Rais Magufuli: Hakuna lockdown Tanzania! Mwanangu amepona COVID-19 kwa kujifukiza (Mei 17, 2020)

Akihutubia Taifa(sina hakika kama ni sahihi kusema hivi) tokea Kanisa la KKKT Usharika wa Chato leo asubuhi, Rais Magufuli amelitangazia Taifa na ulimwengu kuwa mtoto wake ni miongoni mwa waliougua na kisha kupona Corona yumo mtoto wake hapo hajasema ni yupi.
Hii ni aina ya Kiki mbovu ambayo wanaompangia Rais (kama taasisi) kipi aseme na kipi asigusie wanaendelea kumpotosha. Anna Mgwira alipopata Corona alisema na kujitenga, amepona juzi akatutangazia na tumempa pole, lakini Leo ghafla mtu anajitokeza eti na kwangu kulikuwa na mgonjwa amepona Jana. Iwe kweli au uongo lakini kutuambia sasa hivi ni kutaka tuamini haogopi huu ugonjwa huku akiendelea kujificha kwao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Your argument is very weak
 
Kwa staili hii yule daktari naibu waziri lazima atofautiane na mteuzi wake!! Madaktari wamefundishwa umuhimu wa kuzuia MTU hata m1 asiugue,hatari ya virus I na pia kuwa na data sahihi sasa ukikutana na asiyejali anaweka maujanja ujanja kujipa ugangwe mob lazma mpishane
 
Hao wanasheria na mawakili walikuwa hawafi ila wameanza kufa kwa corona tu! It does not make any sense!

Sent using Jamii Forums mobile app
Haujui unalozungumza wewe njoo na takwimu mwaka jana walikufa watu wangapi kuanzia jan-may kisha fanya comparison ,numbers dont lie mkuu ,namba ikiwa tofauti lazima ndio unaweza kuconclude kwamba vifo vimeongezeka au vimepungua na kufanya more analysis ,naomba majibu kuanzia jan-may 2019 walikufa watu wangapi in general na mwaka huu jan -may wamekufa wangapi kisha tufanye analysis.
 
By Malisa GJ

1.Nampongeza Askofu Shoo kwa kuliongoza vizuri kanisa la KKKT na Askofu Keshomshahara wa Dayosisi hii kwa kazi kubwa anayoifanya. Mungu awabariki sana.

2. Wakati Corona inaingia niliwaomba watanzania waombe kwa siku tatu. Nawashukuru Wachungaji, Masheikh na Maaskofu kwa kuitikia wito na Mungu amejibu. Si vibaya tukatenga hata siku moja ya kumshukuru ktk sala zetu za wiki.

3. Mtoto wangu wa kumzaa aliugua corona. Akajifungia ndani akajifukiza, akanywa malimao akapona. Sasa hivi anapiga push-up hana tatizo lolote. Ugonjwa huu utasambaa lakini utaisha wenyewe, tusiwe na hofu.

4. Kuna mambo ya hovyo yalikuwa yanafanyika hospitalini. Kila anayefariki wanakimbilia kumpima corona. Mtu amefariki unampima ya nini? Nguvu za kumpima wanazo lakini za kumhudumia apone hawana.

5. Hali ya maambukizi imepungua sana. Amana ilikuwa na wagonjwa 198 wamebaki 12 tu. Mloganzila 30 wamebaki 6. Kibaha 50 wamebaki 22. Arusha kituo cha Moshono kina wagonjwa 11 vingine havina wagonjwa. Mwanza vituo 10 wagonjwa 6. Dodoma wagonjwa 42 wamebaki wawili tu.

6. Kama hali itaendelea hivi hadi wiki ijayo nimepanga kufungua vyuo ili wanafunzi wetu waendelee kusoma. Pia nimepanga kuruhusu michezo kwa sababu michezo ni sehemu ya burudani. Maisha lazima yaendelee.

7. Mtu akifariki kwa ugonjwa wowote azikwe kawaida. Hakuna sababu ya kumzika kwa dharura, Corona sio Ebola.

8. Hakuna cha lockdown wala baba yake lockdown wala mjomba yake lockdown. Watu waendelee kuchapa kazi.

9. Kuna uwezekano kutokea njaa baada ya corona, kwa sababu nchi nyingi zimefungia watu wake ndani hawazalishi. Kwahiyo tutumie vizuri mvua hizi ndogondogo kulima ili tuwe na akiba ya chakula. Wale waliojifungia siku wakifunguliwa tuwasaidie chakula.

10. Tuna ushirikiano mzuri na nchi za EAC na SADC ktk uchumi na mambo mengne. Lakini hili la corona nimeona kila nchi itumie njia zake. Sisi ni taifa huru hatuwezi kupangiwa cha kufanya. Hata mzee Kikwete alisema za kuambiwa changanya na zako. Wanaoona kujifungia ndani ni njia bora kwao wafanye. Na sisi tutumie njia zetu tunazoona zinafaa, ili mradi kila mmoja anapambana na Corona ktk mazingira yake.
 
Siyo kweli, hizo ni hospitali na kuna saa za kuona wagonjwa!! We jiandae tu na PPE yako ukaangalie wagonjwa. Uwapelekee na matunda nk
Sawa nyie teteeni uovu ila tunachoshukuru kwamba huu ugonjwa ni noma unatwanga kwa wale wale wapiga mapambio wa MEKO.
 
*CROSS-EXAMINATION*

(1) *Wakili:* Unakubaliana na mimi kuwa tuna maabara moja tu ya kupima virus vya Korona hapa Tanzania.

🔹 *Mheshimiwa* Ndio

(2) *Wakili:* Na unakubaliana na mimi kuwa mahabara hiyo ipo kwenye uchunguzi na hivyo haiwezi fanya kazi kwa Sasa

🔹 *Mheshimiwa* Ndio.

(3). *Wakili:* Unakubaliana na mimi pia hospitali zote pamoja na Aghakan na Regency zinaitegea maabara ya taifa kupima Virusi vya Korona.

🔹 *Mheshimiwa* Ndio.

(4). *Wakili:* Sasa mwambie mheshimiwa hakimu iliwezekana vipi Aghakan kutoa negative na muhimbili positive.

🔹 *Mheshimiwa:* Hata mimi mwenye ninashangaa imetokeaje.

(5). *Wakili:* Pia ieleze mahakama umejuaje kuwa wagonjwa wa wa Virusi vya Korona wamepungua ikiwa maabara ipo kwenye uchunguzi.

🔹 *Mheshimiwa:* Mhe. Hakimu ili swali gumu sana, ninaomba kwanza nishauriane na wataalamu wangu kabla ya kujibu swali hili.

True Lies...



Cc: mahondaw
 
Mkuu acha mihemko.kama hujui sema usaidiwe,watanzania tunatumia mikate,chapati mandazi na vitumbua kila siku ngano inalimwa wapi hapa Tanzania na kwa kiwango gani? Mafuta ya kupikia ukiacha ile clude sunflower oil mnayotumia ninyi wanyonge ni kiwanda only My.meru na murzah oil ndo wabazalisha refined sunflower oil na ni kidogo sana All palm oil is refined from imported clude oil toka Malaysia.Mchele.Serikali ikiamua tu kuzuia imported rice wengine wenu hamtaweza kununua.Nimekupa tu bidhaa chache
Mkuu wewe ndio hujui lolote unalozungumza. Tanzania ni kweli inaagiza baadhi ya bidhaa kama malighafi ya "Palm oil" toka Malaysia, lakini uagizaji wa mchele na mahindi ulishasimamishwa muda mrefu, sasa hivi tunazalisha zaidi ya matumizi yetu na ziada tunaeauzia majirani.

Kuhusu sukari, sasa hivi tunazalisha 75% ya mahitaji yetu, juhudi zinafanyika kuhakikisha ikifika mwishoni mwa mwaka Kesho tuweze kujitosheleza kwa sukari.

Hivi Mkuu ulishasikia wapi kwamba nchi imekumbwa na njaa kutokana na upungufu wa sukari?, sukari sio chakula, ila ni kiungo muhimu katika mapishi, unaweza kula mkate, chapati, maandazi bila sukari, kitakachopungua ni ladha ya chakula.

Kuhusu ngano, ni kweli kwamba baadhi ya viwanda, hasa vya Azam vinaagiza ngano toka nje, hii ni kutokana na kwamba, Azam anatengeneza bidhaa kwa ajili ya kuziuza nchi nyingi sio Tanzania pekee, kwahiyo ngano inayozalishwa Tanzania haimtoshi.

Mwisho ni kwamba, sisi tunazungumza kufunga mpaka wa Kenya na Tanzania, Kenya italazimika kutafuta Chakula toka nchi zingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*CROSS-EXAMINATION*

(1) *Wakili:* Unakubaliana na mimi kuwa tuna maabara moja tu ya kupima virus vya Korona hapa Tanzania.

🔹 *Mheshimiwa* Ndio

(2) *Wakili:* Na unakubaliana na mimi kuwa mahabara hiyo ipo kwenye uchunguzi na hivyo haiwezi fanya kazi kwa Sasa

🔹 *Mheshimiwa* Ndio.

(3). *Wakili:* Unakubaliana na mimi pia hospitali zote pamoja na Aghakan na Regency zinaitegea maabara ya taifa kupima Virusi vya Korona.

🔹 *Mheshimiwa* Ndio.

(4). *Wakili:* Sasa mwambie mheshimiwa hakimu iliwezekana vipi Aghakan kutoa negative na muhimbili positive.

🔹 *Mheshimiwa:* Hata mimi mwenye ninashangaa imetokeaje.

(5). *Wakili:* Pia ieleze mahakama umejuaje kuwa wagonjwa wa wa Virusi vya Korona wamepungua ikiwa maabara ipo kwenye uchunguzi.

🔹 *Mheshimiwa:* Mhe. Hakimu ili swali gumu sana, ninaomba kwanza nishauriane na wataalamu wangu kabla ya kujibu swali hili.
haaa haa inaudhi sana
 
Mkuu wewe ndio hujui lolote unalozungumza. Tanzania ni kweli inaagiza baadhi ya bidhaa kama malighafi ya "Palm oil" toka Malaysia, lakini uagizaji wa mchele na mahindi ulishasimamishwa muda mrefu, sasa hivi tunazalisha zaidi ya matumizi yetu na ziada tunaeauzia majirani.

Kuhusu sukari, sasa hivi tunazalisha 75% ya mahitaji yetu, juhudi zinafanyika kuhakikisha ikifika mwishoni mwa mwaka Kesho tuweze kujitosheleza kwa sukari.

Hivi Mkuu ulishasikia wapi kwamba nchi imekumbwa na njaa kutokana na upungufu wa sukari?, sukari sio chakula, ila ni kiungo muhimu katika mapishi, unaweza kula mkate, chapati, maandazi bila sukari, kitakachopungua ni ladha ya chakula.

Kuhusu ngano, ni kweli kwamba baadhi ya viwanda, hasa vya Azam vinaagiza ngano toka nje, hii ni kutokana na kwamba, Azam anatengeneza bidhaa kwa ajili ya kuziuza nchi nyingi sio Tanzania pekee, kwahiyo ngano inayozalishwa Tanzania haimtoshi.

Mwisho ni kwamba, sisi tunazungumza kufunga mpaka wa Kenya na Tanzania, Kenya italazimika kutafuta Chakula toka nchi zingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mnajidanganya kwa kujiaminisha kwamba Kenya inawategemea,njaa zetu ndo zinatusumbua zaidi na Wala si kwamba tunahuruma sana.Tunaangamia kwa kukosa maarifa
 
Na shule zifunghliwe, ukimwi ulikuwepo na masomo yaliendelea, nk
Sasa kama korona hakuna basi msituambie tvae barakoa wala kutakasa mikono kwa maji tiririka au "Santaiza" maana hata tukifa kwa korona sio ajabu maana malaria ,ukimwi, tb nazo zinaua!! Turudi kama awali basi toeni tamko basi msituambie tunawe mikono,waambie wizara ya afya wastop tangazo la mpoto maana hali ni shwari sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom