Rais Magufuli awatimua Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mwenyekiti wa Bodi na Katibu Mkuu Uchukuzi

Najutia sana kumpa kura yangu Lowassa! magufuli 2020 panapo uhai nakupa kura yangu
 
Na mm ndiyo Pombe Magufuli!! Aongezewe ulinzi wananchi tupo tayari kuchangia hela zetu mfukoni kwaajili ya uongeza ulinzi wa Rais Pombe Magufuli
 
Kama katibu mkuu wa wizara amewajibishwa vipi aliyekuwa waziri wake?

Vipi Mwakyembe na Sitta.
 
Rais Dk. John Pombe Magufuli aipiga chini Bodi ya TPA, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) Bw. Awadhi Masawe. Pia amemchomoa Katibu Mkuu wizara ya Uchukuzi Dk. Mwinjaka na kamsimamisha kazi. Pia baadhi ya wafanyakazi wa TPA na TRA wamesimamishwa kwa uchunguzi zaidi.

Massawe aliteulia na Samwel Sitta kushikila nafasi ya Mhandisi Madeni Kipande aliyesimamishwa kwa tuhuma za utendaji mbovu ili kupisha uchunguzi.

kipande ndio alikua mtu sahihi na bandari ilikua infanya kazi vzr nadhan maguful amrudishe kipande enzi zake bandari ilikua inafanya kwa ufanisi '''relatively'"'
 
Rais Magufuli amemtimua Mkurugenzi Mtendaji Bandari TPA Awadhi Masawe na mwenyekiti wa bodi ya TPA Prof. Msambichaka na watendaji kadhaa kwa kushindwa kazi.

Aidha amemtimua Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi kwa kushindwa kuisimamia TRL.

Taarifa zaidi nawaletea soon...

Safi sana ukipigwa chini unachomwa ndani kwanza halafu unatapishwa kodi yetu, kile kibabu cha TRL hicho cha kuchoma ndani tena kiende segerea kwanza kitwambie zile bil 13 za kufufua reli ziko wapi.
 
Ukweli nausema. Namuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake kwa mapambano dhidi ya ufisadi, rushwa na dhuluma waliyoyaanzisha. Nawatakia kila lililo jema katika mapambano yao. Lakini, nchi si TRA na Bandari tu. Na wala si TRL tu. Nchi ni wananchi.

Fukuzafukuza na shtakishtaki inayoendelea kutokea TRA,Bandari na TRL si mwarobaini wa nchi nzima. Nchi si Dar es Salaam tu ambapo mambo yote yanayoendelea sasa yanafanyika huku. Dar es salaam ni mkoa mmojawapo tu wa Tanzania.

Watanzania wana imani kubwa na Serikali yao. Bado wanaisubiri. Wanaisubiri kwakuwa yanayoendelea sasa hayawafaidishi moja kwa moja. Hayawapi malazi, chakula wala mavazi. Wananchi wanataka huduma. TRA,Bandari na TRL zisimkwamishe Rais kuwafikia wananchi wote.

Baraza la Mawaiziri liundwe na kazi ifanywe. Kuna maswali ya Wabunge yanasubiri kujibiwa kwa tafiti hapo Januari. Mawaziri watapata muda gani kutafakari na kuyajibu maswali? Na kadhalika na kadhalika.Muda unataradadi!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es salaam
 
Nakumbuka wakati wa kampeni mgombea wa UKAWA Edward Lowassa alisema "Uongozi ni kufanya maamuzi, ni bora ukafanya mwamuzi ukakosea kuliko kutofanya".

Rais Magufuri anafanya kile ambacho kinatakiwa, "MAAMUZI". Maamuzi afanyayo kiongozi humfanya ajipambanue yeye ni mtu wa aina gani.

Yes mkuu na Lowasa akiwa bado ccm kuna siku bungeni alisema, Tanzania ni nchi ya watu kulalamika, viongozi wanalalamika waziri mkuu analalamika, anatakiwa mtu wa kuchukua maamuzi magumu, watu wakamdhihaki eti mzee wa maamuzi magumu, sasa haya ndio Lowasa aliyokuwa anayataka, Magufuli halalamiki ana tenda tu, ndio angeteuliwa Membe yangekuwa yaleyale. Safi sana sasa aje kwa walio wateua hawa kushika hizo nyadhifa.
 
kipande ndio alikua mtu sahihi na bandari ilikua infanya kazi vzr nadhan maguful amrudishe kipande enzi zake bandari ilikua inafanya kwa ufanisi '''relatively'"'

Wewe akili uliyonayo niyakuvukia Barabara tu....Yaani Watanganyika tuko zaidi ya 45ml mpaka leo unaamini ni Kipande peke yake ndio anaefaa....duh....Nchi hii ndio maana ccm wanajipigia tu
 
Ukweli nausema. Namuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake kwa mapambano dhidi ya ufisadi,rushwa na dhuluma waliyoyaanzisha. Nawatakia kila lililo jema katika mapambano yao. Lakini, nchi si TRA na Bandari tu. Na wala si TRL tu. Nchi ni wananchi.

Fukuzafukuza na shtakishtaki inayoendelea kutokea TRA,Bandari na TRL si mwarobaini wa nchi nzima. Nchi si Dar es Salaam tu ambapo mambo yote yanayoendelea sasa yanafanyika huku. Dar es Salaam ni mkoa mmojawapo tu wa Tanzania.

Watanzania wana imani kubwa na Serikali yao. Bado wanaisubiri. Wanaisubiri kwakuwa yanayoendelea sasa hayawafaidishi moja kwa moja. Hayawapi malazi, chakula wala mavazi. Wananchi wanataka huduma. TRA,Bandari na TRL zisimkwamishe Rais kuwafikia wananchi wote.

Baraza la Mawaiziri liundwe na kazi ifanywe. Kuna maswali ya Wabunge yanasubiri kujibiwa kwa tafiti hapo Januari. Mawaziri watapata muda gani kutafakari na kuyajibu maswali? Na kadhalika na kadhalika.Muda unataradadi!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Hivi umeshindwa kuficha ujinga wako! Hujui umhimu wa bandari na TRA? kweli?
 
Back
Top Bottom