Rais Magufuli: Kama balozi atakaa miezi sita bila kuleta ripoti ya alichokifanya ntamtumbua

Hizi lugha zina ukakasi kwelikweli, bora angekuwa anatengua anamwambia mwenyewe inatosha. Naiona kama haiku sawa hii.
hiyo ndio baabkubwa kusudi iwe fundisho kwa viongozi wengne legelege...mambo ya kubebana yamepitwa na wakati!.
Kiongozi anatakiwa ajue kabisa akiwa mzembe siku anatumbuliwa inakuwa aibu hadi ukweni kudadeki.
 
Awatumbue tu maana hawana jipya na angeanza na Dr wa mihogo
Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli atamuapisha Dkt. Damas Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu Jijini DSM leo tarehe 29 Sept, 2018 kuanzia saa 4:15 asubuhi hii.

Tazama TBC1 na tovuti rasmi ya Ikulu

UPDATES;

Rais Dk John Pombe Magufuli, amemuapisha Dk Damas Ndumbaro, kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.
View attachment 881377
Dk Ndumbaro anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Susan Kolimba ambaye uteuzi wake ulitengukiwa.

Baada ya kuapisha, rais Magufuli katoa neno.

"Nilitaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Prof Adolf Mkenda na yeye nimuondoe kabisa, lakini anabahati kukawa na nafasi iliyowazi Wizara ya Maliasili na Utalii nikampeleka huko. Naamini atakuwa amejifunza na atafanya kazi nzuri."

"Mabalozi sasa watakuwa wanaleta ripoti, kwamba kwa kipindi nilichoteuliwa nimeifanyia Tanzania A, B, C. Kama mtu miezi sita atakuwa hajafanya chochote, ameenda tu kunywa wine, ajiandae kurudi.

"Siku hizi sipendi kutumbua, na hata sipendi kulisikia hilo neno, lakini utafanyaje? Unamteua mtu unaona hafanyi kitu, wengine wanahangaika yeye yupo tu. Ndio maana niliamua kumtoa Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje."

"Lengo letu ni kuipeleka Nchi mbele, Wapo watendaji wengine wazuri pale Foreign lakini barua hazijibiwi, Balozi wa China aliwahi kuandika barua 24 zilijibiwa 2 Tu"

"Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki aliwahi kuandika barua 24 kwenda Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania, lakini zilijibiwa 2 tu. Kuna mambo mengi ya hovyo yanayofanyika katika Wizara ya Mambo ya Nje."-

=====
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 29 Septemba, 2018 amemuapisha Dkt. Damas Daniel Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Hafla ya kuapishwa kwa Dkt. Ndumbaro imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai na viongozi mbalimbali.

Akizungumza baada ya kuapishwa, Dkt. Ndumbaro amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumteua kushika wadhifa huo na ameahidi kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa hasa kwa kuzingatia mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano inayosisitiza kulinda heshima ya Tanzania kwa mataifa mbalimbali duniani, na kuitekeleza vizuri zaidi diplomasia ya uchumi.

Pamoja na kumpongeza, Mhe. Rais Magufuli amemtaka Dkt. Ndumbaro kuhakikisha dosari za utendaji usioridhisha katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zinarekebishwa ikiwemo kuwaondoa watendaji ambao wameonekana kuwa kikwazo cha ufanisi wa wizara hiyo.

“Nataka ukafanye kazi, nimesema mara nyingi na hapa nataka kurudia, wizara hii ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki hainifurahishi, nataka ukaisimamie vizuri, ukiona kuna mkurugenzi hafai mtoe” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amemtaka Dkt. Ndumbaro kuhakikisha Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali wanafanya kazi kwa manufaa ya Tanzania na wanatoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yao ili kujua kila Balozi kafanya nini, na kama anastahili kuendelea kuiwakilisha Tanzania katika nchi husika.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amesema amefanya mabadiliko ya Naibu Waziri na Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kutokana na kutoridhishwa kwake na mwenendo wa wizara hiyo na hivyo amemtaka aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Adolf Mkenda ambaye amehamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha wizara hiyo inaongeza mapato yatokanayo na maliasili zilizopo na vivutio vingi vya utalii vilivyopo hapa nchini.

“Prof. Mkenda uzuri ni kwamba wewe ni mchumi mzuri, natarajia kule Maliasili na Utalii utafanya mabadiliko yatakayoisaidia nchi kupata mapato zaidi, asilimia 32.5 ya nchi yetu ni maeneo ya hifadhi, na nchi yetu ni ya pili kwa vivutio vingi vya utalii duniani, mwaka huu tutaongeza hifadhi nyingine 5, kwa hiyo kahakikishe tunapata mapato zaidi” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli ameagana na Balozi wa Misri hapa nchini Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf ambaye amemaliza kipindi chake cha miaka 3.

Akizungumza baada ya kuagana Mhe. Elshawaf amesema uhusiano na ushirikiano wa Tanzania na Misri ni imara, na ameshukuru kwa ushirikiano mzuri alioupata kutoka Serikalini katika kipindi chote alichoiwakilisha nchi hiyo.

Mhe. Elshawaf amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa uongozi mzuri na ameahidi kufisha salamu za Mhe. Rais Magufuli kwa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah el-Sisi.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

29 Septemba, 2018

 
Inawezekana na madc kawapa hayo masharti ndiyo maana wanalazimishaga kuwaweka watu ndani masaa 48 ili wapate cha kusema kwa mteule wao
Mabalozi sasa watakuwa wanaleta ripoti, kwamba kwa kipindi nilichoteuliwa nimeifanyia Tanzania A, B, C. Kama mtu miezi sita atakuwa hajafanya chochote, ameenda tu kunywa wine, ajiandae kurudi.

"Siku hizi sipendi kutumbua, na hata sipendi kulisikia hilo neno, lakini utafanyaje? Unamteua mtu unaona hafanyi kitu, wengine wanahangaika yeye yupo tu. Ndio maana niliamua kumtoa Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje."
 
Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli atamuapisha Dkt. Damas Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu Jijini DSM leo tarehe 29 Sept, 2018 kuanzia saa 4:15 asubuhi hii.

Tazama TBC1 na tovuti rasmi ya Ikulu

UPDATES;

Rais Dk John Pombe Magufuli, amemuapisha Dk Damas Ndumbaro, kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.
View attachment 881377
Dk Ndumbaro anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Susan Kolimba ambaye uteuzi wake ulitengukiwa.

Baada ya kuapisha, rais Magufuli katoa neno.

"Nilitaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Prof Adolf Mkenda na yeye nimuondoe kabisa, lakini anabahati kukawa na nafasi iliyowazi Wizara ya Maliasili na Utalii nikampeleka huko. Naamini atakuwa amejifunza na atafanya kazi nzuri."

"Mabalozi sasa watakuwa wanaleta ripoti, kwamba kwa kipindi nilichoteuliwa nimeifanyia Tanzania A, B, C. Kama mtu miezi sita atakuwa hajafanya chochote, ameenda tu kunywa wine, ajiandae kurudi.

"Siku hizi sipendi kutumbua, na hata sipendi kulisikia hilo neno, lakini utafanyaje? Unamteua mtu unaona hafanyi kitu, wengine wanahangaika yeye yupo tu. Ndio maana niliamua kumtoa Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje."

"Lengo letu ni kuipeleka Nchi mbele, Wapo watendaji wengine wazuri pale Foreign lakini barua hazijibiwi, Balozi wa China aliwahi kuandika barua 24 zilijibiwa 2 Tu"

"Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki aliwahi kuandika barua 24 kwenda Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania, lakini zilijibiwa 2 tu. Kuna mambo mengi ya hovyo yanayofanyika katika Wizara ya Mambo ya Nje."-

=====
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 29 Septemba, 2018 amemuapisha Dkt. Damas Daniel Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Hafla ya kuapishwa kwa Dkt. Ndumbaro imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai na viongozi mbalimbali.

Akizungumza baada ya kuapishwa, Dkt. Ndumbaro amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumteua kushika wadhifa huo na ameahidi kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa hasa kwa kuzingatia mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano inayosisitiza kulinda heshima ya Tanzania kwa mataifa mbalimbali duniani, na kuitekeleza vizuri zaidi diplomasia ya uchumi.

Pamoja na kumpongeza, Mhe. Rais Magufuli amemtaka Dkt. Ndumbaro kuhakikisha dosari za utendaji usioridhisha katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zinarekebishwa ikiwemo kuwaondoa watendaji ambao wameonekana kuwa kikwazo cha ufanisi wa wizara hiyo.

“Nataka ukafanye kazi, nimesema mara nyingi na hapa nataka kurudia, wizara hii ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki hainifurahishi, nataka ukaisimamie vizuri, ukiona kuna mkurugenzi hafai mtoe” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amemtaka Dkt. Ndumbaro kuhakikisha Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali wanafanya kazi kwa manufaa ya Tanzania na wanatoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yao ili kujua kila Balozi kafanya nini, na kama anastahili kuendelea kuiwakilisha Tanzania katika nchi husika.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amesema amefanya mabadiliko ya Naibu Waziri na Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kutokana na kutoridhishwa kwake na mwenendo wa wizara hiyo na hivyo amemtaka aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Adolf Mkenda ambaye amehamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha wizara hiyo inaongeza mapato yatokanayo na maliasili zilizopo na vivutio vingi vya utalii vilivyopo hapa nchini.

“Prof. Mkenda uzuri ni kwamba wewe ni mchumi mzuri, natarajia kule Maliasili na Utalii utafanya mabadiliko yatakayoisaidia nchi kupata mapato zaidi, asilimia 32.5 ya nchi yetu ni maeneo ya hifadhi, na nchi yetu ni ya pili kwa vivutio vingi vya utalii duniani, mwaka huu tutaongeza hifadhi nyingine 5, kwa hiyo kahakikishe tunapata mapato zaidi” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli ameagana na Balozi wa Misri hapa nchini Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf ambaye amemaliza kipindi chake cha miaka 3.

Akizungumza baada ya kuagana Mhe. Elshawaf amesema uhusiano na ushirikiano wa Tanzania na Misri ni imara, na ameshukuru kwa ushirikiano mzuri alioupata kutoka Serikalini katika kipindi chote alichoiwakilisha nchi hiyo.

Mhe. Elshawaf amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa uongozi mzuri na ameahidi kufisha salamu za Mhe. Rais Magufuli kwa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah el-Sisi.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

29 Septemba, 2018


TZ ndio nchi pekee ambayo watu wake wanatamani madaraka kwa ajili ya kula bata au kuweka title ya wadhifa na sii kulitumikia taifa na wananchi au kutimiza majukumu ya nyadhifa zao. KONGOLE za dhati kwa harakati za Raisi wetu ktk hili Dr. JPM
 
Inaonekana mambo ya nje kuna networks nyingi za wajanja wapigaji. Mindset ni kama bado haijabadilika.
Na hii hutoakana na fikra kuwa TZ bado ni taifa changa hivyo maeneo km hayo huwa hata viongoz wengi hawayafuatilii utendaji wake na pia ilizoeleka kuwa ni mopja ya sekta ambayo nafasi zilikuwa zikitolewa km shukran kwa wahusika waliozipata nafasi hizo. Wakati ni moja ya maeneo mazuri sana ya kuwezesha utangazwaji mzuri wa TZ ktk kila nyanja + fursa zilizopo
 
Na hii hutoakana na fikra kuwa TZ bado ni taifa changa hivyo maeneo km hayo huwa hata viongoz wengi hawayafuatilii utendaji wake na pia ilizoeleka kuwa ni mopja ya sekta ambayo nafasi zilikuwa zikitolewa km shukran kwa wahusika waliozipata nafasi hizo. Wakati ni moja ya maeneo mazuri sana ya kuwezesha utangazwaji mzuri wa TZ ktk kila nyanja + fursa zilizopo
Hapo ndipo wakenya wanapotuzidi, kuelewa ni sekta ipi ipewe kipaumbele na kwa wakati gani.

Walifikia hatua ya kuiambia dunia kwamba mlima kilimanjaro upo kwao, na wakati huo sisi tulikuwa tumelala tu.
 
Hapo ndipo wakenya wanapotuzidi, kuelewa ni sekta ipi ipewe kipaumbele na kwa wakati gani.

Walifikia hatua ya kuiambia dunia kwamba mlima kilimanjaro upo kwao, na wakati huo sisi tulikuwa tumelala tu.
Mwaka 2011 ktk maadhimisho ya siku ya kuzaliwa malkia wa Uingereza, wakenya walisemekana kuwa ndio wenye Lugha ya kiswahili na walitakiwa kutoa speech ktk lugha ya kiswahili. Ukweli ni kwamba wao hawapo vizuri hivyo walimkodi mtanzania MRISHO MPOTO ili akatoe speech ile mbele ya malkia naye akafanya hivyo, sasa km serikali ya awamu ile haikulipigia kelele hilo ingewezaje kupigia kelele suala la mlima Kilimanjaro kuwa ni wa Kenya?

Ila kwa kipindi hiki tarajia kuona watu wakiwajibika ipasavyo, na masuala km hayo ya mlima Kilimanjaro pamoja na Kiswahili hayawez tokea tena.
 
MRISHO MPOTO ili akatoe speech ile mbele ya malkia naye akafanya hivyo,
MPOTO aliihujumu Jamhuri ya Muungano Tanzania kitamaduni, kidesturi,kisiasa na kidiplomasia kama kweli tukio hili lilitokea na yeye alijua kabisa kuwa amekodiwa kwa malengo hayo ya wakenya na UK. Kwa kitendo hicho, Mpoto anatakiwa kuomba radhi Jamhuri ya Muungano Tanzania kabla rungu halijamshukia. Ule ulikuwa utovu wa uzalendo wa hali ya juu kabisa.
 
MPOTO aliihujumu Jamhuri ya Muungano Tanzania kitamaduni, kidesturi,kisiasa na kidiplomasia kama kweli tukio hili lilitokea na yeye alijua kabisa kuwa amekodiwa kwa malengo hayo ya wakenya na UK. Kwa kitendo hicho, Mpoto anatakiwa kuomba radhi Jamhuri ya Muungano Tanzania kabla rungu halijamshukia. Ule ulikuwa utovu wa uzalendo wa hali ya juu kabisa.
Baada ya tukio lile alihojiwa na yeye mwenyewe alitupa lawama kwa viongoz wa taifa,
 
Asante sana mkuu kwa taarifa. Hata hivyo naomba link ya mahojiano hayo ya MPOTO akielekeza lawama kwa taifa. Natanguliza shukrani.
Aisee, utanisamehe kwa suala la link, ila ilikuwa TBC1 ktk kipindi chao cha asubuhi ambacho huruka mida ya saa 12 hivi. Ilikuwa mwaka 2011 nami nilicheki kipindi live
 

Similar Discussions

12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom