Rais Magufuli, haina haja ya kuongeza mshahara kwa watumishi wa Umma

Levels baby

JF-Expert Member
Sep 26, 2019
831
768
Kwanza nianze kwa kusema mimi ni mwana CCM asilia sio wa kuja kama wapiga gitaa hapo ndani Lumumba na mtaani ili mradi mkono uende kinywani na wengine kuanzisha vikundi vya kwaya/blogs kwa ajili ya kumsifia mkuu wa nchi ili wapate chochote maana wameujua udhaifu wa mkuu wa nchi.

Turudi kwenye mada kumekuwa na malalamiko mengi sana ya watumishi wa umma kudai kuongezewa mshahara, 1sasa hapa linakuja suala mbona wenzetu wanang'ang'ania kuongezwa mshahara kwani hizo kazi za umma si ni kama kujitolea na ambae kachoka kujitolea anaweza kutoka na kuja kupambana na wajasiliamali huku mtaani aone mchezo unavyoenda.

Pia mtumishi akiona mshahara haumtoshi si aje mtaani awaachie wengine maana kuna vijana wengi sana mtaani wanahitaji ile nafasi yake na kwa mshahara ule ule anaodai haumtoshi, lakini vijana huku wanaona utawatosha kabisa na wataendesha familia kupitia hikohiko kidogo watachopata serikalini.

Namalizia, mkuu wa nchi haina haja ya kuongeza mshahara ambae hawezi awapishe wenzie ambao wataweza bora hizo hela peleka kwa maendeleo mengine sio kuwapa hao wakaa kwenye viti kungoja mshahara kila mwisho wa mwezi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huna tofauti na ccm wapiga gitaa hapo lumumba kwani mnapishana kwa ala tu! Awali ya yote punguza wivu na wafanyakazi waajiriwa wa umma kwani wakati wao wanasoma kwa bidii wewe ulitegea na usisahau wakipata wao za kuwatosha kwa mwezi mzima nao wajasiriamali watapata nafuu kwa biashara zao!
 
Hoja nzuri.

Na mimi ningeshauri wale wenye mishahara minono kuanzia laki saba kwenda juu mishahara yao ikatwe na ipunguzwe ili hizo fedha zitumike kuajiri vijana wapya!

Tuna mapesa mengi yanaliwa na watu wachache badala ya kugawanywa kwa watu wengi watakaoshiriki kufanya kazi na kujenga nchi!

Jitu moja linatafuna milioni kumi!!!??

Hizo milioni kumi zingeajiri vijana kumi na tano wengine kwa mwezi mmoja!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ata wao wakipewa hizo nafasi watadai kuongezewA mshahara pia

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio ubinafsi huo.

Kila mmoja anataka kurundikiwa mapesa mengi atafune yeye tu!

Ndio maana wanasiasa wanajipilipa mishahara ya kutisha halafu hapo hapo wanashangaa kwanini wengine hawana ajira.

Kila senti ikitumika vizuri na kwa nidhamu tuna uwezo wa kuajiri kila muhitimu katika nchi hii.

Chanzo cha unemployement nchini ni mafisadi wanaoatamia mapesa na kuyaficha vyumbani mwao!

Mtu mmoja anakula mishahara ya watu ishirini!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna aina mbili za mali phsical na intelect sasa boss sukari imepnd ni physical vp kuhusu aina nyngne ya mali si kutakuw na imbalance mkuu
 
Maskini yeyote yule wa mali na akili ana mawazo kama yako

Hayo maendeleo unayo yasema wewe hayawezi kutimia pasipo uwepo wa wasaidizi ambao ndio hao wahitaji kulipwa

Usipo mjali anaye kusaidia kuleta maendeleo utaendelea kupiga hatua kurudi nyuma maana watakuhujumu kwa visasi

Watu wenye mawazo kama yako ni wachache sana ila ndio wajinga walio baki duniani.

Unakosea sana unawapo waita watumish eti wakaa kwenye viti kusubiri mshahara , wewe hakika ni jinga na pumbavu

Hospitalini wagonjwa wanatibiwa na hao hao na ndio msaada wao kwenye maendeleo ya nchi

Barabara zinazo jengwa zina simamiwa na hao hao unao waita wewe wakaaa kwenye viti,

Mh Rais hawezi kutibu wagonjwa , kufundisha wanafunzi, kusimamia ulinzi, ujenzi wa miundo mbinu,usimamizi wa miradi, nk yeye mwenyewe na ndio maana kukawa na wasaidizi ili kumsaidia ili aweze kupeleka nchi mbele

Sasa kama wewe akili yako inaona kwamba Rais anafanya kila kitu mwenyewe hivyo hana haja ya kuwajali walio chini yake basi hakika wewe hukustahili kuwa binadamu bali ni bundi usiye faa hata kwa nyama

Na hapo nikwamba wewe ni kijana mjinga ulie feli masomo ukakosa ajira upo mtaani huna kazi huna pesa huna akili wala ufahamu ndio maana unawachukia wenzio walio soma wakapata ajira ya serikali na wanalipwa mishahara na nikuhakikishie utaendelea kuwachangia kodi ili walendelee kulipwa vizuri zaid huku wewe ukiendeleza kupiga miayo.
 
GODZILLA,
Maskini mwingine huyu hapa hatari hii yaani mshahara wa laki 7 kwako ni mshahara mnono hakika post yako hii inatoa picha ya maisha uliyo nayo kuwa wewe ni maskini wa mali na akili umefeli masomo yako huna ajira ndio maana upo hapa kuchukia wenzenu walio soma wakaajiliwa

Mtaendelea sana kuwachangia watumish wa umma ili waendelee kulipwa vizuri zaid huku nyie mkiendelea kupiga miayo na kuwachukia huku mkiwachangia.
 
Hivi laki saba nao ni mshahara mnono?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa wewe fisadi uliyezoea kujichotea mapesa na kujilipa mamilioni ya shilingi, ni wazi kwamba laki saba ni fedha ya mandazi tu kwako!

Kwa kuzingatia hali ya unemployement nchini, kuwalipa watu wachache mishahara mikubwa huku wengine wakiwa wanateseka kwa kukosa ajira ni kutokuwa na utashi tu!

Kila shilingi ina uwezo wa kugawanywa kwa nidhamu na kuwafikia watu wengi kwa pamoja.

Kila shilingi ikigawanywa kwa nidhamu ina uwezo wa kufuta kabisa tatizo la ajira nchini!

Shida ya wanasiasa na counterparts wao MAFISADI wana uchu na ubinafsi wa kutisha.

Kujilipa milioni kumi mtu mmoja ni DHULMA MBAYA SANA.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom