Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,315
- 24,177
Kama kuna wakati TANROADS ilikuwa na uozo ni wakati wa CEO wake Ephraim Mrema.
Madeni mengi kama siyo yote yaliasisiwa na huyu jamaa.
Nauliza huyu kawekwa kiporo?
Madeni mengi kama siyo yote yaliasisiwa na huyu jamaa.
Nauliza huyu kawekwa kiporo?
Wandugu,
Kama tujuavyo, Waziri wa ujenzi, Dr. John P. Magufuli, mchapa kazi, mbunifu, mchukia ufisadi, na asiyependa ubabaishaji. Wakati huo huo, mkurugenzi TANROADS, Ephraim Mrema, ni mbabaishaji, mzembe, mkumbatia ufisadi, na inasemekana kawekwa pale kulinda uozo wa wakubwa wa nji hii.
Sipati picha siku ikitokea magufuli akiwa katika harakati za kusaficha uchafu kwenye wizara ya ujenzi kama vile kuwafukuza wakandarasi wababishaji, kama ilivyokuwa enzi zile kwenye awamu ya Ben Mkapa. Kufika TANROADS akakutana na madudu ya Mrema. Je mrema atamtunishia kifua kwa sababu tu ni mteule wa Rais na yuko supported na vigogo wala nchi?