha zilizopo nchini.
Fursa hizi ni nyingi na zipo katika shughuli tofauti ikitegemea kiwango cha
elimu
mtaji
na maeneo
kuna fursa za kazi za serikali
kuna fursa za kazi kwenye secta binafsi kama kuajiriwa au kuanzisha biashara mbali
kuna fursa za kilimo , kama ni kilimo cha biashara au cha kujikimu mtu na familia yake
kuna fursa za wavuvi ..kupata fursa za kuvua na kuuza samaki kama pale Ferry
kuna fursa za vibarua mbali mbali wakiwamo
wajenzi na vibarua
wafagia barabara
boda boda
hawa wote wanatumia fursa zilizopo na kwa kiwango fulani wanalindwa lindwa na vijisheria ..angalau wanafanya kazi zao bila bughudha ..wanatambuliwa.
kuna kundi moja la wananchi wako hawana fursa za kuwa huru nchini mwao. Wao biashara zao kila siku haramu , kila siku wana chezea virungu vya mgambo , nakumbuka uliwahi kusema mgambo wa jiji kupiga masikini hawa itakua mwishio...hawa ni pamoja na

  • wauza Madafu na Baiskeli zao hawa mtaji wao ni elfu 40...hawa masikini wa mungu wana watoto , wanataka kuwapeleka watoto wao shule nao wanataka kula nao wanataka kufaidi fursa lakini Mgambo wanawanyima fursa hio, kila siku ya mungu wanafukuzana nao, wanawanyanganya baskeli zao na kuchukua madafu (mtaji) . wauza madafu sio wahalifu...wanafanya kazi halali...na madafu ni bidhaa muhimu ni kiburudisho na dawa kwa wagonjwa. .. hawa wanatembeza na baiskeli zao hawachafui mji ..sioni sababu ya kuwanyima fursa masikini hawa kutoa huduma hii...mgambo wanawapiga kila siku inakua kama wanauza unga...ni dhulma kwa masikini hawa...sioni sababu yao kwa nini wasiuze madafu ...sioni sababu yao kuwa wahalifu kuuza madafu ndani ya nchi yao...ni uonevu
  • Pili kuna mama ntilie...hawa nao bado wanasumbuliwa hasa maeneo ya upanga , mjini , kariakoo, ilala nk. Mgambo bado wamekua wakipita kila siku kumwaga na kuwapiga na kuwadhalilisha kina mama hawa masikini wa mungu...sioni dhambi ya huduma hiii , kazi yao sio haramu nao pia wanatumia fursa ya kuwa huru na ukweli watanzania wengi wanatumia chakula cha kina mama hawa..chakula chao ni rahisi na kitamu pia..lakini inasikitisha kuona mgambo wanapita kila siku kuwapiga marungu na kumwaga chakula na mitaji yao..kuwarejesha katika ufukara...tunapiga vita ukahaba...lakini biashara hizi za kina mama wasio na mitaji mikubwa nayo tunaipiga vita ..hii sio haki hii ni dhulma
  • tatu kuna wauza matunda..nimeona mara kadhaa Mawaziri wengi husima njiaani kununua matunda kutoka vijana hawa ambao wamebeba matunda yao kwenye Carts au Baiskeli , wakiwa wameketi pembeni ya baadhi ya mitaa ya mjini , upanga , masaki, nk nk....hawa nao wanatumia fursa za kuwa huru ndani ya nchii yao. Biashara ya matunda sio Haramu, ni halali na wanasaidia wana nchi wengi kuwasogezea huduma hii....wengi hawachafui mazingira wanajitahidi kufanya kwa usafi ...lakini hakki hio ina pondwa na mgambo na jiji ..kila siku wanapondwa pondwa na mgambo hakika inatia uchungu , sio haki ni dhulma kuwafanyia wananchi mambo haya.
naelewa haya mambo huyajui kama yana tendeka ndani ya utawala wako, bila ya shaka haya huambiwi lakini yanatendeka na yanahitaji neno lako kuyaingilia..masikini hawa nao wana familia na hizi kazi sio haramu ni halali..Mimi sio muuza madafu...lakini ninapoona wanavo dhulumia hawa vijana inaniuma sana..sio haki Mr President tafadhali ingilia kati ...
kama ni suala la usafi au utaratibi...basi jiji ...lije na ubunifu...waweke utaratibu wanaotaka . madafu yanatakiwa na yanapendwa waje na wazo la vipi wauza madafu wafanye biashara zao..waweke utaratibu..sio kuwapiga marufuku bila ya solution ya kuwasaidia
wauza matunda nao waagize jiji waje na solution ..lakini sio kukataza
na mama ntilie nao jiji waje na utaratibu...huduma yao inapendwa kuifuta kwa kumwaga chakula chao sio haki
Naamini utasikiliza kilio hichi na kupiga marufuku uonevu huu..kwa kuwataka Jiji waache maonevu haya na badala yake waje na utaratibu wanao utaka...lakini kabla ya kutoa muuongozo tunakuomba usimamishe uonevu huu kwa masikini hawa...ambao ndio nguzo yako
ahsante

Good point...ni kweli kumekua na uonevu secta hii ya walala hoi...Rais ingilie ...wamepata shida miaka na miaka..it need to stop nao watambulwe
 
Ni wwzi wanavo onewa hawa jamaa wa madafu na matunda inatia huruma...na inaonesha namna gani nchi hii namna gani maskini wasivo na haki na eanavo dhulumiwa....wanatia huruma kila siku kukimbizana na mgambo ambao hawana elimu hata ya ubinadamu...mara nyengine hata jambazi anashikwa vizuri kuliko hawa raia wema..Mungu awasaidie..kwani hakuna anae waona
 
Kwa uandishi wako na maelezo yake inaelekea unaishi Dsm. Uchambuzi wako wa kero za wananchi ni mzuri na tungetafuta jinsi ya kuwafikia kwa mabandiko hapa Jamiiforums kuwauliza kina RC Paul Makonda, DC Polepole wanafanya nini baada ya kuteuliwa!

Maana hata jinsi ya kuwasaidia Mama- Ntilie, Wauza Madafu wafanye kazi zao bila wasiwasi kazi hiyo pia afanye Magufuli kweli ataweza labda tu tungeomba Mh. Rais kuwatimua kazi hawa kina Mkuu wa Mkoa/Wilaya n.k maana wameshindwa kumwakilisha vyema.

Nitachambua "mfumo mpya" wa utendaji hapo chini kuona kama una/tuna imani na wateule wa Mh. Rais au la . Na pia kuona kama tunafanya mazoea kila kitu ni "cha Mh. Magufuli" wengine wateuliwa wake wanasubiri "Bwana Mkubwa" aseme na wao watakazia hapohapo bila ubunifu wa kutatua kero za maeneo yao husika na sisi raia tunaona ni sawa kila kitu aseme Mh. Rais ndiyo njia bora ya utendaji wa "mfumo".

Tayari Mh. Magufuli amemaliza kuweka "mfumo wa kiuongozi wa hapa kazi tu " na ameteua viongozi wakimwakilisha mkoani Dsm kama mkuu wa mkoa RC kina Paul Makonda wapo, Polepole kama DC yupo n.k sasa kuuruka "mfumo mpya wa kiutendaji unaodai Hapa Kazi Tu ngazi zote" na kuomba Rais afanye hata maamuzi yanayohusu ngazi ya mkoa, jiji, wilaya, halmashauri,kata n.k maana yake inaashiria "mambo hayaendi ipasavyo"?

Pia labda nasema labda tena, huna imani na mfumo mpya pamoja na wasaidizi wateule wa Mh. Rais wa kuhakikisha mfumo unafanya kazi kama kina Mkuu wa Mkoa DSM na wateule wengine wa Rais jijini Dsm? Je wakuu wa mikoa au wilaya wameshindwa kusuka ''mifumo midogo'' inayoweza kuwapatia taarifa za kero za maeneo yao ili kuunga mkono jitihada za ''mfumo mkubwa'' toka kwa Rais?

Na ikiwa ni hivyo basi inaonesha "mfumo" una mapungufu maana hautoi nafasi kwa viongozi wa mkoa, wilaya, halmashauri na kata kutambua kero za ngazi hiyo ya mkoa kwenda chini na kupatia ufumbuzi wa kero hizo au pia unaonesha viongozi wa ngazi za mkoa kwenda chini hawana ukaribu, ubunifu, maono ya kuona fursa kuondoa kero za wananchi wa maeneo yao kiasi cha wananchi kupeleka ombi kwa Rais atafute ufumbuzi wa kero zao.
 
Hivi ni kwa nini muuza azamu lamba lamba anakubalika kuuza popote tofauti na wa madafu?.

Good point.....ati analipa kodi ! Hakuna sababu wauza madafu na matunda ndani ya baiskeli wanyanganywe madafu yao na kupigwa virungu...lazima uonevu huu ustop.
Hawa jamaa hawana wa kuwatetea wala kuwaonea huruma
 
Kwa uandishi wako na maelezo yake inaelekea unaishi Dsm. Uchambuzi wako wa kero za wananchi ni mzuri na tungetafuta jinsi ya kuwafikia kwa mabandiko hapa Jamiiforums kuwauliza kina RC Paul Makonda, DC Polepole wanafanya nini baada ya kuteuliwa!

Maana hata jinsi ya kuwasaidia Mama- Ntilie, Wauza Madafu wafanye kazi zao bila wasiwasi kazi hiyo pia afanye Magufuli kweli ataweza labda tu tungeomba Mh. Rais kuwatimua kazi hawa kina Mkuu wa Mkoa/Wilaya n.k maana wameshindwa kumwakilisha vyema.

Nitachambua "mfumo mpya" wa utendaji hapo chini kuona kama una/tuna imani na wateule wa Mh. Rais au la . Na pia kuona kama tunafanya mazoea kila kitu ni "cha Mh. Magufuli" wengine wateuliwa wake wanasubiri "Bwana Mkubwa" aseme na wao watakazia hapohapo bila ubunifu wa kutatua kero za maeneo yao husika na sisi raia tunaona ni sawa kila kitu aseme Mh. Rais ndiyo njia bora ya utendaji wa "mfumo".

Tayari Mh. Magufuli amemaliza kuweka "mfumo wa kiuongozi wa hapa kazi tu " na ameteua viongozi wakimwakilisha mkoani Dsm kama mkuu wa mkoa RC kina Paul Makonda wapo, Polepole kama DC yupo n.k sasa kuuruka "mfumo mpya wa kiutendaji unaodai Hapa Kazi Tu ngazi zote" na kuomba Rais afanye hata maamuzi yanayohusu ngazi ya mkoa, jiji, wilaya, halmashauri,kata n.k maana yake inaashiria "mambo hayaendi ipasavyo"?

Pia labda nasema labda tena, huna imani na mfumo mpya pamoja na wasaidizi wateule wa Mh. Rais wa kuhakikisha mfumo unafanya kazi kama kina Mkuu wa Mkoa DSM na wateule wengine wa Rais jijini Dsm? Je wakuu wa mikoa au wilaya wameshindwa kusuka ''mifumo midogo'' inayoweza kuwapatia taarifa za kero za maeneo yao ili kuunga mkono jitihada za ''mfumo mkubwa'' toka kwa Rais?

Na ikiwa ni hivyo basi inaonesha "mfumo" una mapungufu maana hautoi nafasi kwa viongozi wa mkoa, wilaya, halmashauri na kata kutambua kero za ngazi hiyo ya mkoa kwenda chini na kupatia ufumbuzi wa kero hizo au pia unaonesha viongozi wa ngazi za mkoa kwenda chini hawana ukaribu, ubunifu, maono ya kuona fursa kuondoa kero za wananchi wa maeneo yao kiasi cha wananchi kupeleka ombi kwa Rais atafute ufumbuzi wa kero zao.


Kwa ufupi naweza kusema hizi amri zinatoka kimkoa, labda jiji au ofisi ya wilaya au mkuu wa mkoa wenyewe.
Hivyo haya yanayo endelea yana baraka zao. Wanafanya hivi na kwao wao tayari wanadhani ndio solution. Hawana ubunifu wa kutatua matizo madogo haya...ni mambo madogo sana lakini sio wanunifu...slogan ya Rais hapa kazi tu wana itafsiri vibaya kwa maana ya maamuzi ya nguvu..lakini maana ya hapa kazi tu sio kutumia mgambo kumwaga chakula cha mamam ntilie au kuiba matunda ya masikini hawa bali ni kufanya kazi kwa ubunifu ili kuondoa matatizo ya watu unao waongoza...nachelea kusema mkoa bado haujapata kiongozi anaejua matatizi na shughuli ya jiji hili...hawajlijui jiji kwa maneno ya Khadija Kopa
 
Back
Top Bottom