G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,873
Hivi jamani hata aibu watu hawaoni? Mbunge anapigwa risasi hadharani tena mchana kweupe na hakuna chochote kinachofanyika kutoka serikalini zaidi ya kuendelea kumuumiza!
Tunaenda kwenye ibada kufanya nini! Tena mbaya zaidi na baadhi ya viongozi wa dini wanafumbia macho ukiukwaji huu mkubwa wa haki ya mtu ya kuishi! Hapana labda kuna watu ambao hawajaumbwa kwa nyama na damu! Labda wapo wenye miili iliyoundwa kwa chuma!
Tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi hadharani na mwisho kuvuliwa ubunge limefehdehesha taifa na kuonekana kuwa sisi ni binadamu wenye roho za kikatili kuliko kawaida. Hilo linachangiwa kwa kiasi kikubwa na vyombo vya usalama kufumba macho.
Tunaenda kwenye ibada kufanya nini! Tena mbaya zaidi na baadhi ya viongozi wa dini wanafumbia macho ukiukwaji huu mkubwa wa haki ya mtu ya kuishi! Hapana labda kuna watu ambao hawajaumbwa kwa nyama na damu! Labda wapo wenye miili iliyoundwa kwa chuma!
Tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi hadharani na mwisho kuvuliwa ubunge limefehdehesha taifa na kuonekana kuwa sisi ni binadamu wenye roho za kikatili kuliko kawaida. Hilo linachangiwa kwa kiasi kikubwa na vyombo vya usalama kufumba macho.