Rais Magufuli awachana Kilwa kwa kumchagua mpinzani Bwege. Awataka kutofanya makosa tena uchaguzi ujao

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,075
4,111



Wakuu, MAENDELEO HAYANA CHAMA

Rais Magufuli akiwa safarini kutoka Mtwara, ameombwa na mwanakijiji Jimbo la Kilwa kwamba hawana Stendi ya Magari hivyo anaomba wajengewe. Rais Magufuli amejibu kwamba siku nyingine waangalie wawakilishi wanaowachagua ili waweze kufanya vile yeye anavyowaagiza. Mbunge wa jimbo hili aliyemaliza muda wake ni Seleman Bungara aka Bwege Mzee wa ''Umesikia Wapi'' ambaye alikuwa anatokea chama cha wananchi CUF Habari

Rais amezidi kusema kwamba miradi kama hiyo ni ya wabunge na Madiwani ndiyo wanapaswa kuisimamia hivyo kuwataka wabaki na Bwege wao


Rais Magufuli amesema haya...

Nilikuja hapa nikasema nichagulieni watu nitakaokuwa nawaagiza wanafanya ninayoyataka mkasema hapana, Mkamchagua Bwege basi shauri yenu na bwege wenu mwambie awatengenezee stendi

Kazi ya Stendi ni ya madiwani, wabunge. Ukikosea kuchagua, nafuu ukosee kuoa au kuolewa. Ukikosea kuchagua ni tatizo kubwa.


Na hili ndugu zangu niwaombe, muwe waangalifu katika kuchagua. Mchague watu ambao watakuwa kwa ajili ya watu masikini.

Tunatuma hapa fedha za road fund, tunatuma fedha hapa za halmashauri, zimeshindwa kweli kujenga stendi?

Lakini kwa sababu mnanichagulia, wao wenyewe mastendi unategemea mimi mwenyewe nifanyeje? Huo ndiyo ukweli sitaki kuwaficha mlikosea kuchagua.


Sasa katika uchaguzi wa mwaka huu mjipange vizuri, mchague mtu ambaye mtakuwa mmempa stendi akikataa nitamfukuza hata kwenye chama. Lakini leo nitamfukuza huyo aliyeko kwenye chama sijui hata yuko kwenye chama gani, nitamchukulia hatua gani?


Chama cha ACT Wazalendo kimelaani vikali na kuwahamasisha wananchi kukemea vikali kauli hizi za kibaguzi. Wamedai kuwa kitendo cha kuhamasisha ubaguzi na kuingilia mamlaka ya wananchi katika kuchagua mtu wamtakaye kinakiuka misingi ya Katiba yetu.
 
Du kwahiyo ili tupate maendeleo ni lazima tuchague wabunge wa CCM.
CCM wapo wengi Bungeni(ndiyo wenye majimbo mengi) , maana yake kama majimbo yao yote yangekuwa na maendeleo, Taifa lingekuwa mbali sana kiuchumi. Tunalia umasikini kila siku, changamoto ni zile zile maji, barabara, afya,elimu halafu anakuja hapa kuleta porojo za kijinga.
 
CCM wapo wengi Bungeni(ndiyo wenye majimbo mengi) , maana yake kama majimbo yao yote yangekuwa na maendeleo, Taifa lingekuwa mbali sana kiuchumi. Tunalia umasikini kila siku, changamoto ni zile zile maji, barabara, afya,elimu halafu anakuja hapa kuleta porojo za kijinga.
Tunachagua wabunge tunao waelewa, wanaojua kuwasiliana na sisi, wanaosikiliza hoja na shida zetu.
Sasa kama mgombea tunaemuelewa na akatuelewa yuko ACT Wazalendo ni lazima tumuache tumchague wa CCM.

Ni nini maana ya kuwa na vyama vingi?
 
Back
Top Bottom