elivina shambuni
JF-Expert Member
- May 31, 2018
- 461
- 295
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli leo Novemba 26, 2019 anatarajiwa kuwa na ziara ya kikazi ya siku mbili katika halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga.
Akizungumzia ujio wa Rais Magufuli mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha amesema Rais Magufuli anatarajiwa kuwasili kesho Novemba 26 na kuanza ziara yake ambayo itamalizika Novemba 27 mwaka huu.
Kutokana na ziara hiyo ya Rais Dkt Magufuli mkuu wa wilaya ya Kahama amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kumlaki kiongozi huyo wa kitaifa.