Rais Magufuli kama Tanzania ni Tajiri mbona una suasua kumwaga pesa kwenye miradi mingi yenye tija?

Nchi yetu ina karibia miaka 60 sasa, huo utajiri wa rasilimali tuko nao toka dunia imeumbwa, mbona hatuoni ukiakisi kwenye maisha ya wananchi waliowengi? Ina maana miaka yote 60 hatujajua njia nzuri ya kuutumia huo utajiri? Huu ni mwaka wa tano wa Magufuli madarakani, mbona huo utajiri bado haujaakisi zaidi ya deni la taifa kupaa kutokana na mikopo? Naomba iwekwe vizuri, nchi yetu ni tajiri au nchi yetu ina rasilimali nyingi? Maana naona hili neno utajiri linatumika kama Hadaa ya kiki ya kisiasa. Unapowaambia watu nchi ni tajiri lakini vijana hawana ajira, na wanaokubali nchi ni tajiri ni wale walio katika vyeo vya ulaji, ni kama kuwasanifu wananchi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana. Umenifanya nitokwe na machozi. Umenigusa sana.

Kwa nini hasa sisi watanzania tunashindwa kutumia rasilimali zetu kujiendeleza wenyewe?

Kwa Statements zako hizo ndiyo hizo zinanifanya nimlaumu Magufuli ninapo ona akiwafokea watanzania wa vijijini kuwa walime ili wazalishe mazao mengi! Kitu ambacho yeye hajakitambua ni kwamba hawa watu wamekuwa so paralize kiasi kwamba hawaelewi anacho maananisha.

Wazalishe kwa dhana zipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwenye kilimo hali ni mbaya sana na sioni namna tunaweza kutoka hasa hasa nikiangalia midset za wakulima wetu na wafanyakazi wa serikali kule wizara ya kilimo na halimashauri zetu ,last year nilipata nafasi ya kuhudhuria mkutano wa wadau wa kilimo mkoani Iringa, kuna mdau mmoja aliombwa na serikali kujenga kiwanda cha kuprocess nyanya pale Iringa kwa madai kwamba kuna nyanya nyingi,mzee akajenga kiwanda chenye uwezo wa kuprocess tan 200 a day,Guess what? jamaa anaoperate only two months a year kwa sababu nyanya hakuna,wakulima hawana elimu wala technology, Sasa jamaa yuko busy anajenga SGR,SGR haitengenezi pesa,kinachotengeneza pesa ni kile kinachosafirishwa na SGR,sasa angalia production kama hii ya huyo mdau hiyo SGR itasafirisha nini
 
Awali ya yote naomba kuchukua nafasi hii kwanza kumshukuru mungu wa wingi wa rehema kuniwezesha mimi na wapendwa wangu nchini na ughaibuni hasa Ujerumani kuuona mwaka huu mpya wa 2020. Pili nampongeza Rais wetu Mpendwa JPM na watendaji wake wote wa serikali anayo iongoza na ambao wako mstari wa mbele kushirikiana naye katika jitihada anazo zifanya za kuliletea Taifa letu maendeleo ya kweli ambayo yatatuwezesha sisi na nchi yetu kwa ujumla kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Nawatakia baraka njema nua maendeleo mema ya kulijenga taifa letu kwa mapenzi yao ya dhati.

Pamoja na hayo yote hata hivyo napata kigugumizi kidogo Rais wetu ninapo sikia kauli zako kama hizi za kudai kuwa Tanzania ni tajiri. Kama Tanzania ni tajiri, swali langu ninalo jiuliza ni kwa nini sasa una suasua kumwaga pesa nyingi kwenye miradi mingi yenye tija?

Nashangaa na kustaajabu nchi kama China ambayo haina rasilimali nyingi kama sisi kuwa nchi moja wapo ambayo imekusudia kutumia nguvu zake zote, pamoja na kuwa na madini ya chuma kidogo, kipindi cha takribani miaka kumi na tano tu, kuwekeza kwenye kueneza SGR nyingi na za masafa marefu nchi nzima, wakati sisi katika kipindi cha miaka mitatu sasa bado tuna suasua na ka SGR kamoja, hata ule umbali wa kilometa chache mpaka Mororogoro hatuja maliza.
Sasa kama sisi ni matajiri kweli, kama unavyo dai, kwanini tushindwe kumwaga pesa nyingi kwenye miradi mingi tofauti ya maendeleo ili vijana wetu wasio na ajira, wanao zurura zurura tu mijini baada ya masomo yao, wakapata ajira na pia utaalam ambao uta iwezesha nchi yetu kusonga mbele? Kitugani kina kuzuia kufanya hivyo?

Rais Magufuli nakuomba utambue kuwa wewe mwenyewe mara nyingi umekuwa ukiutangazia ulimwengu na kuwaaminisha watanzania kwamba nchi hii ni tajiri na utajiri huu unatokana na kuwa nchi yetu kujaliwa kuwa na depo kubwa ya madini ya aina tofauti yakiwemo, dhahabu, almasi, chuma, gas asilia, Uran, cobalt, graphite, helium, makaa ya mawe na madini ya vito kama Tanzanite, Rubin na kadhalika vile vile Mbuga za wanyama kem kem, mito mingi, maziwa na Mlima Kilimanjaro juu na kwamba uchumi wake unakua kwa asilimia saba point moja, lakini nikiangalia hizo projects ulizo zianzisha na utekelezaji wake na ukuaji wa uchumi kwa asilimia hizo, naona mambo bado hayaendani pamoja vile!

Infact kimaisha watanzania wengi ambao kipato chao bado ni cha chini mno wanapata shida sana. Hiyo miradi yako uliyo ianzisha bado haina impact yeyote kubwa kwao kiasi kwamba wakajenga matumani ya kuona mwanzo wa maendeleo mbeleni ili nao waanze sasa kuwa katika position yakujenga mentality au state ya kuanza kujiamini kwa mambo mengi wanayo yafanya.

Nimemsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango, Waziri Mpango, alivyo toa hotuba yake ya kufunga mwaka juu ya hali ya uchumi wa nchi yetu na kutoa Statement ya madeni ambayo nchi yetu inakabiliana nayo.

Hotuba yake kusema kweli ilinipa matumaini makubwa sana baada ya kusikia kuwa total amount ya madeni yetu yote ya ndani na ya nje ni about 54.84 Trillion TSHs. Hii amount ukiibadili kwenye US Dollar, unapata 25.76 Billion US Dollar. Tokitoa ile amount ya 6 Billion US Dollar ambayo Serikali ime i deposit kweye National General Reserve tuna bakiwa na tofauti ya US Dollar Billion 19.76.

Sasa nikijiuliza, what is 20 Billion US Dollar kwa nchi yenye population ya watu zaid ya milioni 56.5 na Resources zote hizo ambazo inayo? Jibu lake ni kwamba kila mtanzania ana deni la US Dollar 354 ambalo ni sawa sawa na TSHs laki 7 na nusu. Yaani, mmh, "It is nothing!"

Nikiangalia Debt-to-GDP Ratio yetu ambayo kwa kulingana na Statement ya Waziri Mpango ni 27.2%, kama sijakosea, naona bado tuna capacity kubwa sana ya kuweza kuchukua mikopo mingine mikunwa ambayo itatuwezesha sisi kugharamia miradi mikubwa yenye kuleta impact kubwa kwa wananchi na hivyo kuongeza kipato chao na hatimaye kuleta maendeleo makubwa kwenye Taifa letu kwa haraka zaidi.

Kwa uwezo huu tulio nao kirasilimali na Buffer ambayo bado tunayo ya kuendelea kukopa zaidi sioni sababu ya serikali kuendelea kusuasua kukopa hela nyingine zaidi ili kuongeza capacity ya uzalishaji wa bidhaa ambazo tunaweza kuziuza na kuleta maendeleo yetu kwa haraka zaidi.

Mimi binafsi sioni ulazima wa serikali yetu kuwasubiri wagenu au makampuni kutoka sekta binafsi waje kuwekeza kwenye uchimbaji wa madini yetu na kuyasafirisha nje kwa ajili ya ku make profit zao tu nje, nchi yetu hivi sasa inahitaji wataalam wake wenyewe ambao wanajua njia mbalimbali za kutumia madini yetu ya chuma, dhahabu, gas yetu asilia, graphite na mengineyo kutengeneza vitu mbali mbali vyenye thamani kwa mahitaji yetu wenyewe na kuuza nje.

Follow up ya takwimu hii hapa juu ya nchi zilizo wahi ku produce chuma kwa wingi duniani, inaonyesha kuwa, kuwa na chuma ni maendeleo ya nchi pia. Bila chuma ni vigumu nchi kuwa na watu wenye spirit ya kubuni vitu ambavyo vitaiwezesha jamii ku improve maisha yao kwa haraka zaidi. Hivi sasa China inaongoza kwa uzalishaji wa chuma, na ndiyo maana ni nchi inayo ongoza dunia kiuchumi pia. Chuma inawapa wananchi uwezo wa kuthubutu mambo mengi yanayo husu maisha yao.

Kuifanya nchi yetu iwe ya uchumi wa kati, sio hali ambayo italetwa kwa kujenga barabara, madaraja na fly overs, mahospitali na majengo ya shule na mahakama peke yake au kutoa huduma za elimu na afya bure, bali pia ni hali ambayo italetwa na investiment kubwa ya serikali kwenye mambo mengi tofauti yakiwemo; ujenzi wa vinu vya kuoka chuma nchini, mtambo wa kusindika gas asilia, Refinery ya mafuta na mengineyo ambayo yata changamsha bongo za watanzania kuhusu matumizi ya products zake na hivyo kuwa na Taifa lenye vijana wengi ambao wana participate kwenye product creation na hivyo kukuza uchumi wa ndani na kuboresha maisha ya watu na vitu na hatimaye maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Kama Dangote mzawa wa Nigeria anatengeneza Refinery kubwa Nigeria ili kuondoa matatizo ya uhaba wa mafuta nchini kwake na ku create Jobs kwa jamii yake, ina kuwaje serikali kama hii yetu inayo simamia mali asili zetu zote ishindwe kugharamia kitu kama hiki kwa about 12 billions US Dollar?

Nchi yetu ili ije kuwa na uwezo wa ku creat products zenye thamani kubwa kwa kutumia mali ghafi yetu wenyewe kama ya chuma, dhahabu na mengineyo, inahitaji watu waitwao smithy, mechanical engineers, chemical engineers, Process Engineers, Design Engineers, product designers na industrial designers. Hawa ni watu ambao wana uwezo mkubwa wa kuipa mali ghafi yetu directly thamani kwa kuyabadilisha madini hayo kuwa products ambazo zina weza kutumiwa na binadam.
Wataalam wa aina hii watakuwepo kwa wingi kutegemeana na urahisi na wingi wa upatikanaji wa mali ghafi nchini kama chuma, dhahabu, gas asilia na kadhalika na pia serikali kulisimaia hili swala kimkakati.

Rais Magufuli nakuomba tumia serikali yako kutuvusha sisi. Wewe ndiyo Rais uliye jaliwa na mungu kuja kuwaokoa watanzania. Kwenye nchi yetu Mzee amini watanzania wanacho sema, hakuna mtu wa mfano wako, mtu mwenye power ya kuchukua maamuzi magumu na mazito kama unavyo fanya.
Rais wetu wa awamu ya pili Rais Ali Hassan Mwinyi amediriki kusema haya;
Hiyo sio uongo anacho kisema. Ni ukweli mtupu. Hakuna matanzania ambaye ameweza kuwa na uwezo na ushujaa wa kutenda mambo hayo unayo yafanya na wala hatutegemei baada yako kama itakuwa rahisi kumpata mtu wa calibre yako. Wewe so far ni mtu wa pekee nchini mwenye ku embrace sifa hizi. Una maono ya mbali na ujasiri wa kipekee.

Nakuomba tumia uwezo wako na kipaji chako ambacho mungu kakujalia kuwaongoza watanzania ili kutufikisha mahali ambapo itakuwa rahisi sisi wenyewe kujiendeleza zaidi, bila kuteteleka. Endelea hivyo hivyo na msimamo wako Mzee. Watanzania walio wengi wana kuhitaji sana wewe kwa maisha yao na ya vizazi vyao vya baadae.

Tumia nguvu zako na karisma yako kumwaga pesa kwenye miradi itakayo waletea watanzania uwezo wa kujiendeleza wenyewe pindi tutakapo kuwa peke yetu bila wewe. Wewe ni mzalendo wa kweli kwa nchi yako, wewe ni upendo na nuru ya matumaini ya watanzania wengi. Nakuomba tafadhali usituache njia panda. Waongoze watanzania kwenye maendeleo ya kweli ili tuje ku rejoyce na wewe mbeleni kwa kulifanya Taifa letu, ambalo lilikwisha tabiliwa kifo, kuinuka tena na kuwa Taifa la kutambulika na kuheshiniwa Duniani.

Pindi watanzania watakapo pata nguvu na ufahamu wa kujiamini na kuchukua maamuzi yao wenyewe mikononi mwao kwa maendeleo yao, watanzania watalitukuza sana jina lako nakulifanya litambulike milele, kama Alexander The Great wa wagiriki na Virgin Queen Elizabeth I. wa England.

Watanzania tumeteseka sana na kuwa intimidated kwa mda mrefu sana na watu wachache ambao tuliwaamini kuwapa madaraka ya kutuongoza, tukitegemea kuwa ni watu ambao wangetuendeleza sisi kiuchumi, badala yake walionekana kuwa ni mabogus walio mind sana maisha yao, ya familia zao na marafiki zao kuliko maisha ya wengi ambao tulikuwa tuna sota na kukosa mwelekeo thabiti.

Kuja kwako Rais Magufuli sisi watanzania tulio kuwa upande wa ma looser, tumeanza kuwa ni watu ambao tunaanza taratibu kupata imani ya kuuona mwanga wa maendeleo, japo kuwa sio kwa kiasi kikubwa, ila tendence tunaziona. Yasimamie maendeleo na mafanikio yetu ya uchumi na maisha kwa moyo mmoja, kwani kama sio wewe nadhani hivi sasa Mzee, tungekuwa katika mkondo mwingine wa maisha. Tulikuwa kwenye margin ya kuliangamiza Taifa letu sisi wenyewe.
Shukran na pongezi nyingi zikujie wewe Rais wetu kwa kuleta stability kwenye jamii yetu.

Mbali na hayo ingekuwa busara kwa serikali yako kuhimiza kwa kasi kubwa mno SGR ya Southern Corridor kati ya Mtwara na Mbamba Bay pia SGR ya kutoka Mtwara mpaka Tanga kupitia DSM, Bagamoyo na Pangani. Ikiwezekana, badala ya kujenga daraja la baharini kama wana diaspora wa Ulaya huko Sweeden na Norway walivyo pendekeza, lingejengwa Tunnel kati ya Bagamoyo na Zanzibar kama lile la Eurotunnel kati ya Calais na Dover.

Kwa kutekeleza hayo ninauhakika mkubwa miji na vijiji vingi vya Malawi kama Nkhata Bay, Mzuzu, Nkhotakota na mingineyo ambayo haina infrastructure nzuri, SGR hii inge boost kwa haraka sana hali ya masha ya watu wa kusini na kuiingizia Taifa pato la kutosha. Vile vile SGR ya costal Coridor Mtwara, DSM na Tanga na Tunnel la Bagamoyo Zanzibar inge warahisishia maisha sana watu wakusini na watu wa kando kando ya pwani ya Bara na Visiwani kwa kuweza kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi na haraka zaidi.

Miradi kama SGR, Suspension au Sky Train, Commuter Train na Trams sio tu iko kwa kwaajili ya Transportation System Service bali pia ni uenezaji wa karakana ambazo zitatoa ajira kubwa na utaalam mkubwa kwa wananchi na hasa vijana.
Kuwekeza kwenye miundo mbinu hii, Taifa letu litafaidika kwa kiasi kikubwa sana kiutalaam.

Ikumbukwe kuwa baada ya serikali ya Ujerumani ku introduce train ya kwanza kati ya Fürth na Nürnberg mwaka 1835, Daimler Benz miaka 50 baadae aligundua gari la kwanza duniani. Hii ina imply kwamba baada ya technology transfer ya train kutoka Englang kwenda Ujerumani, Transformation procces yatechnology ilianza kuchukua mkondo wake.

Waturuki ambao wengi wao wanafanya kazi kwenye viwanda vya uzalishaji magari na trains ujerumani, wali peleka technology ya kutengeneza magari na reli kwao na sasa hivi wamekuwa wataalam wa kujenga reli za kimataifa wao wenyewe. Na pia wameanza kutengenezaji magari yao wenyewe kwao. Kwa wachina mambo nako ni hivyo hivyo.
"I conclude that the process of technology transformation is inevitable wherever the technology transfer takes place!"

Kama nilivyo dokeza hapo awali Rais Magufuli, kitu kingine ambacho ungekitazama kwa makini sana ni uwezo wa watanzania wengi hasa wa vijijini na mikoani wa kutumia dhana za kisasa katika kuzalisha mazao kwa wingi. Kusena kweli, uwezo wao sio mkubwa sana.

Haitakuwa busara kuendelea kuwahimiza wazalishe mazao mengi kwa nyenzo ambazo zimepitwa na wakati na methodes ambazo tumerithi kutoka kwa mabavu zetu. Katika hili ingekuwa busara kwa serikali yako kumwaga pesa kwenye kuwawezesha wakazi na wakulima wa vijijini na mikoa duni kutumia vifaa vya kisasa ambavyo vitawawezesha wakulima hao wasio na uwezo mkubwa wa ku afford dhana za kisasa, kuwa na access ya hizo dhana, aidha kwa kuazima au kukodi kutoka halmashauri za vijiji au mitaa yao.

Hii itakuwa motisha kubwa sana kwao na hasa kwa vijana wa vijijini kuwa na uwezo wa kuzalisha mazao kwa wingi ambayo yata wawezesha wao "kutoka", badala ya kwenda mijini kutafuta riziki zao kwenye shughuli za umachinga au waendesha Bodaboda na mabajaji.

Watanzania wengi bado hawako vizuri katika uzalishaji kwa dhana za kisasa, kwa sababu wana kosa maarifa ya kutumia dhana hizo na hii inasababishwa na ukosekanaji mkubwa wa upatikanaji wa hizo dhana, hasa tukizingatia udogo wa kipato chao kuweza ku afford hizo dhana.

Itambulike kuwa mda mrefu wakulima wetu wamekuwa katika state ya helplessness kwa sababu ya vikundi vya wahaini ambavyo permanently vimekuwa viki wa intimidate na kuwa-terolize kwa hili au lile. Na kwa vile sisi watanzania kwa ujumla wetu sio jamii ambayo tumelelewa kwenye misingi ya ku revolt, tunakubali tu, japo kwa masikitiko makubwa, kuburuzwa kama punda na hao walio jiita watawala au mashirika.

Kwenye miji mikubwa kama DSM na mingineyo, serikali yako haina budi kuwekeza kwenye majengo marefu ya gorofa ya makazi ili kupunguza upanukaji wa miji kwa haraka na ujengaji wa nyumba holela holela. Garden kwa ajili ya akina mama au familia na watoto wao kucheza na kuwa na free time karibu na maeneo ya makazi yao ni kitu muhimu sana katika maisha ya binadam.
Miundombinu ya sewage system nayo ni very crucial. Najua umeplan hivyo lakini inatakiwa utekelezaji utokee kwa kasi kubwa ili wananchi wafeel impact yake kwa haraka.

Natambua ya kwamba miradi kama hii yote haiwezi kufanyika bila pesa, ndiyo maana nimesisitiza hapo awali kuwa serikali lazima ichukue mikopo mikubwa ili kuwa na uwezo wa kuitekeleza miradi hiyo. Vinginevyo naomba tusijidanganye wenyewe, sioni uwezekano wowote ule wa nchi yetu kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati 2025 bila mkazo wa serikali. Hiyo itakuwa ni Illusion!

Serikali yetu chini ya uongozi wako Rais Magufuli ndiyo taasisi au chombo pekee kilichopewa dhamana ya kikatiba ku safeguard na kuleta maendeleo ya maisha ya watanzania kwa kutekeleza hayo yote ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma za msingi kulingana na kanuni za haki za binadam duniani.

In the long run hatuna cha ku loose, kwani capacity ya kukopa bado iko kubwa na potential ya kulipa madeni yetu tunayo pia, hata kama lingekuwa deni la US Dollar bilioni 500, kwa mali asili na rasilimali tuliyo nayo tungemudu kulipa pasipo na shaka.
Na zaidi ya hayo, who knows, pengine kuna genariton itatokea ambayo itakuwa na ubunifu mkubwa wa uzalishaji na uuzaji wa products ambazo wame zi develop wenyewe!

Mwisho wa yote nakuomba Rais wetu mpendwa kutosita kumwaga pesa za maendeleo katika miradi mbali mbali itakayo tuletea utaalam na kupunguza uhaba wa ajira kama tulio nao sasa kwa vijana wetu.

Watanzania wengi bado hatuna ile spirit ya kujituma na kufanya kazi kwa kujitambua na ufanisi zaidi kama watu wa mataifa mengine yaliyo endelea. Bado tuna attitude ya kupenda mtelemko, kwani imechukua vizazi vya generations tatu mpaka kuja kwenye hali hii tuliyo nayo, haitakuwa rahisi Taifa lenye mentality kama hii yetu kuweza kupata ufahamu wa kujituma kwa haraka katika kipindi cha Generation moja. Ili tuvuke kiuhakika tunahitaji mda wa Generations kama mbili hivi.

Kufanikisha mambo yatendeke katika ulazima sioni kama ni busara. Taifa lenye watu wengi kama letu, linahitaji Process ndefu na ya utulivu ili kubadilisha akiri na fikra za watu. Mambo mengi yanayo husu maisha yetu yanahitaji maono na utayari wa wananchi wenyewe. Sipirit yetu ya uwajibikaji bado iko nyuma sana kwa sasa na ndiyo maana vijana wetu wako radhi kuacha kila kitu pindi wanapo pata nafasi za kwenda ughaibuni!!!




Sent using Jamii Forums mobile app

Du shule za siku mnaenda kusomea nini jamani? Magufuli huwa anasema tuna utajiri ambao haujawa utilized na siyo kuwa uchumi wetu umekua na kulingana na nchi tajiri zilizonendela!! Haya mambo mbona nakumbuka sekondari tulisoma sana, mpaka nakumbuka national exam kulikuwa na swali moja lilikuwa linauliza: ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''!
 
Barabara ya kimara kibaha kilometa 17 tu sasa inakata mwaka na haijulikani itamalizika lini,sasa imagine ingekuwa kilometa mia,si ndo ingefika mpaka 2030?Sometimes nikikutana na jamaa wa kusifu na kuabudu huwa naisikitikia sana Tanzania.
Du shule za siku mnaenda kusomea nini jamani? Magufuli huwa anasema tuna utajiri ambao haujawa utilized na siyo kuwa uchumi wetu umekua na kulingana na nchi tajiri zilizonendela!! Haya mambo mbona nakumbuka sekondari tulisoma sana, mpaka nakumbuka national exam kulikuwa na swali moja lilikuwa linauliza: ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''!
 
... unafanya makusudi na kuchukua kauli ya JPM out of context, literally Rais hua anamaanisha utajiri wa nchi in terms of natural resources ambazo nchi yako imejaa liwa na Muumba.

Wakati maana ya utajiri unaotaka kulazimisha kuwa JPM alimaanisha ni ule wa high levels za HDI yaani hali nzuri ya juu ya maisha ya mtu mmoja mmoja. The means justfy the ends; JPM anasema tunatakakiwa kulinda na kutumia resources zetu vizuri ili na sisi tufikie level hizo za juu za HDI kama wenzetu wa nchi za Scandinavia, walivyofanya..

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ni ukomo wa mawazo yao usiwalaumu sana. Rais Magufuli huwa anasema tuna utajiri ambao haujawa utilized na siyo kuwa uchumi wetu umekua na kulingana na nchi tajiri zilizoendelea!! Haya mambo nakumbuka sekondari tulisoma, mpaka nakumbuka national exam mwaka fulani kulikuwa na swali moja lilikuwa linauliza: ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''! Sasa hawa wagambo wa kukariri wangekumbana na swali kama hili wangetoka flat!
 
Du shule za siku mnaenda kusomea nini jamani? Magufuli huwa anasema tuna utajiri ambao haujawa utilized na siyo kuwa uchumi wetu umekua na kulingana na nchi tajiri zilizonendela!! Haya mambo mbona nakumbuka sekondari tulisoma sana, mpaka nakumbuka national exam kulikuwa na swali moja lilikuwa linauliza: ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''!
Haya unaongea wewe si magufuli lakini pia kama unadhani matango pori uliyolishwa na mwalimu wako kwenye shule ya kata ndo ukweli huo I am so sorry for you
 
Hukumsikia Mhe. Mbowe Mkt Chadema aliposema Tanzania sio masikini???? Hata Biblia inakataza kukiri umasikini kwani Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa masikini ili sisi tuwe matajiri.

Queen Esther

Sent using Jamii Forums mobile app
[/QUOTE]
 
Haya unaongea wewe si magufuli lakini pia kama unadhani matango pori uliyolishwa na mwalimu wako kwenye shule ya kata ndo ukweli huo I am so sorry for you
Weweeeee. Mimi nilisoma shule ya kata? Weweeee. Acha kabisa! Elimu yangu ya sekondari tu nina uhakika wewe hata ufike chuo kikuu, uchukuwe degree ya masters, hutafikia uelewa wangu niliokuwa nao nilipomaliza form six. Ungekuwa una uelewa mdogo tu usingeshindwa kuelewa rais anamaanisha nini na siyo matango pori. Ona swali la mtihani hili... nililijibu vizuri na kupata A kwenye somo husika, tena form four. ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''!
 
China imekataa kuwa siyo nchi tajiri. Imesema wananchi wake wengi bado ni maskini. GDP yao ni kubwa kutokana na uwingi wa watu na ukubwa wa nchi. China ni mchi ya 89 Duniani katika maendeleo ya watu.

Cha ajabu ni kuwa wakati China inasema bado ni nchi maskini, Tanzania inasema ni nchi tajiri!!
Why not? The sky is the limit!
Queen Esther
 
Nchi yetu ina karibia miaka 60 sasa, huo utajiri wa rasilimali tuko nao toka dunia imeumbwa, mbona hatuoni ukiakisi kwenye maisha ya wananchi waliowengi? Ina maana miaka yote 60 hatujajua njia nzuri ya kuutumia huo utajiri? Huu ni mwaka wa tano wa Magufuli madarakani, mbona huo utajiri bado haujaakisi zaidi ya deni la taifa kupaa kutokana na mikopo? Naomba iwekwe vizuri, nchi yetu ni tajiri au nchi yetu ina rasilimali nyingi? Maana naona hili neno utajiri linatumika kama Hadaa ya kiki ya kisiasa. Unapowaambia watu nchi ni tajiri lakini vijana hawana ajira, na wanaokubali nchi ni tajiri ni wale walio katika vyeo vya ulaji, ni kama kuwasanifu wananchi.
Utajiri wetu hatujaweza kuu-utilize kwa sababu ya uvivu na uzembe wetu wenyewe. Hakuna wa kumyooshea mwingine kidole kwani viongozi wetu ni reflection yetu wenyewe. Na hii ni kwa watu weusi wote. Bila kukiri hili na kujisahihisha hatujaenda popote. Watu weusi hatuna weledi wa kutumia utajiri luluki tuliojawaliwa na Mungu. Tangu miaka ya sitini kuna nchi viongozi wamekuwa wanapinduana ili ''kurekebisha makosa'' ya wenzao lakini haikusaida. Na vyama vingi vilipoingia kuna waliobadilisha na kuchagua vyama vingine lakini ikawa bure.
 
Weweeeee. Mimi nilisoma shule ya kata? Weweeee. Acha kabisa! Elimu yangu ya sekondari tu nina uhakika wewe hata ufike chuo kikuu, uchukuwe degree ya masters, hutafikia uelewa wangu niliokuwa nao nilipomaliza form six. Ungekuwa una uelewa mdogo tu usingeshindwa kuelewa rais anamaanisha nini na siyo matango pori. Ona swali la mtihani hili... nililijibu vizuri na kupata A kwenye somo husika, tena form four. ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''!
Hahahah wewe jamaa, ''a country may be poor although is reach'' ungekuwa na akili ungejua hili swali halimake any sense. Hiyo ni elimu wanayopewa watoto wa Tanzania na ccm,badala ya kufundishwa critical thinking and creativity ninyi mnakaririshwa kwamba nchi yenu ni tajiri kisa ina madini mito,misitu etc. Jiulize wangapi wanashinda njaa hapa mjini na baba zao wamewachie maeka na maeka huko vijijini
 
Weweeeee. Mimi nilisoma shule ya kata? Weweeee. Acha kabisa! Elimu yangu ya sekondari tu nina uhakika wewe hata ufike chuo kikuu, uchukuwe degree ya masters, hutafikia uelewa wangu niliokuwa nao nilipomaliza form six. Ungekuwa una uelewa mdogo tu usingeshindwa kuelewa rais anamaanisha nini na siyo matango pori. Ona swali la mtihani hili... nililijibu vizuri na kupata A kwenye somo husika, tena form four. ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''!

Mkuu hiyo elimu yako ulienda kukariri na kujuana na wanafunzi wengine, hii ni post ya nne, ila mistari ya mwisho na maneno ni hayo hayo, huoni hiyo elimu ina shida?
 
Hahahah wewe jamaa, ''a country may be poor although is reach'' ungekuwa na akili ungejua hili swali halimake any sense. Hiyo ni elimu wanayopewa watoto wa Tanzania na ccm,badala ya kufundishwa critical thinking and creativity ninyi mnakaririshwa kwamba nchi yenu ni tajiri kisa ina madini mito,misitu etc. Jiulize wangapi wanashinda njaa hapa mjini na baba zao wamewachie maeka na maeka huko vijijini
You are single minded to understand anything. Mimi sikusoma shule za kukariri kama wewe nakuelewesha tena. Kusema nchi yetu haina utajiri wa maliasili ndiyo ukariri lakini mwenye kuwaza kwa mapana anaona tofauti!
 
Ndo maana nikasema sometimes unaweza kudhani tunalaana,nyerere amekuwa rais wa Tanzania for 23 good years kama sijakosea, sasa mtu asiyepapenda akiwatawala for 23 good years huku wajomba zenu,wadogo zenu,kaka zenu,dada zenu na watoto wenu wakimlinda ili awanyanyase for 23 good years sasa kama hiyo si laana ni nini?Kuhusu magufuli kuwapenda watanzania hilo una uhakika nalo kweli? Hivi matatizo ya nchi hii yana muhusu magufuli pekee yake? kama hayamhusu pekee yake kwa nini anawazuia wasisema mambo yanayoihusi nchi yao? na je hivi vyama vya upinzani yeye kwa akili yake plus PhD aliyonayo anaona viongozi,wanachama na wananchi qaliovichagua ni wakenya?Kwangu mimi magufuli ni rais wa hovyo kuwa kutokea kwenye nchi yetu
Ndo maana nikasema sometimes unaweza kudhani tunalaana,nyerere amekuwa rais wa Tanzania for 23 good years kama sijakosea, sasa mtu asiyepapenda akiwatawala for 23 good years huku wajomba zenu,wadogo zenu,kaka zenu,dada zenu na watoto wenu wakimlinda ili awanyanyase for 23 good years sasa kama hiyo si laana ni nini?
Tuseme hivi, hizo zilikuwa ni nyakati nyingine ambazo nyie vijana wa siku hizi itakuwa vigumu kuzielewa nyakati hizo, kwani mnayapata mengi kupitia stories ambazo mnazisoma au kupewa na wazazi wenu.

Mimi binafsi sikumwona Nyerere kama ni mbaya au ana iendesha nchi vibaya, nilikuwa bado mdogo na sijakomaa kimawazo kiasi kwamba nikaweza kutambua mabaya yake na mazuri yake wakati ule. Kama nina mcriticise Nyerere hivi sasa ni kwa sababu ya kulinganisha utawala wake wakati ule na utawala wa sasa na vitu ambayo tumevishuhudia wakati ule na sasa.
Generally hata mimi wakati ule ungeniuliza nani namwona bora kati yake na baba yangu, jibu lake lingekuwa Nyerere.

Rais Myerere kama binadam alikuwa na karisma ambayo watu walivutiwa nayo. Sio sisi tu waafrika bali hata wazungu walivutiwa naye, kama nyie leo Diamond Platinumz anavyo wavutia.

Haita kuwa busara kwako kuwapa lawama wazazi, wajomba, shangazi na makaka na madada wa wakati ule kwa kumsujudu Nyerere na kumlinda. Hai make any sense! Kwa vile hukuwepo wakati ule, yachukue matendo yao kama history. Usijiachie sana katika maswala haya yaliyo pita ambayo huna affinity nayo kubwa, kiasi kwamba yaka ku affect kwenye carrier yako ya maisha.

Kwa wale walio yashuhudia ya wakati ule, wengi wao walikuwa happy na sustfied na maisha yale. Haikuwa shida kwao kupenda na kumlinda Rais wao, hata kama angetawala mile mile. Kwao ilikuwa sawa.
Hii demokrasia mnayo ijua nyie hivi sasa wakati ule watu hawakuijua. Toka asubuhi mpaka usiku unaenda kulala unasikia Propaganda za CCM na Nyerere tu na communists Parties na kila kitu kinacho husu ujamaa na socialism.

Hatukuwa na Smart phones na TV Stations kama nyie wakati huu. Kwa mimi nanfamilia yangu matatizo tulianza kuya feel baada ya kuwa tume husika kwenye pigo la kuvunjika kwa EAC 1977. Kwa watanzania wengi walianza ku experience shida baada ya vita vya Kagera. Hiyo ni Story nyingine ambayo sita weza kuimaliza leo.

Cha kuzingatia ni kwamba Nyerere hakuwa tu Rais bali ni Popstar, Iconic na role model wa kila mtanzania aliye kuwa teenager wakati ule.
Kuhusu magufuli kuwapenda watanzania hilo una uhakika nalo kweli?
Oo yaa! Magufuli ni Rais wa wanyonge na yuko tayari ku sacrifice maisha yake kuwatetea wanyonge. Hiyo ni undeniable!

Hivi matatizo ya nchi hii yana muhusu magufuli pekee yake? kama hayamhusu pekee yake kwa nini anawazuia wasisema mambo yanayoihusi nchi yao? na je hivi vyama vya upinzani yeye kwa akili yake plus PhD aliyonayo anaona viongozi,wanachama na wananchi qaliovichagua ni wakenya?Kwangu mimi magufuli ni rais wa hovyo kuwa kutokea kwenye nchi yetu
Sorry! Siko kumzungumzia sana yeye kuhusu tabia zake. Siasa zake. I am not concerned abouti his politics. Mimi binafsi kwa ujumla nawaona yuko Ok. My big concern is about our economy and the prosperity of our future generations.

Hafanyi kazi mbaya, by the way, ila aongeze kasi ili atuvushe haraka na wanachi waipate faida ya kuwa na rasilimali nyingi.

Kama ulivyo sema nakubaliana na wewe sisi kweli tutakuwa tumelaaniwa au kulogwa, maana hata kujenga toiletts za shule tuna hitaji wawekezaji? Duuh! Huyo kali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Weweeeee. Mimi nilisoma shule ya kata? Weweeee. Acha kabisa! Elimu yangu ya sekondari tu nina uhakika wewe hata ufike chuo kikuu, uchukuwe degree ya masters, hutafikia uelewa wangu niliokuwa nao nilipomaliza form six. Ungekuwa una uelewa mdogo tu usingeshindwa kuelewa rais anamaanisha nini na siyo matango pori. Ona swali la mtihani hili... nililijibu vizuri na kupata A kwenye somo husika, tena form four. ''A country may be poor athough is reach. Discuss with vivid examples from our country''!

Ukitaka kujua ww na mwalimu wako mlikuwa mnapotezeana muda, yeye anakuuliza hilo swali kisha anakupa ww A, lakini yeye mpaka leo ni masikini! Kwanini asitumie huo uelewa wake kujikomboa na umasikini zaidi ya kuishia kutemea Chaki mate ili iandike vizuri ubaoni? Tena ilitakiwa ww na huyo mwalimu wako mkamatwe kwa kosa la kuhujumu hewa safi hapo shuleni.
 
Hahahah wewe jamaa, ''a country may be poor although is reach'' ungekuwa na akili ungejua hili swali halimake any sense. Hiyo ni elimu wanayopewa watoto wa Tanzania na ccm,badala ya kufundishwa critical thinking and creativity ninyi mnakaririshwa kwamba nchi yenu ni tajiri kisa ina madini mito,misitu etc. Jiulize wangapi wanashinda njaa hapa mjini na baba zao wamewachie maeka na maeka huko vijijini

Ni kweli kabisa, kuna mjinga mwingine siku moja anasema ukimiliki ardhi ww ni tajiri, nikamwambia mbona masikini wengi ni wale wanaokaa vijijini ambao wote wanamiliki ardhi? Halafu ukija hapa mjini kuna muhindi hajawahi kumiliki hata ndoo ya kuoteshea maua lakini anaendesha duka la kubet na ana maisha ya hali ya juu.

Hili nchi bana, unashangaa kuna kiongozi anapiga kelele na kuishia kutemea watu mate, lakini huko kwao walikuwa wanamiliki ardhi na bado walikuwa masikini. Ila kapata madaraka kageuka tajiri, anasema hii nchi ni tajiri kwakuwa ina ardhi nzuri! Kichekesho muambie atoke madarakani akiitumie hiyo ardhi anayosema inaleta utajiri, hakubaliani na yuko tayari kuharibu uchaguzi na hata kuleta mauji ili aendelee kukaa madarakani!
 
Back
Top Bottom