Rais Magufuli, kauli yako inaenda kuizika elimu ya juu

Aaron

JF-Expert Member
Nov 18, 2010
3,019
4,693
Habari zenu wanajukwaa.
Hili andiko ilibidi nilipeleke jukwaa la elimu ila ni vyema lijadiliwe hapa kwa kuwa huyu anayeivuruga elimu ni mwana siasa.

Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu niliyeadiliwa kwa mfumo TCU online.

Juzi baada ya jpm kutoa kauli yake juu ya TCU kuwapangia vyuo wanafunzi wasio vitaka. Ila ukweli ni kwamba tcu haiwezi kumpangia mwanafunzi chuo ambacho hakuchagua na kikubwa zaidi inamsaidia mwafunzi aliyekosa ushindani kwa vyuo ulivyovichagua. Hili linaeleweka na waliodahiliwa kwa mfumo huu watanisaidia kuongezea hapa.

Sasa baada ya kauli ya Rais wakati akifungua mabweni pale udsm. TCU wameamua isiwe shida kila chuo kipokee maombi na kupeleka TCU baadae. Kwa jicho la haraka ni kwamba wanafunzi wengi watakosa vyuo na udahili huu utakuwa mgumu sana.Mfano leo chuoni kwetu wametoa tangazo la kuanza kupokea maombi na ada ya maombi ni elfu 50.

Ina maana kama unataka kuomba vyuo zaidi ya kimoja ili kujiweka kwenye mazingira ya kutokosa chuo itabidi ulipie fomu ya kila chuo.. Wakati tcu online tulikuw tunalipia elfu 50 na kuomba vyuo vitano.

Sasa ili uombe vyuo vitano itabidi utumie 250000 hapo bado huna uhakika wa kupata nafasi kulingana na ushindani wakati tcu ulikuwa unalipia mara moja elfu 50.

Mapungufu ya mfumo huu ni mengi na hapa vyuo lazima vifanye udanganyifu na kuwadahili wanafunzi wasio na sifa. Yale ya miaka ya nyuma yanajirudi.

Serikali mjirudi na TCU waendelee kufanya udahili huu.. Na mapungufu yatakayojitokeza muwahukumu hawa TCU.
 
Pamoja na Mapungufu yote hayo, ni njia nzuri zaidi kwani humpa mwanafunzi wigo mpana wa kuchagua Chuo cha hitajio lake. Hutumika sana nchi za Wenzetu huko Ughaibuni.

Ili kupunguza Swala la gharama zisizo na msingi, Nashauri yafuatayo yafanyike.
Moja, gharama za fomu za kuomba Udahili ziwe bure kabisa kwa kila chuo. Hii itasaidia wanafunzi kuepukana na gharama nyingi za kuomba udahili katika vyuo vingi. Badala yake, ada ya form Tsh 50,000 ilipwe na mwanafunzi ambaye amedahiliwa na kufanikiwa kusajiliwa katika chuo tajwa. Fedha hii ilipwe pindi wanafunzi waliodahiliwa kufika Chuoni wanapowasili kwa ajili ya Usajili.

Hii ni nzuri kwani itaepusha gharama zisizo na msingi kwa wanafunzi na walezi wao. Pia, vyuo vingi vinaweza kupokea fedha nyingi kwa mgongo wa fomu ya Udahili ilihali haina uwezo wa kuwadahili wanafunzi wote hao.

Pili, kila chuo kiwe na system yake ya Udahili online. Mfano, UDOM walitengeneza system ya kudahili mwaka jana. Vyuo vyote vitengeneze website ambayo itaweza kupokea taarifa pamoja na nyaraka mbalimbali za wanafunzi wanaoomba Udahili. Hii itasaidia kupunguza gharama za nauli pamoja na matumizi mengine kwa wanafunzi. Hii itamuwia ugumu sana Mwanafunzi kutoka Kigoma mwenye nia ya kusoma vyuo vya Dar es Salaam kutoka huko mpaka huku kwa ajili ya kuomba usahili. Gharama za usafiri pamoja na malazi ni kubwa sana. Ingelikuwa rahisi kama kila chuo kitakuwa na System yake.

Nawasilisha.
 
Kufuta ada za fomu ya maombi lazima kuambatane na ruzuku itakayo viwezesha vyuo kugharamia zoezi la kupitia hizo fomu. Maamuzi kama haya hayakosi gharama, hapa ni swala tu la kuchagua ni nani wa kuzilipa!

Mkuu alikuwa na nia njema ya kutatua tatizo la TCU kuwapangia waombaji vyuo au programu wasizozitaka, ila napenda kuamini mashauriano na mijadala iliyohusisha wataalam na wadau wa sekta hii ingeweza kuleta suluhisho bora zaidi la tatizo husika.

Pengine alisikiliza ushauri binafsi wa Prof. Ndali na wengine wachache waliokuwa karibu yake siku ile..
 
Hilo la TCU kupangia watu vyuo wasivyochagua mimi ni muhanga mmojawapo kwa hapo nakukatalia mimi ni miongoni mwa walioanza na mfumo wa udahili wa pamoja (CAS) na ulianza 2011 kulikua na machaguo 8 katika machaguo yote nilochagua sikuchaguliwa hata sehemu moja ingawa sifa nilikuanazo nikapangiwa IFM na vile vyuo nilivyochagua nafasi zilibaki kibao na mwaka huo nikakosa mkopo nikashindwa kwenda chuo, mwaka ulofuatia niliaply upya na kulikua na machaguo 5 nilichagua nikachaguliwa tena IFM chuo ambacho sikukiomba na pia hata fani nilochaguliwa sikuwahi kuwaza nitaisoma TCU walileta option ya kuchagua tena kama hatukuridhika mimi nilirudisha tena kule nilikokua nataka system ilinikubalia na kunionyesha nimechaguliwa ajabu selection zilipotangazwa nilichaguliwa palepale IFM na mkopo nilipewa 100% nilipofika chuo nilifanya mchakato wa kuhama chuo iliwezekana ila kwenye suala la kuhamisha mkopo ilikua mtihani mwisho wa siku nilisoma nisichokipenda na ni nje ya ndoto zangu siku zote nilikua nalaani hilo dubwana CAS
 
Habari zenu wanajukwaa.
Hili andiko ilibidi nilipeleke jukwaa la elimu ila ni vyema lijadiliwe hapa kwa kuwa huyu anayeivuruga elimu ni mwana siasa.

Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu niliyeadiliwa kwa mfumo TCU online.

Juzi baada ya jpm kutoa kauli yake juu ya tcu kuwapangia vyuo wanafunzi wasio vitaka. Ila ukweli ni kwamba tcu haiwezi kumpangia mwanafunzi chuo ambacho hakuchagua na kikubwa zaidi inamsaidia mwafunzi aliyekosa ushindani kwa vyuo ulivyovichagua. Hili linaeleweka na waliodahiliwa kwa mfumo huu watanisaidia kuongezea hapa.

Sasa baada ya kauli ya rais wakati akifungua mabweni pale udsm. Tcu wameamua isiwe shida kila chuo kipokee maombi na kupeleka tcu baadae. Kwa jicho la haraka ni kwamba wanafunzi wengi watakosa vyuo na udahili huu utakuwa mgumu sana.mfano leo chuoni kwetu wametoa tangazo la kuanza kupokea maombi na ada ya maombi ni elfu 50.

Ina maana kama unataka kuomba vyuo zaidi ya kimoja ili kujiweka kwenye mazingira ya kutokosa chuo itabidi ulipie fomu ya kila chuo.. Wakati tcu online tulikuw tunalipia elfu 50 na kuomba vyuo vitano.

Sasa ili uombe vyuo vitano itabidi utumie 250000 hapo bado huna uhakika wa kupata nafasi kulingana na ushindani wakati tcu ulikuwa unalipia mara moja elfu 50.
Mapungufu ya mfumo huu ni mengi na hapa vyuo lazima vifanye udanganyifu na kuwadahili wanafunzi wasio na sifa. Yale ya miaka ya nyuma yanajirudi.

Serikali mjirudi na tcu waendelee kufanya udahili huu.. Na mapungufu yatakayojitokeza muwahukumu hawa tcu.
Dogo, kabla ya mfumo wa udahili wa TCU online kulikua na udahili kupitia vyuoni,na baadhi ya vyuo vilikua havikudahili hadi ufanyr mtihani wao kama chuo, vingine havikua na huo mfumo.Na elim ndo hyo hyo.Mfumo wa TCU online ndo uloleta VILADHA ambao wamenyofolewa baadhi ya vyuo.Na mfumo wa TCU baadhi ya vyuo havikuupenda like UDSM so ndo wangefanyaje wakaukubali.MUM waliukataa na hawajawah kuutumia.

Labda kwa usomi wako njoo na takwimu hapa kabla ya TCU online elim ilikuwaje?Ilipokuja TCU online ikawaje?

Kisha ndo uje na hitimisho.

Halafu kuhusu ada ya maombi mbona ilikuwepo hata siku za nyuma huko?

Mfano hata kwa level ya Masters ada ya maombi hutozwa kwa kila kozi unayoomba kwa chuo husika.Kama unaomba kozi tatu na ada ya maombi ni 20,000/- bas itakutoka 60,000/-.

Tatizo hayo mambo yalikuwepo ww ukiwa bado unasoma msingi, hata TCU hukuwa unaijua na nenda kasome kazi za TCU,kazi za TCU ni kusimamia vyuo vikuu kwa mujibu wa sheria za nchi,kudahili ni kazi ya CHUO,
TCU walipora majukumu ya chuo
 
Habari zenu wanajukwaa.
Hili andiko ilibidi nilipeleke jukwaa la elimu ila ni vyema lijadiliwe hapa kwa kuwa huyu anayeivuruga elimu ni mwana siasa.

Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu niliyeadiliwa kwa mfumo TCU online.

Juzi baada ya jpm kutoa kauli yake juu ya tcu kuwapangia vyuo wanafunzi wasio vitaka. Ila ukweli ni kwamba tcu haiwezi kumpangia mwanafunzi chuo ambacho hakuchagua na kikubwa zaidi inamsaidia mwafunzi aliyekosa ushindani kwa vyuo ulivyovichagua. Hili linaeleweka na waliodahiliwa kwa mfumo huu watanisaidia kuongezea hapa.

Sasa baada ya kauli ya rais wakati akifungua mabweni pale udsm. Tcu wameamua isiwe shida kila chuo kipokee maombi na kupeleka tcu baadae. Kwa jicho la haraka ni kwamba wanafunzi wengi watakosa vyuo na udahili huu utakuwa mgumu sana.mfano leo chuoni kwetu wametoa tangazo la kuanza kupokea maombi na ada ya maombi ni elfu 50.

Ina maana kama unataka kuomba vyuo zaidi ya kimoja ili kujiweka kwenye mazingira ya kutokosa chuo itabidi ulipie fomu ya kila chuo.. Wakati tcu online tulikuw tunalipia elfu 50 na kuomba vyuo vitano.

Sasa ili uombe vyuo vitano itabidi utumie 250000 hapo bado huna uhakika wa kupata nafasi kulingana na ushindani wakati tcu ulikuwa unalipia mara moja elfu 50.
Mapungufu ya mfumo huu ni mengi na hapa vyuo lazima vifanye udanganyifu na kuwadahili wanafunzi wasio na sifa. Yale ya miaka ya nyuma yanajirudi.

Serikali mjirudi na tcu waendelee kufanya udahili huu.. Na mapungufu yatakayojitokeza muwahukumu hawa tcu.


Ni mtizamo kwako tu. Waulize walipelekwa St. Joseph Songea kama waliomba na nini kimewapata.

Kuna wanafunzi walikuwa na ufaulu mzuri kabisa wakatupwa kusikojilikana kisa TCU.
 
Kuhusu hiyo elfu 50 ni rahisi tu; vyuo vipunguze gharama za fomu. Kama enzi za TCU ilikuwa elfu 50 then unaomba vyuo vitano; then kwa utarataibu huu "mpya" (sio mpya ndivyo ilivyokuwa zamani hizo) gharama ya fomu iwe 10,000/=; as simple as that.
 
Dogo, kabla ya mfumo wa udahili wa TCU online kulikua na udahili kupitia vyuoni,na baadhi ya vyuo vilikua havikudahili hadi ufanyr mtihani wao kama chuo, vingine havikua na huo mfumo.Na elim ndo hyo hyo.Mfumo wa TCU online ndo uloleta VILADHA ambao wamenyofolewa baadhi ya vyuo.Na mfumo wa TCU baadhi ya vyuo havikuupenda like UDSM so ndo wangefanyaje wakaukubali.MUM waliukataa na hawajawah kuutumia.

Labda kwa usomi wako njoo na takwimu hapa kabla ya TCU online elim ilikuwaje?Ilipokuja TCU online ikawaje?

Kisha ndo uje na hitimisho.

Halafu kuhusu ada ya maombi mbona ilikuwepo hata siku za nyuma huko?

Mfano hata kwa level ya Masters ada ya maombi hutozwa kwa kila kozi unayoomba kwa chuo husika.Kama unaomba kozi tatu na ada ya maombi ni 20,000/- bas itakutoka 60,000/-.

Tatizo hayo mambo yalikuwepo ww ukiwa bado unasoma msingi, hata TCU hukuwa unaijua na nenda kasome kazi za TCU,kazi za TCU ni kusimamia vyuo vikuu kwa mujibu wa sheria za nchi,kudahili ni kazi ya CHUO,
TCU walipora majukumu ya chuo
MKuu fikiria umepata division three ili ujiweke kwenye mazingira ya ushindani inabidi angalau uombe vyuo vingine kidogo!
Sasa fikiria walewale masikini huko vijijini ambao hata ile elfu 50 tu ulikua mtiti!
Imagine sasa lako na ushehe huko bado loan board!!
Ni Suala la muda tu wakupiga kelele kama anaumia atapatikana tu
 
Pamoja na Mapungufu yote hayo, ni njia nzuri zaidi kwani humpa mwanafunzi wigo mpana wa kuchagua Chuo cha hitajio lake. Hutumika sana nchi za Wenzetu huko Ughaibuni.

Ili kupunguza Swala la gharama zisizo na msingi, Nashauri yafuatayo yafanyike.
Moja, gharama za fomu za kuomba Udahili ziwe bure kabisa kwa kila chuo. Hii itasaidia wanafunzi kuepukana na gharama nyingi za kuomba udahili katika vyuo vingi. Badala yake, ada ya form Tsh 50,000 ilipwe na mwanafunzi ambaye amedahiliwa na kufanikiwa kusajiliwa katika chuo tajwa. Fedha hii ilipwe pindi wanafunzi waliodahiliwa kufika Chuoni wanapowasili kwa ajili ya Usajili.

Hii ni nzuri kwani itaepusha gharama zisizo na msingi kwa wanafunzi na walezi wao. Pia, vyuo vingi vinaweza kupokea fedha nyingi kwa mgongo wa fomu ya Udahili ilihali haina uwezo wa kuwadahili wanafunzi wote hao.

Pili, kila chuo kiwe na system yake ya Udahili online. Mfano, UDOM walitengeneza system ya kudahili mwaka jana. Vyuo vyote vitengeneze website ambayo itaweza kupokea taarifa pamoja na nyaraka mbalimbali za wanafunzi wanaoomba Udahili. Hii itasaidia kupunguza gharama za nauli pamoja na matumizi mengine kwa wanafunzi. Hii itamuwia ugumu sana Mwanafunzi kutoka Kigoma mwenye nia ya kusoma vyuo vya Dar es Salaam kutoka huko mpaka huku kwa ajili ya kuomba usahili. Gharama za usafiri pamoja na malazi ni kubwa sana. Ingelikuwa rahisi kama kila chuo kitakuwa na System yake.

Nawasilisha.
Nimependa mchango wako, nadhani serikali ya magufuli ni sikivu italifanyia kazi
 
Ni mtizamo kwako tu. Waulize walipelekwa St. Joseph Songea kama waliomba na nini kimewapata.

Kuna wanafunzi walikuwa na ufaulu mzuri kabisa wakatupwa kusikojilikana kisa TCU.
Shida iko hapa tatizo wanafunzi wengi wana amini akiwa n div one lazima aende udsm.. Sasa udsm itaweza kupokea wanafunzi wote wenye div 1. Hivyo hivyo muhimbili nafasi ni chache sana hawawezi kudahili wanafunzi wote waliofaulu vizuri... Mfano mwaka jana wanafunzi waliofaulu vizur na kuwa na sifa za kusoma udaktari walikuwa elfu 10 lakini nafasi zilizokuwepo kwenye vyuo vya serikali ni elfu 25 tu. Sasa hapa ukipangiwa kampala utalalamika?
 
Ni mtizamo kwako tu. Waulize walipelekwa St. Joseph Songea kama waliomba na nini kimewapata.

Kuna wanafunzi walikuwa na ufaulu mzuri kabisa wakatupwa kusikojilikana kisa TCU.
Asikudanganye MTU wengi waliopelekwa st Joseph walishindwa competition kwenye vyuo vya serikali kama udsm etc!
Nimesoma st Joseph kabla ya kuhama wengi waliopo pale tulikuwa na division three kwa upande wa science!
Sijui upande huo mwingine!
 
Dogo, kabla ya mfumo wa udahili wa TCU online kulikua na udahili kupitia vyuoni,na baadhi ya vyuo vilikua havikudahili hadi ufanyr mtihani wao kama chuo, vingine havikua na huo mfumo.Na elim ndo hyo hyo.Mfumo wa TCU online ndo uloleta VILADHA ambao wamenyofolewa baadhi ya vyuo.Na mfumo wa TCU baadhi ya vyuo havikuupenda like UDSM so ndo wangefanyaje wakaukubali.MUM waliukataa na hawajawah kuutumia.

Labda kwa usomi wako njoo na takwimu hapa kabla ya TCU online elim ilikuwaje?Ilipokuja TCU online ikawaje?

Kisha ndo uje na hitimisho.

Halafu kuhusu ada ya maombi mbona ilikuwepo hata siku za nyuma huko?

Mfano hata kwa level ya Masters ada ya maombi hutozwa kwa kila kozi unayoomba kwa chuo husika.Kama unaomba kozi tatu na ada ya maombi ni 20,000/- bas itakutoka 60,000/-.

Tatizo hayo mambo yalikuwepo ww ukiwa bado unasoma msingi, hata TCU hukuwa unaijua na nenda kasome kazi za TCU,kazi za TCU ni kusimamia vyuo vikuu kwa mujibu wa sheria za nchi,kudahili ni kazi ya CHUO,
TCU walipora majukumu ya chuo
Uzuri wa magu akisema anatulia, usimalize wino mkuu! TCU hii hii ambayo unageuza karakana kuwa chuo na wanakujazia wanafunzi idadi kubwa kuliko chuo kinachomeet standards
 
MKuu fikiria umepata division three ili ujiweke kwenye mazingira ya ushindani inabidi angalau uombe vyuo vingine kidogo!
Sasa fikiria walewale masikini huko vijijini ambao hata ile elfu 50 tu ulikua mtiti!
Imagine sasa lako na ushehe huko bado loan board!!
Ni Suala la muda tu wakupiga kelele kama anaumia atapatikana tu
Mdau kusoma ni gharama,acha kulalamika sana,umelipa ada shilingi ngapi kwa miaka mingapi uache kulipia 200,000/- kwa application ya kusoma?
Kwa sababu kama ni hivyo utasema mbona HESLB wanadai ada ya maombi?Hayo mambo yalikuwepo tangu huko nyuma, halaf pia vyuo havitatoza application fees ya 50K, watatoza elf 20 au 25.

Unapoliendea swala la elimu GHARAMA hazikwepeki hata kidogo,hata hii ELIM BURE YA JPM ina gharama pia.

Kama mtu anataka kwenda kusoma aanze kujipanga kuanzia sasa,
 
Back
Top Bottom