Rais, Magufuli ingilia kati vita dhidi ya dawa za kulevya

Mchange

Senior Member
Jul 21, 2009
158
325
VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA.
----------------------------------------------------------
Kwako Rais John Pombe Magufuli,

Waziri Wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba na Viongozi wengine waandamizi wa serikali.

Watumiaji wakuu wa Dawa za kulevya za aina zote hapa nchini ni watanzania.

Wawe vijana, watu wazima wa makamo ama wazee kabisa lakini ni Watanzania.

Leo kelele zimeongezeka kwa sababu watanzania wenzetu hasa wanaotuburudisha katika Sanaa kama Chid Benz na wengine kuonekana unga umewasonga.

Nimemwona Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba ameenda Nyumbani kwa Mama yake Mzazi Chid Benz. Pengine ameenda kumpa pole ama tu kumsabahi,

Nimeona pia waziri huyo ameshika tuzo za msanii huyo ambaye kwa sasa hakika amepotea.

Utafiti wangu mdogo unaonyesha kwamba hivi sasa Unga (Madawa ya Kulevya ) unauzwa kwa wingi kuliko kipindi kingine chochote hapa nchini, wauzaji wanauuza hadharani na wanunuzi pia wananunua na wanatumia hadharani.

Polisi wetu baadhi ya maeneo wamekuwa wakibishania malipo na wauzaji ili wadiwakamate.

Hili tatizo sio Dogo.

Tatizo la Dawa za Kulevya haliwezi komeshwa kwa watanzania kuendelea kulalamika bila kuchukua hatua.

Wala tatizo hili haliwezi kumalizika kwa waziri kusema kuwa :serikali ipo serious inapambana na unga na itawakamata wauzaji na waache Mara moja".

Iko Hivi.

Wauzaji wote wanaishi mitaani hapa nchini.

Wanunuzi na Watumiaji wote wanaishi mitaani hapa hapa nchini.

Wasio kuwa watumiaji nasi tunaishi humu humu mitaani.

Mitaa yote Na vijiji vyake vina wenyeviti wa Mitaa.

Mitaa yote na vijiji vyake vina wajumbe wa serikali za Mitaa na wajumbe wa nyumba kumi kumi wa CCM, CHADEMA, ACT na vyama vinginevyo.

Kwa kifupi ni kwamba wauzaji na wanunuzi pamoja na wasiotumia wote wanajuana.

Watumiaji wanaishi huku mitaani.

Rais, anzisha Ambush. Mwenyekiti wa Mtaa ambaye mtaani Kwake kutakutwa Mateja waathirika wa unga, yeye na wajumbe wake wakamatwe na wafunguliwe mashtaka ya uhujumu uchumi.

Mwenyekiti wa Mtaa ambaye mtaani Kwake anaviona na kuvijua vijiwe vya kuuzia unga, bange na Dawa nyingine, wakamatwe na wafungwe kwa makosa ya kuhujumu uchumi.

Rais, wakamate wenyeviti wa Mitaa wote ambao wananchi wao wanawajua wauzaji wa unga na hawaripotiwi.

Wafukuze kazi askari wote wanaohongwa ili kuendelea kuacha wauzaji waendelee kuuza unga.

Huu unga hauuzwi hewani. Wanaouza tunaishi nao na wananunua kadharika.

Serikali iache sasa kulalamika. Ichukue hatua.

Hatua ni Viongozi wawakilishi wa chini huku mitaani kuwajibika.

Habib Mchange
Mwananchi
 
Acha wanaotumia madawa wapungue humu duniani maana bajeti ya Tanzania ni ndogo kuhudumia watu mili 50
 
Unga ni vigumu kuzuilika cha msingi ni kuomba Mungu.
Mtandao ni mkubwa na hatari.
Ata raisi mwenyewe hawezi sababu kubwaa watu wanaotakiwa kumpa taarifa wamewekwa kiganjani.
 
Yaani upeo wako ni mkubwa au mdogo kiasi gani.,?

Jana uliangalia malumbano ya hoja ITV pale kulikuwa hadi kuna watu waliotumia na walio athirika tayari. Ila wanadai kuwa ishu ya madawa sio ishu ndogo Kama unavyoandika huu uzi hapa.

Wanadai kuwa madawa ya kulevya wanao Fanya biashara hiyo ya kuingiza na kutoa ni watu Wazito na wengine ni vigogo madarakani., unaposema umtaje mtu anaeuza au anaesambaza ulinzi wako upo wapi, kuna kupotezwa .,

Au RAISI JPM aamuwe kukamata watu ambao wanatumia au viongozi WA vitongoji vyao ni sawa na uonevu mkubwa uliokithiri.. Kinachotakiwa ni kuhakikisha mipaka yetu ya ulinzi iwe imara katika hili iwe Airport Bandari Border Na kila kitu.

Ukishamaliza hilo uone Kama kutakuwa Na Dawa Za kulevya nchini. Hizo nyingine ni Propaganda kinyume Na hapo Tumpigie Gita Mbuzi akate mauno Kwa mana hata USA bado Mbuzi Wao anaserebuka tu. Wao walishindwa ije kuwa sisi!
 
Vita ya madawa ya kulevya kiukweli haipo kwenye Nchi hii.

Wafanyabiashara wakubwa wa hii bidhaa serikali inawajua lakini sijui kwanini wanaufyata.

Le Mutuz... usijifanye unapigana kwenye hii vita ya madawa ya kulevya as most of your close colleagues are in this dirty and dangerous business.
Wadanganye wale followers wako wajinga kule Instagram.
 
Yaani upeo wako ni mkubwa au mdogo kiasi gani.,? Jana uliangalia malumbano ya hoja ITV pale kulikuwa hadi kuna watu waliotumia na walio athirika tayari. Ila wanadai kuwa ishu ya madawa sio ishu ndogo Kama unavyoandika huu uzi hapa. Wanadai kuwa madawa ya kulevya wanao Fanya biashara hiyo ya kuingiza na kutoa ni watu Wazito na wengine ni vigogo madarakani., unaposema umtaje mtu anaeuza au anaesambaza ulinzi wako upo wapi, kuna kupotezwa ., Au RAISI JPM aamuwe kukamata watu ambao wanatumia au viongozi WA vitongoji vyao ni sawa na uonevu mkubwa uliokithiri.. Kinachotakiwa ni kuhakikisha mipaka yetu ya ulinzi iwe imara katika hili iwe Airport Bandari Border Na kila kitu. Ukishamaliza hilo uone Kama kutakuwa Na Dawa Za kulevya nchini. Hizo nyingine ni Propaganda• kinyume Na hapo Tumpigie Gita Mbuzi akate mauno Kwa mana hata USA bado Mbuzi Wao anaserebuka tu. Wao walishindwa ije kuwa sisi!
KwaninI ukikutwa unavuta bangi unakamatwa na mteja hakamatwi?
 
Vita ya madawa ya kulevya kiukweli haipo kwenye Nchi hii.

Wafanyabiashara wakubwa wa hii bidhaa serikali inawajua lakini sijui kwanini wanaufyata.

Le Mutuz... usijifanye unapigana kwenye hii vita ya madawa ya kulevya as most of your close colleagues are in this dirty and dangerous business.
Wadanganye wale followers wako wajinga kule Instagram.
Jana le m~bebez..akili kubwa alitema point za kutosha kwenye kipima joto,pongezi kubwa kwake!
Kwakuwa kaamua nae kupambana na ni mtu wa siku nyingiiiii sanaa hapa town muache apambane na itakuwa njema km ataamua KUTUTAJIA MAJINA YA WAHUSIKA WAKUU!
 
VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA.
----------------------------------------------------------
Kwako Rais John Pombe Magufuli,

Waziri Wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba na Viongozi wengine waandamizi wa serikali.

Watumiaji wakuu wa Dawa za kulevya za aina zote hapa nchini ni watanzania.

Wawe vijana, watu wazima wa makamo ama wazee kabisa lakini ni Watanzania.

Leo kelele zimeongezeka kwa sababu watanzania wenzetu hasa wanaotuburudisha katika Sanaa kama Chid Benz na wengine kuonekana unga umewasonga.

Nimemwona Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba ameenda Nyumbani kwa Mama yake Mzazi Chid Benz. Pengine ameenda kumpa pole ama tu kumsabahi,

Nimeona pia waziri huyo ameshika tuzo za msanii huyo ambaye kwa sasa hakika amepotea.

Utafiti wangu mdogo unaonyesha kwamba hivi sasa Unga (Madawa ya Kulevya ) unauzwa kwa wingi kuliko kipindi kingine chochote hapa nchini, wauzaji wanauuza hadharani na wanunuzi pia wananunua na wanatumia hadharani.

Polisi wetu baadhi ya maeneo wamekuwa wakibishania malipo na wauzaji ili wadiwakamate.

Hili tatizo sio Dogo.

Tatizo la Dawa za Kulevya haliwezi komeshwa kwa watanzania kuendelea kulalamika bila kuchukua hatua.

Wala tatizo hili haliwezi kumalizika kwa waziri kusema kuwa :serikali ipo serious inapambana na unga na itawakamata wauzaji na waache Mara moja".

Iko Hivi.

Wauzaji wote wanaishi mitaani hapa nchini.

Wanunuzi na Watumiaji wote wanaishi mitaani hapa hapa nchini.

Wasio kuwa watumiaji nasi tunaishi humu humu mitaani.

Mitaa yote Na vijiji vyake vina wenyeviti wa Mitaa.

Mitaa yote na vijiji vyake vina wajumbe wa serikali za Mitaa na wajumbe wa nyumba kumi kumi wa CCM, CHADEMA, ACT na vyama vinginevyo.

Kwa kifupi ni kwamba wauzaji na wanunuzi pamoja na wasiotumia wote wanajuana.

Watumiaji wanaishi huku mitaani.

Rais, anzisha Ambush. Mwenyekiti wa Mtaa ambaye mtaani Kwake kutakutwa Mateja waathirika wa unga, yeye na wajumbe wake wakamatwe na wafunguliwe mashtaka ya uhujumu uchumi.

Mwenyekiti wa Mtaa ambaye mtaani Kwake anaviona na kuvijua vijiwe vya kuuzia unga, bange na Dawa nyingine, wakamatwe na wafungwe kwa makosa ya kuhujumu uchumi.

Rais, wakamate wenyeviti wa Mitaa wote ambao wananchi wao wanawajua wauzaji wa unga na hawaripotiwi.

Wafukuze kazi askari wote wanaohongwa ili kuendelea kuacha wauzaji waendelee kuuza unga.

Huu unga hauuzwi hewani. Wanaouza tunaishi nao na wananunua kadharika.

Serikali iache sasa kulalamika. Ichukue hatua.

Hatua ni Viongozi wawakilishi wa chini huku mitaani kuwajibika.

Habib Mchange
Mwananchi


Naunga mkono yote uliyosema isipokuwa kwa askari kufutwa kazi. Mimi nasema, kama kuna askari kabainika anakula rushwa ili asikamate wauza unga na wabugiaji basi anyongwe ili kuwa fundisho kwa wengine. Tukifanya hivi kwakweli tutafika mbali sana kwa kutokomeza hili jambo.
 
Nini kazi ya Mwigulu Nchemba??????? Mbona Kitwanga makeke yake yalionekana na wauza madawa walipwaya sana, ila kwa Mwigulu sioni akifanya lolote juu ya ujambazi na madawa, au labda mimi sijui tu?
 
Nini kazi ya Mwigulu Nchemba??????? Mbona Kitwanga makeke yake yalionekana na wauza madawa walipwaya sana, ila kwa Mwigulu sioni akifanya lolote juu ya ujambazi na madawa, au labda mimi sijui tu?
Kweli..
Mwigulu hayupo kabisa kwenye hii vita.
Kitwanga alipambana sana na hii issue.
 
Vijana wanaangamia sana, huku mtaani, hao wasanii mnaowaona huko ni sample ndogo sana ya waathirika.
 
Jana le m~bebez..akili kubwa alitema point za kutosha kwenye kipima joto,pongezi kubwa kwake!
Kwakuwa kaamua nae kupambana na ni mtu wa siku nyingiiiii sanaa hapa town muache apambane na itakuwa njema km ataamua KUTUTAJIA MAJINA YA WAHUSIKA WAKUU!

Le Mutuz jana at some points aliboa sana tu hasa alivyojaribu kupinga jitihada zinazofanywa na Mchungaji Ananja wa KKKT Kigogo katika kuwasaidia mateja kuondoka utejani.

Otherwise alijitahidi kidogo kujenga hoja ila alifeli kwa kiasi. Hata hivyo nampongeza kwa kwenda kwenye kipindi.
 
...Mtoa Rushwa na Mpokea Rushwa wote wanatenda Kosa.......iwe hivyo kisheria pia kwa Unga, .........Muuzaji Unga na Mnunuaji Unga wote wanatenda kosa... tuanzie hapo
 
Thumbs up le mutuz. Lakini wauzaji wengi wanajulikana na wengi in makada,watoto Wa viongozi,wabunge, wauza nguo na vipodozi maarufu,wasanii marafiki zetu masuper bilioneaazz unknow. Akili kubwaaaz na huwa wanatransform their cash into legit business. Mfano europe watu wengi wanao own night clubs, security guards firms,restaurants,casinos ni watu wa ngada. Na ngada huwa haijifichi kwa mtu anaye deal NATO maana INA create a certain attitude.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom