Rais Magufuli awaapisha Wakuu wa Mikoa, Awaongelea Kasesela na aliyepigwa fimbo na Ndugai

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Leo Tarehe 29 Rais Magufuli anawapisha wakuu wa mikoa na wilaya asubuhi hii live from Azam two na TBC1.

Rais Magufuli:
Gondwe ninajua unatangaza,sasa utakwenda kutangaza maendeleo unakokwenda,ufanye kama unatangaza tangaza tu.

Rais Magufuli:
Mchakato wa kuwapata Ma-DC haukuwa rahisi, ilibidi tutizame historia ya kila mmoja wao.

Rais Magufuli:
Kuna mabadiliko madogo tuliyoyafanya kutokana na jina lilikosewa, kwa hiyo aliyestahili tumeshamuweka.

Rais Magufuli:
Ningeweza nikataja majina yote mliopo hapa mpaka yule aliyepigwa fimbo na mtani wangu, karibu kila jina nalifahamu na sifa yake.

Rais Magufuli:
Mna mamlaka makubwa ya kumuweka mtu Mahabusu ila msiende tu kuonea watu.

Rais Magufuli:
Mnaweza kufikiri tumewachagua sisi lakini inawezekana Mungu ametutumia sisi kuwachagua ninyi.

Rais Magufuli:
Nilikuwa namuona DC wa Iringa anabeba watoto wakamsema sana, na mimi nikasema abaki hapa hapa

Rais Magufuli:
Nilitegemea sana baada ya kuwateua, nilitegemea labda mngekuja robo tu, ninawashukuru sana kwa kuja.

Rais Magufuli:
Watanzania wengi tumezoea kulalamika, tunapenda tu kupewa, hatutaki kufanya kazi.

Rais Magufuli:
Ni matumaini yangu hamtaniangusha, hata sura zenu zinaonyesha ni wachapa kazi, nendeni mkachape kazi.

Rais Magufuli:
Nyinyi wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya mna mamlaka hata ya kuweka watu mahabusu, ila msiende kuonea watu.

Rais Magufuli: Mkasimamie yale tuliyowaahidi sisi wana CCM, mkayatekeleze kwa nguvu zote

Rais Magufuli:
Watanzania wengi wana changamoto nyingi, nina imani hamtaiangusha serikali hii.

Rais Magufuli:
Nataka niseme ukweli, wale ma-DC tuliowaacha hawakufikia vigezo

Mchakato wa kuwapata ma-DC ulikuwa mgumu, ilibidi tuangalie historia ya kila mmoja, tuliangalia mambo mengi sana.

Rais Magufuli anazungumza kwenye sherehe za kuwaapisha kiapo cha uadilifu wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa wapya.
 

Unaguna nini? kigeu geu cha hawa kimekuchefua?

13233029_1590768097881921_7440964151336377693_n-jpg.360620
 
Wakati anamalizia mh Rais amesema kuna marekebisho kidogo kwa wakuu wa wilaya,aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida ni Miraji Mtaturu ambaye alikuwa katibu wa CCM mkoa wa Mwanza na pia wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro ameteuliwa Agnes Hokororo.Kwa Ikungi awali alitangazwa mtu mwingine na kwa Rombo aliyeteuliwa awali alikuwa pia Mbunge na Rais amesema hakuna sababu ya mtu mmoja kuwa na vyeo viwili yaani ubunge na ukuu wa wilaya
 
Back
Top Bottom