Rais Magufuli awaambia Waandishi wa Habari wawe makini, hawako huru kihivyo...

Magazetini

JF-Expert Member
Aug 16, 2014
588
1,698


Habari waungwana, leo Rais John Magufuli anaapisha watu kadhaa na miongoni ni teuzi iliyozua rapsha ya wizara ya habari, sanaa, utamaduni na michezo ambayo ilimuondoa Nape Nnauye kwenye nafasi yake huku timing ikileta mjadala. Nafasi hio inachukuliwa na aliyekuwa waziri wa katiba na sheria, Dkt Harisson Mwakyembe huku Palamaganda Kabudi akiiziba nafasi yake anapotoka.

Pia Leo anaapishwa katibu mkuu wa Ikulu ila kwa sasa wanaoapishwa ni mabalozi mbalimbali wanaowakisha nchi zao.
===========

Mawaziri Dkt Harisson Mwakyembe na Palamaganda Kabudi wameshaapa, wanaoapa kwa sasa ni mabalozi wanaonda kuwakilisha katika nchi mbalimbali.
======

Anaeongea kwa sasa ni Rais Magufuli na kuwapongeza wote walioteuliwa. Amewaambia wasitegemee mazuri sana kwa kazi huwa zina lawama hasa kwa Tanzania ambapo kuna grupu la watu wao siku zote ni kulalamika.

Amedai Mwakyembe mitandao ilisema asingekuja kuapishwa pia wapo walioposti kuwa Kinana angeongea leo ilhali yeye kamtuma India kwa matibabu.



====​

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John P. Magufuli, leo amewaapisha Dr Harrison Mwakyembe na Prof Palamagamba Kabudi pamoja na mabalozi kadhaa Ikulu Jijini Dar.

Mwakyembe ameapishwa kuwa Waziri mpya wa habari, Profesa Kabudi kaapishwa kaapishwa kuwa waziri wa Katiba na Sheria.
==>Haya ni mambo machache aliyoyasema Rais Magufuli Leo
1.Kuna wengine walisema Kinana leo angezungumza na waandishi, wakati nimemtuma India ambapo atakuwa kwa zaidi ya siku 10
2.Tunataka kuitoa nchi katika hali ya mazoea kuipeleka katika mstari ambao ni sahihi
3.Ukiangalia siku iliyofuata baada ya Rais wa Benki ya Dunia kuja, magazeti yote yaliandika habari nyingine tofauti-
4.Niwatake waandishi wa habari muwe wazalendo, Tanzania ikiharibika na nyie pamoja na wanaowatuma muandike wote mtaharibikiwa
5.Hata magazeti ya leo yana picha ya mtu mmoja ambaye amefanya kosa moja, utadhani kosa ni linaungwa mkono na serikali
6.Niwatake wamiliki wa vyombo vya habari muwe waangalifu, kama mnadhani mna uhuru wa namna hiyo, kuweni makini sana
7.Kuna vyombo vingine vya habari sehemu yenye ugomvi ndio wanapeleka kamera na habari hizo zinapewa muda mrefu, 'watch out'
8.Vyombo vingine haviandiki mazuri ya mtu, lakini wakipata mabaya yake ndiyo yanajaza kurasa
 
FB_IMG_1490301542054.jpg
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom