Brigedia Chan-ocha
JF-Expert Member
- Mar 7, 2014
- 1,353
- 2,842
Rais wa Uturuki Bwana Tayip Edorgan aliomba mitandao ya kijamii nchini mwake ifungwe kabisa kwa sababu ilikuwa inaichafua serikali yake na yeye mwenyewe, Baada ya Muda mfupi, Jeshi lilifanya jaribio la mapinduzi, akiwa kwenye mapumziko kwenye mji mwingine hapo hapo UTURUKI, Muda mfupi baada ya kujulishwa kuwa Kikosi cha Jeshi kinataka kumpindua, Rais huyo haraka sana, aliondoka ndani ya Hotel aliyokuwemo, lakini wakati huo huo, akaukumbuka mtandao wa kijamii wa Whatsapp na Tweeter, Rais alijirecord akizungumza kwa sauti, akiwasihi wafuasi na wananchi wote kwa ujumla kujitokeza kwa wingi mitaani kupinga jaribio hilo la kijeshi, Rais Edorgan aliutuma ujumbe huo na mara moja ukaanza kusambaa kwa kasi ya ajabu kwa wananchi, wananchi wa UTURUKI walipoona na kusikia sauti yake, walianza kumiminika mitaani wakiwapinga wanajeshi walioongoza mapinduzi hayo huku wanajeshi wengine wakipigwa na Raia waliojitokeza mitaani.
Hivyo, Rais Magufuli, tukio la uturuki linaweza kutoa somo Fulani kwako, ingawa si kwa dhana hiyo hiyo ya mapinduzi ya kijeshi la hasha, kunaweza kutokea tukio lolote ambalo serikali ingependa wananchi wote kwa haraka sana wapate taarifa au serikali yako inaweza kuwa na jambo Fulani ambalo ungependa upate mwitikio wa wananchi, hivyo, si busara sana kuanza kupambana na vyombo vya habari au mitandao ya kijamii, maana nyote mnahitajiana, Wewe unauhitaji mtandao wa Jamii forums na mtandao wa Jamii forums unakuhitaji, Mh, Rais kabla hujawa Rais mtandao huu ulikuwepo, na wenzio wote waliuacha, sasa kwa nini wewe tu ndo uumie?
Serikali ina siri gani ambayo hamtaki iandikwe humu? hivi kama kuna Jaribio la mapinduzi ya kijeshi limepangwa dhidi yako, na mtandao huu ukaliibua, hivyo kuzimwa haraka, huwezi kushukuru huu mtandao? au kama Tanzania imevamiwa unataka tusihabarishwe? au kama kuna wizi umetokea sehemu Fulani na ukaandikwa humu ina maana napo ni dhambi?
Tafakari sana Mh. Rais, tulianza kuwa na Imani na wewe, ila kwa jinsi unavyoenda, inatia shaka sana, kibaya Zaidi, huu ni mwaka wa kwanza tu toka umeingia madarakani, tunajiuliza, je ikifika miaka 5 hali itakuwaje?
Hivyo, Rais Magufuli, tukio la uturuki linaweza kutoa somo Fulani kwako, ingawa si kwa dhana hiyo hiyo ya mapinduzi ya kijeshi la hasha, kunaweza kutokea tukio lolote ambalo serikali ingependa wananchi wote kwa haraka sana wapate taarifa au serikali yako inaweza kuwa na jambo Fulani ambalo ungependa upate mwitikio wa wananchi, hivyo, si busara sana kuanza kupambana na vyombo vya habari au mitandao ya kijamii, maana nyote mnahitajiana, Wewe unauhitaji mtandao wa Jamii forums na mtandao wa Jamii forums unakuhitaji, Mh, Rais kabla hujawa Rais mtandao huu ulikuwepo, na wenzio wote waliuacha, sasa kwa nini wewe tu ndo uumie?
Serikali ina siri gani ambayo hamtaki iandikwe humu? hivi kama kuna Jaribio la mapinduzi ya kijeshi limepangwa dhidi yako, na mtandao huu ukaliibua, hivyo kuzimwa haraka, huwezi kushukuru huu mtandao? au kama Tanzania imevamiwa unataka tusihabarishwe? au kama kuna wizi umetokea sehemu Fulani na ukaandikwa humu ina maana napo ni dhambi?
Tafakari sana Mh. Rais, tulianza kuwa na Imani na wewe, ila kwa jinsi unavyoenda, inatia shaka sana, kibaya Zaidi, huu ni mwaka wa kwanza tu toka umeingia madarakani, tunajiuliza, je ikifika miaka 5 hali itakuwaje?