Rais Magufuli: Kiswahili sasa ni lugha rasmi ya nne ya SADC. Tumefuta machozi ya Baba wa Taifa

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,516
Mwenyekiti wa SADC na Rais wa Tanzania, Dr. John Pombe Magufuli ametoa taarifa kuwa Wakuu wa nchi wa SADC wamekipitisha rasmi Kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne ya SADC.

Rais Magufuli, ambaye hivi punde ametoa hotuba ya kufunga Mkutano huo huko Dar es Salaam, amesema kuwa kwakuwa kihistoria Kiswahili ni lugha ya Waafrika na ilitumika kutuunganisha hasa wakati wa kujikomboa, kupitishwa kwake ni kufuta machozi ya ya Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mwenyekiti Magufuli amesema kuwa kiujumla, Mkutano huo wa 39 wa SADC, umekuwa wa mafanikio makubwa kutikana na yaliyojadiliwa na kuamuliwa na Wakuu wa Nchi wanachama. Amegusia kujiunga kwa Burundi kwenye SADC na kuhusu vikwazo vya Zimbabwe.

Kongole kwa viongozi wote wa Tanzania walioanzisha, kusimamia na kuwezesha kupitishwa kwa Kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne ya SADC. Najivunia Kiswahili, najivunia kuwa mtanzania!
 
Wamekubaliana yapi ya kufanyia kazi ?
target ni ipi na kwa muda gani ?
Kama sio mbaya au siri mkutano umegharimu kiasi gani na tunaexpect kupata ngapi kwa makubaliano hayo?

Najua labda hauwezi kujibu hayo lakini kwa yoyote anayejua naomba taarifa kwa manufaa ya wote ili mwisho wa siku tuone mafanikio ni hii iwe template ya mikutano kama hii (faida na hasara)
 
Mwenyekiti wa SADC na Rais wa Tanzania, Dr. John Pombe Magufuli ametoa taarifa kuwa Wakuu wa nchi wa SADC wamekipitisha rasmi Kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne ya SADC.

Rais Magufuli, ambaye hivi punde ametoa hotuba ya kufunga Mkutano huo huko Dar es Salaam, amesema kuwa kwakuwa kihistoria Kiswahili ni lugha ya Waafrika na ilitumika kutuunganisha hasa wakati wa kujikomboa, kupitishwa mwake ni kufuta machozi ya ya Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mwenyekiti Magufuli amesema kuwa kiujumla, Mkutano huo wa 39 wa SADC, umekuwa wa mafanikio makubwa kutikana na yaliyojadiliwa na kuamuliwa na Wakuu wa Nchi wanachama. Amegusia kujiunga kwa Burundi kwenye SADC na kuhusu vikwazo vya Zimbabwe.

Kongole kwa viongozi wote wa Tanzania walioanzisha, kusimamia na kuwezesha kupitishwa kwa Kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne ya SADC. Najivunia Kiswahili, najivunia kuwa mtanzania!
Ni zaidi ya mwaka sasa tangu Rwanda watangaze Kiswahili kuwa moja ya lugha kuu za mawasiliano, na ni miezi kadhaa tangu Afrika Kusini nao watangaze Kiswahili kuwemo kwenye mitaala yao. Tell me my learned bro, nini kimeshafanyika kutumia fursa hizo?

Kama mtu ninayeshiriki kukisambaza Kiswahili kimataifa (as a tutor) nadhani adui wetu mkubwa ni kuweka mbele siasa kwenye masuala ya kitaaluma na kitaalamu.

Na katika taswira pana, uenyekiti wa SADC wa Mzee Meko unaweza kuishia kuwa hoja ya kisiasa tu (wanadai uchapakazi wake ndio umefanya apewe uenyekiti huo) badala ya kuwa fursa muhimu kiuchumi na kijamii.
 
Hongera JPM, lugha ya kiswahili itapunguza mipaka ya kikoloni na kuchangamana kwa ndugu na majirani wa Africa.
 
Ni zaidi ya mwaka sasa tangu Rwanda watangaze Kiswahili kuwa moja ya lugha kuu za mawasiliano, na ni miezi kadhaa tangu Afrika Kusini nao watangaze Kiswahili kuwemo kwenye mitaala yao. Tell me my learned bro, nini kimeshafanyika kutumia fursa hizo?

Kama mtu ninayeshiriki kukisambaza Kiswahili kimataifa (as a tutor) nadhani adui wetu mkubwa ni kuweka mbele siasa kwenye masuala ya kitaaluma na kitaalamu.

Na katika taswira pana, uenyekiti wa SADC wa Mzee Meko unaweza kuishia kuwa hoja ya kisiasa tu (wanadai uchapakazi wake ndio umefanya apewe uenyekiti huo) badala ya kuwa fursa muhimu kiuchumi na kijamii.
Nakuelewa kaka Chahali. Haitoshi hatua tulizofikia kukihusu Kiswahili. Tunapaswa, kama nchi, kuchangamkia fursa zinazozalishwa na Kiswahili.
 
Badala ya kuanzisha sarafu moja visa free zone na mambo ya kuchochea uchumi sasa ndio nimeamini Darwin alikuwa mkweli.
 
lugha haikuzwi tu kwa kuwaomba watu waitumie.., bali kuwafanya watu wapende kuitumia kwa kupata kitu fulani..., kwahio ni jukumu la wasanii kutengeneza vitu kama nyimbo nzuri na movies ili watu wapende kuelewa ni nini kinasemwa..., wewe unadhani kusema kuchi kuchi hotai.., au andhaa kanoon ni sababu india walituomba au kazi nzuri ilituka tu tunasema.....

Yeh andha kanoon hai (law is blind)
jaane kahan daga dede (it can cheat you anywhere)
Jaane kise saza dede (it can punish anyone)
Saath na de kamzoron ka (It doesn't stand on the side of the weak)
Yeh saathi hai choron ka (It's the companion of the robbers)
Baaton aur daleelon ka (It belongs to words and arguments)
Yeh hai khel vakeelon ka (It's a game of lawyers)
Yeh insaaf nahi karta (It doesn't give justice)
 
Ok sawa.Ila hawa viongozi wetu sasa waanze kufikiria katika kuwa na free movement of people within the 16 countries .
Waondoe visa na resident permit. Yaani kama mtanzania nikitaka kwenda kuishi na kufanya kazi South Africa au Botswana naenda na nikiwa huko nitakuwa na haki zote kama msouth Africa ai mtswana kasoro kupiga kura tu ya uchaguzi mkuu wa Rais.
Mbili waweke pia free movement of goods.
Nina nyanya zangu,nikitaka kwenda kuuza Malawi naenda.
Najua hasa hapa kwenye free movement of goods kutakuwa na changamoto kama ushuru ama tax vinalipwa wapi.
Hayo ndo mambo mazito ya kujadili.
Miaka 39 leo since SADCC now SADC tokea ianzishwe hakuna hata free movement of people !Na hakuna hata member anayeitoa kama hoja. Sijui wanagopa nini?
Au utofauti wa maendeleo between members ndo kikwazo?
 
Kiswahili ni Lugha ya Afrika sasa anataka kuwazuia wengine ambao sio member wa SADC wasizungmze kiswahili??

Mlitegemea SADC angezungumza KIZULU? hebu acheni mambo yenu
 
Kiswahili ni Lugha ya Afrika sasa anataka kuwazuia wengine ambao sio member wa SADC wasizungmze kiswahili??

Mlitegemea SADC angezungumza KIZULU? hebu acheni mambo yenu
Afrika ipi? Historia ya Kiswahili isipotoshwe. Sio kweli kwamba Magufuli ni mpenzi wa Kiswahili. Hana namna. Ni lugha ya pili anayoweza kuongea kwa uhuru. Amefanikiwa kuipitisha kama lugha rasmi EAC. Wakuu walikubali ili naye apate kuongea! SADC wamekubali kwa sababu hiyo. Yawezekana kabisa wakamuomba kugharamia vikorombwezo vya kuwezesha itafsirike ndani ya mikutano ya SADC. Pili, kutakuwa hakuna udhuru tena kwake kukacha mikutano. Kikwazo cha lugha kimeondolewa. Kiswahili kinakuwa lugha rasmi katika mikutano ya SADC na sio lugha rasmi katika nchi za SADC!
 
Watu wenye akili ya kitwana wameumbuka.
Mtoto akiitwa Tizo, matatizo hayamwishi. Akiitwa Shida ni shida hadi siku ya mwisho. Akiitwa Tabu, tabu zote zinafanya makao ndani yake. Chagulieni watoto majina mazuri wale mema ya nchi!
Waliopewa majina mabaya wanakutana na kila lililo baya. Huyu aliyejiita mwenyewe Magonjwa Mtambuka anayaugua sana. Hayamwishi, afadhali mwenye Ukimwi! Leo ana schizophrenia, kesho ankylostomiasis, mara jingaitis au pumbavitis. Baadhi acute na mengine chronic. Ilimradi tu ni magonjwa mtambuka. Anayo!
 
Kwa EAC ni Kenya na Tanzania tu ndo wanao ongea Kiswahili. nenda Uganda kama wanakijua kiswahili. Hahaaaa
Hongera JPM, lugha ya kiswahili itapunguza mipaka ya kikoloni na kuchangamana kwa ndugu na majirani wa Africa.
 
Nakuelewa kaka Chahali. Haitoshi hatua tulizofikia kukihusu Kiswahili. Tunapaswa, kama nchi, kuchangamkia fursa zinazozalishwa na Kiswahili.
Kuchangamkia furusa zipi? Wachina wako Dunia nzima wanajua Kichina pekee. Hiki Kiswahili ndo kitatufanya tupige hatua za Kimaendeleo?

Tunataka kuaminishwa umasikini tulio nao ni kwa sababu Kiswahili hakizungumzwi huko SADC?

Hicho Kireno kwa SADC si kinazungumzwa na nchi mbili tu kwa sababu walitawaliwa na Ureno?

Tuambie mfano Tanzania tunajitihada gani na Kireno? make nayo ni Lugha ya SADC.

Hizi ni siasa tu hakuna kitu hapa
 
Badala ya kuanzisha sarafu moja visa free zone na mambo ya kuchochea uchumi sasa ndio nimeamini Darwin alikuwa mkweli.
Hii SADC ni ya ajabu sana. Mbona wachina wamjeaa kwetu na nchi zingine na wanajua Kichina tu?

EAC tu kiswahili kinazungumzwa Kenya na Sisi basi.

Na Je Kiswahili ndo kitapeleka nchi za SADC kwenye Uchumi mkubwa?
 
Afrika ipi? Historia ya Kiswahili isipotoshwe. Sio kweli kwamba Magufuli ni mpenzi wa Kiswahili. Hana namna. Ni lugha ya pili anayoweza kuongea kwa uhuru. Amefanikiwa kuipitisha kama lugha rasmi EAC. Wakuu walikubali ili naye apate kuongea! SADC wamekubali kwa sababu hiyo. Yawezekana kabisa wakamuomba kugharamia vikorombwezo vya kuwezesha itafsirike ndani ya mikutano ya SADC. Pili, kutakuwa hakuna udhuru tena kwake kukacha mikutano. Kikwazo cha lugha kimeondolewa. Kiswahili kinakuwa lugha rasmi katika mikutano ya SADC na sio lugha rasmi katika nchi za SADC!
Hahaaaa kumbe ni kwenye Mikutano ya SADC? Dah
 
Mtoto akiitwa Tizo, matatizo hayamwishi. Akiitwa Shida ni shida hadi siku ya mwisho. Akiitwa Tabu, tabu zote zinafanya makao ndani yake. Chagulieni watoto majina mazuri wale mema ya nchi!
Waliopewa majina mabaya wanakutana na kila lililo baya. Huyu aliyejiita mwenyewe Magonjwa Mtambuka anayaugua sana. Hayamwishi, afadhali mwenye Ukimwi! Leo ana schizophrenia, kesho ankylostomiasis, mara jingaitis au pumbavitis. Baadhi acute na mengine chronic. Ilimradi tu ni magonjwa mtambuka. Anayo!
Acha kuongea upuuzi mara moja.
 
Back
Top Bottom