Rais Magufuli hajui kuna waliotekwa, wakarudishwa wakiwa mahakamani, wengine porini na wengine hawajawai kuonekana? Kazi ya vyombo vya dola ni ipi?

Ninashauri wapinzani waipe uzito hii hoja ya utekaji wakati wa kampeni, mtu anapaswa akigeuka kulia ni Ben saa nane yuko wapi? Akigeuka kushuto Azory yuko wapi, akigeuka nyuma ni kina nani waliompiga tundu lissu
risasi.

Amin Amin nawaambia, hakuna kete nzito kama hiyo, maana mtakuwa na platform huru ya kuongea bila kuzuiwa. Mnakumbuka 2015 mwigulu alivyokuwa anatembea na bwana yule aliyemwagiwa tindikali? Sasa imagine nyepesi kama ile kwa ccm ndo ilikuwa hoja tegemezi, hili la wapendwa wetu lenye kutia majonzi mazito inapaswa kuwatoa wao chozi la damu kabisa ikibidi. Bila kujali mgombea ni nani hii iwe hoja kuu

Hapo lazima mbichi na mbivu zitajulikana. Msimamo ni ule ule, mtu akiongelea madaraja swali ni wapendwa wetu wako wapi?

Akiongelea ndege swali wasiojulikana tutawajua lini?

Hapo Tutaelewana tu. Ndo kile kipindi mtu atatubu bila kupenda kwa kuona roho za waliopotea zinamuandama kila aendako

Itakuwa vizuri tukawa na picha kubwa za hawa wapendwa wetu zitandazwe kwenye kila mkutano wa kampeni, ikibidi hata katikati ya bendera za vyama wawekwe maana najua polisi hawatakuwa nyuma kupambana nazo.

Nionavyo mimi, hii kete ya utekaji inatosha kumweka pembeni ikijengewa hoja kwa uzito wa kipekee kabisa kama kauli mbiu ya kila mkutano wa kampeni.

Kwa akili ya kibinadamu hii itawapandisha hasira watawala na kujikuta wanashindwa hata kuzungumza sera yeyote kwani kazi yao itakuwa moja tu kujitetea dhidi ya tuhuma.

Kazi kwenu kina Zitto njia nyeupe kabisa hiyo


Sent using Jamii Forums mobile app
Kate ya utekaji,Maisha kuwa magumu,kusomeshwa namba ccm hawana hoja ya utetezi.Tegemeo lao ni ndege,sgr ,Stella goerge,
 
Utamaduni mpya wa kutekana na kumiminiana marisasi mchana mchana umeanza awamu hii...Tangu Mwalimu mwaka 1961, Mwinyi mwaka 1985, Mkapa mwaka 1995 na Jakaya mwaka 2005 haya mambo hayakuwepo..kuna HOJA ya msingi ya kujibu WHY NOW? watanzania huu si utamaduni wetu!!
Kauli kama zile ndizo ushahidi mzuri the hague wanatusubiria sisi tu ndo tufanye maamuzi wamfate mtu wao
 
Imran kombe awamu gani?
Utamaduni mpya wa kutekana na kumiminiana marisasi mchana mchana umeanza awamu hii...Tangu Mwalimu mwaka 1961, Mwinyi mwaka 1985, Mkapa mwaka 1995 na Jakaya mwaka 2005 haya mambo hayakuwepo..kuna HOJA ya msingi ya kujibu WHY NOW? watanzania huu si utamaduni wetu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninashauri wapinzani waipe uzito hii hoja ya utekaji wakati wa kampeni, mtu anapaswa akigeuka kulia ni Ben saa nane yuko wapi? Akigeuka kushuto Azory yuko wapi, akigeuka nyuma ni kina nani waliompiga tundu lissu
risasi.

Amin Amin nawaambia, hakuna kete nzito kama hiyo, maana mtakuwa na platform huru ya kuongea bila kuzuiwa. Mnakumbuka 2015 mwigulu alivyokuwa anatembea na bwana yule aliyemwagiwa tindikali? Sasa imagine nyepesi kama ile kwa ccm ndo ilikuwa hoja tegemezi, hili la wapendwa wetu lenye kutia majonzi mazito inapaswa kuwatoa wao chozi la damu kabisa ikibidi. Bila kujali mgombea ni nani hii iwe hoja kuu

Hapo lazima mbichi na mbivu zitajulikana. Msimamo ni ule ule, mtu akiongelea madaraja swali ni wapendwa wetu wako wapi?

Akiongelea ndege swali wasiojulikana tutawajua lini?

Hapo Tutaelewana tu. Ndo kile kipindi mtu atatubu bila kupenda kwa kuona roho za waliopotea zinamuandama kila aendako

Itakuwa vizuri tukawa na picha kubwa za hawa wapendwa wetu zitandazwe kwenye kila mkutano wa kampeni, ikibidi hata katikati ya bendera za vyama wawekwe maana najua polisi hawatakuwa nyuma kupambana nazo.

Nionavyo mimi, hii kete ya utekaji inatosha kumweka pembeni ikijengewa hoja kwa uzito wa kipekee kabisa kama kauli mbiu ya kila mkutano wa kampeni.

Kwa akili ya kibinadamu hii itawapandisha hasira watawala na kujikuta wanashindwa hata kuzungumza sera yeyote kwani kazi yao itakuwa moja tu kujitetea dhidi ya tuhuma.

Kazi kwenu kina Zitto njia nyeupe kabisa hiyo


Sent using Jamii Forums mobile app
Uchaguzi 2020 ni mwepesi sana kwa mgombea wa wapinzani
1. Kurudisha Uhuru wa maoni
2. Kurudisha upendo na mshikamano
3. Kurudisha demokrasia
4. Kurudisha usalama,was RAIA
5. Kurudisha uchumi mikononi mwa watu
6 kurudisha uchumi was sekta binafsi
7 kuleta katiba mapya ya wariobs
8 kufuta mbio za mwenge
9 kupandisha wafanyakazi mishahara na madaraja
Upinzani watashinda asubuhi kukiwepo tume huru.
 
"Mimi ningekua kiongozi ningeumizwa zaidi na hawa wanaotekwa au kupotea kweli, kuliko wale wanaozusha kutekwa au kupotea. Mtu mmoja aliyepotea au kutekwa na hajaonekana ataniuma zaidi kuliko wajinga 100 waliojizushia kupotea au kutekwa."

Hakuna shaka kuwa maneno haya yameandikwa na mtu mwenye akili kubwa!
 
Utamaduni mpya wa kutekana na kumiminiana marisasi mchana mchana umeanza awamu hii...Tangu Mwalimu mwaka 1961, Mwinyi mwaka 1985, Mkapa mwaka 1995 na Jakaya mwaka 2005 haya mambo hayakuwepo..kuna HOJA ya msingi ya kujibu WHY NOW? watanzania huu si utamaduni wetu!!
Kama Iran wamemshtukia Ayatollah basi na Watanzania washtuke! Adui yetu hayuko nje ya magogoni Bali anaishi humo. 2020 nasi tuseme basi kama 1979 Watanzania walivyokuwa na msemo "APIGWE NDULI APIGWE!" na ikawa hivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ujumla nchi hii magufuli ndie anaewaongoza upinzani.

Maana sera zote kakamilisha na hata ilani ya chama chake ya ahadi za uchaguzi kamaliza.

Ila kilichobaki kwa sasa ni watu kukosa sera na hoja zaidi ya kuvizia hotuba na kauli za viongozi wa CCM.ili watafutie kick.

Mleta thread hii ukiwa mmojawapo.

JPM bado yupo tu na tunajiandaa kumkabidhi nchi hadi 2025 viva bulldozer!

Sent using Jamii Forums mobile app


Yote ni kwa kuwa hujatekwa wewe au mtu yoyote katika familia yako , Mzigo wa mwenzako ni ganda la usufi

Siku yakikufika utaiona raha ya kutekwa
 
Kama Iran wamemshtukia Ayatollah basi na Watanzania washtuke! Adui yetu hayuko nje ya magogoni Bali anaishi humo. 2020 nasi tuseme basi kama 1979 Watanzania walivyokuwa na msemo "APIGWE NDULI APIGWE!" na ikawa hivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app


Irani ni mambo mengine , ule wote ni ugomvi wa mafuta ulianza tokea enzi za Shah wakati serikali ilitaifisha makampuni ya kuchimba mafuta ya Uingereza . Hao watu ukiwakatia mrija ndio utakiona. Pia wakazidi kutia mchanga kwenye ugali kwa kuwacha kuitumia dollar kuuzia mafuta.

Saddam na Gadaffi walifanya hivyo na yaliwafika , Bashar wa syria ndio yuko kwenye mechi
 
Na G malisa
View attachment 1321852
Watu wanaotekwa wapo. Wengine wanapatikana, wengine hawapatikani. Roma na Mo Dewji ni mifano ya waliotekwa wakapatikana. Azory Gwanda ni mfano wa waliotekwa lakini hajapatikana.

Mke wa Azory anadai mumewe alimfuata shambani akiwa kwenye gari lenye watu kadhaa ndani yake (hakuwatambua). Akamuomba funguo za nyumba akidai kuna nyaraka anaenda kuchukua ndani. Azory akaenda akiwa kwenye gari hiyo, baadae akamrudishia mkewe funguo. Hakuonekana tena hadi leo.

Watu wanaopotea baadae wakapatikana wapo. Mkulima mmoja wa bamia huko Mbutu, Yericko Nyerere aliwahi kupotea tukiwa nae pale Mayfair Hotel. Ghafla hatukumuona. Tukapiga simu hazikupatikana. Baada ya masaa kadhaa tukawasiliana na familia yake hakuwa nyumbani. Kesho yake familia yake ikaanza kuhaha kumtafuta.

Sisi marafiki kwa kushirikiana na familia tukazunguka vituo vyote vikubwa vya polisi jijini Dar lakini Polisi WAKAKANUSHA kumshikilia. Baada ya siku 15 tukamuona Yericko akipandishwa mahakamani Kisutu kwa tuhuma za uchochezi. Polisi walewale waliokanusha kwamba hawamshikilii Yericko ndio haohao waliomsindikiza mahakamani kusomewa mashtaka. Paradox.!

Watu wanaopotea na hawapatikani wapo. Ben Saanane ni mmoja wapo. Ben alitoweka/alitoweshwa katika mazingira ya kutatanisha. Tuliwataka TCRA waiagize kampuni ya simu ambayo Ben alikua akitumia mtandao wake watoe mawasiliano yake ya mwisho kwa polisi, ili polisi wapate mahali pa kuanzia upelelezi. Walifanya hivyo, lakini hadi leo polisi wanadai hawajui alipo Ben.

Kwahiyo wanaotekwa wapo. Wanaopotea wapo. Na wanaozusha kutekwa au kupotea wapo.

Mimi ningekua kiongozi ningeumizwa zaidi na hawa wanaotekwa au kupotea kweli, kuliko wale wanaozusha kutekwa au kupotea. Mtu mmoja aliyepotea au kutekwa na hajaonekana ataniuma zaidi kuliko wajinga 100 waliojizushia kupotea au kutekwa.

Kimsingi hawa wanaojizushia kupotea au kutekwa wanafanya hivyo baada ya kuona kuna watu wanapotea au kutekwa kweli. Kwahiyo nikiweza kudhibiti vitendo vya watu kutekwa au kupotea, nitakua nimewadhibiti pia wajinga wanaozusha. Kama hakuna mtu amewahi kutekwa au kupotea, mtu mwingine atapata wapi "locus" ya kuzusha kuwa ametekwa? Simple logic.!

Kwahiyo tukideal na hawa "wajinga" wanaozusha kutekwa/kupotea lakini tukaacha kudeal na wale waliotekwa/kupotea kweli, bado hatujatatua tatizo. Kwa sababu jamii yetu haiumizwi na wanaojizushia kutekwa/kupotea, bali inaumizwa na wale waliotekwa au kupoteza kweli.

Watu wa Rombo hawaumizwi na "Bwana Shirima" aliyedai kupotea kumbe amefichwa na nyumba ndogo, wanaumizwa na kijana wao Ben Saanane aliyepotea tangu November 2016 na hadi sasa hajulikani alipo. Machozi yao, kilio chao, na sala zao ni kwa Ben sio kwa "Bwana Shirima". Vivyo hivyo kwa familia ya Azory Gwanda na wengine.!

Tukiumizwa zaidi na kelele za "wazushi" badala ya kuumizwa na kilio cha familia za waliotekwa au kupotea kweli, tutakua hatujaitendea haki jamii. Kilio cha waliopotea au kutekwa kweli KINAUMIZA kuliko kelele za wanaozusha kutekwa/kupotea.!
Kilichoongelewa ni kuzushia vyombo vya ulinzi uongo kwamba ndio wanaoteka na kuua watu bila ya kuwa na ushahidi! Kuzushia vyombo vya usalama uongo!
Msibadilishe - kuzushia vyombo vya ulinzi wetu uongo ndicho kinacho katazwa na mkiendelea mtapata cha mtema kuni.
Kuumizwa na waliotekwa na waliopotea na waliokufa hiyo rukhsa, hakuna aliyekukataza. Sote tunaumizwa na hilo - lakini kusingizia mtu au chombo chochote bila ya kuwa na ushahidi, na pia ushahidi huo bila ya kuuwasilisha kwenye vyombo vinavyo husika, basi ukikamatwa usimlaumu mtu. Umetaka mwenyewe. Muwe wepesi wa kuelewa kilichosemwa.
 
Kauli hio ni udhihirisho Watekaji wamepewa kinga jamii itumie self defense act kujilinda kama ya tarime ndo funzo sahihi.
Kumbuka wamekuja kukuteka wakakuhoji na sio kukuuwa on sport hivo usiogope bunduki ogopa gari usikubali kuingia garini ukikubali umekwisha pambana nao hata wakikuuwa on spot hawawezi kukubeba ndugu watakuaga kwa heshima kuliko kuliwa na chatu.Heri pigana kufa kuliko kutolewa kafala kwa shetani na hawa washirikina
Hii nimeipenda zaidi, ogopa Gari usiogope bunduki..
naanza rasmi mafunzo ya kareti Ni kuzichapa tu kwa sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kauli hio ni udhihirisho Watekaji wamepewa kinga jamii itumie self defense act kujilinda kama ya tarime ndo funzo sahihi.
Kumbuka wamekuja kukuteka wakakuhoji na sio kukuuwa on sport hivo usiogope bunduki ogopa gari usikubali kuingia garini ukikubali umekwisha pambana nao hata wakikuuwa on spot hawawezi kukubeba ndugu watakuaga kwa heshima kuliko kuliwa na chatu.Heri pigana kufa kuliko kutolewa kafala kwa shetani na hawa washirikina
Kuna siri nzito hapa,Moyo wangu umekufa ganzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilichoongelewa ni kuzushia vyombo vya ulinzi uongo kwamba ndio wanaoteka na kuua watu bila ya kuwa na ushahidi! Kuzushia vyombo vya usalama uongo!
Msibadilishe - kuzushia vyombo vya ulinzi wetu uongo ndicho kinacho katazwa na mkiendelea mtapata cha mtema kuni.
Kuumizwa na waliotekwa na waliopotea na waliokufa hiyo rukhsa, hakuna aliyekukataza. Sote tunaumizwa na hilo - lakini kusingizia mtu au chombo chochote bila ya kuwa na ushahidi, na pia ushahidi huo bila ya kuuwasilisha kwenye vyombo vinavyo husika, basi ukikamatwa usimlaumu mtu. Umetaka mwenyewe. Muwe wepesi wa kuelewa kilichosemwa.
Kwa hiyo wale alio washuti Zakaria kule Tarime ni ngedele?
Msipende kutisha watu nyie! Awamu hii inahusika sana na yanayoendelea. Mkiambiwa mnateka basi kanusheni kwa kuwakamata watekaji na sio ngonjera

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilichoongelewa ni kuzushia vyombo vya ulinzi uongo kwamba ndio wanaoteka na kuua watu bila ya kuwa na ushahidi! Kuzushia vyombo vya usalama uongo!
Msibadilishe - kuzushia vyombo vya ulinzi wetu uongo ndicho kinacho katazwa na mkiendelea mtapata cha mtema kuni.
Kuumizwa na waliotekwa na waliopotea na waliokufa hiyo rukhsa, hakuna aliyekukataza. Sote tunaumizwa na hilo - lakini kusingizia mtu au chombo chochote bila ya kuwa na ushahidi, na pia ushahidi huo bila ya kuuwasilisha kwenye vyombo vinavyo husika, basi ukikamatwa usimlaumu mtu. Umetaka mwenyewe. Muwe wepesi wa kuelewa kilichosemwa.
Swali ni moja,Toka utekaji huu umeanza ni hatua gani imechukuliwa na hivyo vyombo vya ulinzi na usalama ili Wananchi waachane hizo hisia zakuviisi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom