Rais Magufuli: Kama una korosho na huna shamba hutalipwa

Mambo mengine ni kudhulumu watu tu. Kama Korosho zilinunuliwa kihalali kwa makubaliano kati ya Mnunuzi na Mkulima kosa ama tatizo liko wapi. Mbona wauza mahindi wengi siyo wenye mashamba ya mahindi.

Dhana ya biashara hapa iko wapi? Na wachuuzi iwe ni Kangomba ama wowote wale wanatokana na mfumo mbovu na mbaya wa masoko kwa mazao ya Kilimo nchini mwetu. Dunia nzima wauzaji wa mazao mara nyingi huwa si wakulima. La maana watozwe faini kwa kufanya biashara bila ya kuwa na leseni.
Tatizo ni sera za Serikali yenyewe. Angalia mfano wa mahindi. Walizuia kuyauza nje ya nchi. Matokeo yake bei imeshuka mno. Sasa wamefungulia lakini hakuna soko tena. Waganda sasa ndiyo wanauza kwenye masoko ya Tanzania.
Ndiyo maana mkulima anaweza kuuza hayo maua apate chochote kuliko akose kabisa.
Serikali iwe mteja wa mahindi kama wengine.
 
Tulia kidogo, hebu fikiria ukipeleka kitambaa cha nguo kwa fundi...ile anaanza kukata kata huwezi elewa nini kinatokea baadae! jamaa naona anakata kata! Hizi hela za madalali wa kangomba ndio huwa zinawanunulia mama zetu kanga na vilemba vya "Chagua CCM" matokeo tunawakilishwa na akina ......ndiyoooooooo!
True wacha wakae sawa si waliandamana
 
Kiongozi ana viashiria vya umaskini ndani yake.....

Tulikosea sana kumpa nchi mtu mbinafsi kama huyu...
Uzalendo kwake ni kuwa masikini, kipaumbele chake ni kuzalisha mashetani, uchumi wa viwanda ni wimbo wa majukwaani wa kujenga viwanda kwenye makaratasi
 
Hawa viongozi Hivi hawajawahi kuishi maisha ya kawaida ya huko vijijini unakuta mkulima wakati wa kuandaa shamba Lake hana hela anakwenda kukopa kwa hao kina kangomba?

, wamejiandaa kuwakopesha. Wakulima wakati watakapokuwa na uhitaji?
Ndio maana wanasema kweli serikali ni chombo cha mabavu.
Wanajua nini Hawa ndomana wanampelekea rais taarifa tofauti

Ova
 
Jamaa ni dhulumati sana mpaka rambirambi anachikichia huyu mtu sembuse awalipe korosho?Hao wakulima wasikilizie maumivu.Na hiyo hela ya mauzo ya korosho hata mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali anaweza asizione kwenye hesabu zake!
Wataikumbuka wafanyabiashara, achelewi kuwaambia hela imeenda kujenga SGR
 
Angesema mapema Hakuna kagoma angeonana na wabangua korosho, angeuza zake msumbiji
Hahhahahhah unyang'anyi wa wazi kabisa.

Yeye angenunua tu korosho za wakulima hao wengine awaachie korosho zao.
 
Tatizo ni sera za Serikali yenyewe. Angalia mfano wa mahindi. Walizuia kuyauza nje ya nchi. Matokeo yake bei imeshuka mno. Sasa wamefungulia lakini hakuna soko tena. Waganda sasa ndiyo wanauza kwenye masoko ya Tanzania.
Ndiyo maana mkulima anaweza kuuza hayo maua apate chochote kuliko akose kabisa.
Serikali iwe mteja wa mahindi kama wengine.
Mbaazi sahv ndy bye bye
Ishafukiwa kaburini na hatujawahi skia serikali ikitaka ipiganie mbaazi irudi kwenye mstari,mpaka Sasa wakulima wa mbaazi wanalia njaa alafu hpo utasema serikali ina huruma na mkulima

Ova
 
Umasikini ndio vipaumbele vyao vikuu ili iwe rahisi kuwatawala hakuna rangi tusiyoiona.Akubaliki duniani wala mbinguni
Tatizo ni sera za Serikali yenyewe. Angalia mfano wa mahindi. Walizuia kuyauza nje ya nchi. Matokeo yake bei imeshuka mno. Sasa wamefungulia lakini hakuna soko tena. Waganda sasa ndiyo wanauza kwenye masoko ya Tanzania.
Ndiyo maana mkulima anaweza kuuza hayo maua apate chochote kuliko akose kabisa.
Serikali iwe mteja wa mahindi kama wengine.
 
  • Hofu yangu ni kwamba mkishikilia korosho za mtu wakati alizinunua kwa makubaliano na mkulima, je itakuwa ni haki kweli?, maana mkulima ana haki ya kuuza korosho yake hata kwa shilingi mbili kwa kilo,maana ni mali yake
  • Hii practice ya Kangomba imeanza leo baada ya sakata la korosho au imekuwepo toka misimu iliyopita na je serikali ilifanya nini?
  • Kama mkulima anahitaji hela ya kwenda hospitali, kulipia ada ya mtoto akaweka bondi korosho zake then huyu aliyelipwa kwa korosho ana kosa gani?
  • Je ni kinyume cha sheria kumiliki korosho bila kuwa na shamba?
  • Je Kangomba ni kinyume cha sheria ya nchi, sheria gani hiyo?
  • Kama serikali haiwezi kuwalipa wenye korosho si iwaachie korosho zao wakaziuze wanapoona zinafaa, kwa nini serikali izishikilie?
  • Kama kangomba ni kinyume cha sheria ya nchi mbona hamjawakamata hao waliovunja hiyo sheria na kuwafikisha mahakamani?, na kama ni viongozi mbona hamjawapeleka kwenye tume ya maadili ya viongozi?
Mbona kila wakati unatafuta tu kosa ambalo serikali linafanya? Sikukuona kuwa mstari wa mbele kuwalaum hao wafanya biashara ambao walikuwa wana suasua kununua korosho ya mkulima mnyonge? Baada ya serikali kutoa umuzi wa kuwasaidia wakulima ambao walikuwa desperate, wewe ndiyo una kuja na Mambo ya kutaka kuonyesha unajua kuliko hata serikali.

Achana na fikra za kikoloni hizo. Ipende nchi yako na watanzania wenzako, hata kama sio ndugu zako, ni watanzania wenzako. Mkoloni na hao wafanya biashara wako hawana mpango na sisi na pia na maendeleo ya nchi yetu. Wanalimbikiza hela zao nje kwa manufaa yao na mabepari wenzao.

Hao ndiyo waafrika ambao Puttin kawazungumzia. Wana enjoy maisha ya kizungu lakini wakifa mizoga yao ndiyo inaletwa kuwa dumped in Anfrica.

Soma history ya George Stephenson na mtoto wake Robert Stephenson

George Stephenson - Wikipedia

nafikiri utajifunza mengi juu ya uzalendo na mapenzi kwa wananchi wenzako.
 
wewe ndiyo una kuja na Mambo ya kutaka kuonyesha unajua kuliko hata serikali..
Kwani serikali si inaongozwa na watu tena na wanasiasa ambao kikawaida wanaongozwa zaidi na maslahi yao kuliko ya wenzao.

Hivi si serikali ndiyo ambayo ilisema kuwa fedha za ESCROW si mali ya Umma?
 
Mbona kila wakati unatafuta tu kosa ambalo serikali linafanya? Sikukuona kuwa mstari wa mbele kuwalaum hao wafanya biashara ambao walikuwa wana suasua kununua korosho ya mkulima mnyonge? Baada ya serikali kutoa umuzi wa kuwasaidia wakulima ambao walikuwa desperate, wewe ndiyo una kuja na Mambo ya kutaka kuonyesha unajua kuliko hata serikali.

Achana na fikra za kikoloni hizo. Ipende nchi yako na watanzania wenzako, hata kama sio ndugu zako, ni watanzania wenzako. Mkoloni na hao wafanya biashara wako hawana mpango na sisi na pia na maendeleo ya nchi yetu. Wanalimbikiza hela zao nje kwa manufaa yao na mabepari wenzao.

Hao ndiyo waafrika ambao Puttin kawazungumzia. Wana enjoy maisha ya kizungu lakini wakifa mizoga yao ndiyo inaletwa kuwa dumped in Anfrica.

Soma history ya George Stephenson na mtoto wake Robert Stephenson

George Stephenson - Wikipedia

nafikiri utajifunza mengi juu ya uzalendo na mapenzi kwa wananchi wenzako.

Nyie ndiyo mtaji wa fisiemu, wew na ukoo wako wote muendelee kutawaliwa na mtu kama jiwe
 
Ni mpaka 2027 penda usipende, majiizi na wapiga madili waendelee kulia tu! 2025/2026 tutashuhulika na katiba mpya, 2027 ndiyo itumike kwa uchanguzi mkuu(general election)! In short Dr Magufuli ni mpaka 2027. 2020 anapita bila kupingwa!


Unajuwa nimecheka...hivi majizi ni akina nani?
Rambi rambi mmenyakuwa
1.5trion mmenyakuwa
Korosho mnakwapua ..sasa wezi apa ni akina nani?
 
Huyu aliye kutwa na korosho bila shaka ndie aliye zitunza sabab wakulima wengi hawana mitaji,nawati huo serikali inakua haiko karibu kabisa na mteja na serikali haiwezi kumpa mkulima pesa ya matunzo huyu jamaa mliye mkuta anakorosho ndie anae msaidia mkulima toka ni toke yaani kwa lugha nyepesi wanatunza wote mwingine anashamba mwingine anapesa.bila shaka zao hilo linawakatisha tamaa wakulima na watunzaji
Kama hujui kitu uliza upewe uelewa.usikurupuke
 
Mambo mengine ni kudhulumu watu tu. Kama Korosho zilinunuliwa kihalali kwa makubaliano kati ya Mnunuzi na Mkulima kosa ama tatizo liko wapi. Mbona wauza mahindi wengi siyo wenye mashamba ya mahindi.

Dhana ya biashara hapa iko wapi? Na wachuuzi iwe ni Kangomba ama wowote wale wanatokana na mfumo mbovu na mbaya wa masoko kwa mazao ya Kilimo nchini mwetu. Dunia nzima wauzaji wa mazao mara nyingi huwa si wakulima. La maana watozwe faini kwa kufanya biashara bila ya kuwa na leseni.
Lipo tatizo kubwa la ukenfeufu wa kiwango kisicho cha kawaida katika nchi hii. Kama wauza korosho hawatalipwa wala kuachiwa wauze korosho zao kwingineko eti sababu hawawezi kuthibitisha umiliki wa mashamba ya korosho, basi huu utakuwa ni unyangayi kwa kutumia silaha. Dhambi hii haitamwacha magu na serikali yake salama. Jasho la mtu ni sumu ya kufisha. Dhuluma na udhalimu havilipi na ni laana kwa taifa zima!
 
Back
Top Bottom