Rais Magufuli, Ikulu umeshaijua milango yote toka sasa

kipara kipya

JF-Expert Member
May 2, 2016
14,055
15,885
Amani kwenu wadau

Tangu rais wetu ma JMT alipokabidhiwa madaraka hajatoka kwenda safari ya umbali mrefu zaidi ya nchi jirani za ukanda wetu huu.

Ninalo muomba rais atoke aende nchi za nje kama mwenyewe alivyo jipambanua si muoga wala hana aibu ifikapo muda wa kuomba

Mara ya kwanza nilitegemea ile pin yako ya safari za nje na wewe mwenyewe inakubana lakini si hivyo na kama ilikuwa unataka kuijua milango yote ya ikulu tayari ushaifahamu ni miaka miwili na nusu fanya utoke,

Nenda kawaeleze wazungu uchumi wa tanzania umekuwa kwa 7%,nenda kawaeleze demokrasia inazidi kustawi,uhuru wa habari,uhuru wa kujieleza,vita ya ugaidi na madawa ya kulevya vyote umefanya vizuri waambie elimu bure,afya,maji,umeme,na kama ilivyo ada na miundo mbinu na umedhibiti vyema suala la rushwa na ufisadi na serikali yako ni ya kidemokrasia umeteua mpaka wapinzani na unasimamia vyema rasilimali za nchi kama ulivyo onyesha uzalendo kwenye mchanga wa madini

Na uwaombe waje wawekeze katika miradi mikubwa ya viwanda kama dhumuni la serikali yako lilivyo imetosha rais kuona wale viongozi wote wanaokuja hapa kwetu uwezo wa ni kama wetu hivyo hawaleti tija na hawana ushawishi

Ni hayo ndugu rais labda nichukue nafasi kukupongeza kumteua mama mghwira kuwa Rc mpya

Najua wewe ni msikivu na sio mbishi kufuata ushauri kama ulivofuata ushauri wa tume ya mashobo!

Akhsante!
 
Kama nawe ni mteuliwa kama Rc atakusikiliza lakini kama si hivyo tuililie tanzania yetu
 
Subr 2025 mpate rais shehe( Muslim) hao ndo huwa hawajambo kuombaomba na kupenda misàada na maisha mteremko
 
Back
Top Bottom