Rais Magufuli atoa wiki moja taratibu za uwekezaji kwa Kampuni ya Sugar Investment Trust(SIT) zimalizike

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Ameelezeka maagizo hayo kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara baada ya Kampuni hiyo, Sugar Investment Trust(SIT) kucheleweshwa kuwekeza katika uzalishaji wa sukari tangu mwaka 2017

Ametoa maagizo hayo leo Aprili 17, 2019 akiwa Ikulu jijini Dar baada ya kukutana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Kampuni hiyo kutoka Mauritius, Gansam Boodram aliyeongozana na Balozi wa Mauritius nchini, Jean Pierre Jhumun

Boodram ameeleza kuwa yupo tayari kulima ekari 25,000 za mashamba ya miwa na uwekezaji huo utawezesha kuzalishwa kwa tani 125,000 za sukari, kutoa ajira za kudumu 3,000 na ajira za muda 5,000

Rais ameagiza ufanyike uchambuzi wa haraka katika maeneo ya Bonde la Mto Rufiji Mkoani Pwani, shamba la Mkulazi Mkoani Morogoro na eneo la Kibondo Mkoani Kigoma ili mwekezaji huyo aanze mara moja uwekezaji

Aidha, amezionya Taasisi za Serikali kikiwemo Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kwa kutoharakisha taratibu za kuwawezesha wawekezaji kuwekeza
1555506826599.png


IMG-20190417-WA0012.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa kazi tu. Kigoma kuna maeneo kama Mukarazi-Kibondo na Mayange-Kasulu ambayo yanastawi miwa na kuna maji ya kutosha kwa hiyo ni mazuri kwa uwekezaji huo wa viwanda vya sukari.
Hapa kazi tu...awamu ya tano mambo ni moto
 
Asante Mr President kwa kunirahisishia mazingira ya uwekezaji, kuna eneo nimelitamani hapa pwani nataka nianze kujenga kiwanda kesho nione mtu atakayekuja kuniuliza.
 
Kwa hilo nampongeza Magufuli, watumishi wanafanya makusudi kuchelewesha vibali.

Hasa wafanyabishara wakubwa wa Sukari (wale wanaopewa vibali kuagiza nje) Tanzania ndio wanaotumia nguvu nyingi kukwamisha miradi ya kilimo cha miwa nchini.
 
Waswahili wataacha lini ubabaishaji?
Tamaa ya baadhi ya watu ziwakoseshe ajiri maelfu ya watu.

Kama kuna tatizo kwanini hawalisemi? La sivyo tunajua wanataka 10% isiyokuwa na risiti
Mr President deal with these problems accordingly
Na weka ndani baadhi maana hili la kufukuza kazi halisaidii kitu

Sent from my SM-G570F using Tapatalk
 
Back
Top Bottom