Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Iddy Kimanta amesema kuwa mwili wa aliyekuwa katibu Tawala mkoa wa Arusha Richard Kwitega aliyefariki jana kwa ajali ya gari, utaagwa kesho katika uwanja wa mpira wa Sheikh amri abed jijini Arusha na Kisha kusafirisha kwa ndege ya serikali iliyotolewa na Rais Magufuli, kwenda Mkoani Mwanza kwa mazishi yatakayofanyika siku ya jumamosi wilayani Sengerema, nyumbani kwa marehemu.
Marehemu Kwitega alipoteza maisha hapo Jana katika eneo la Mdorii Mkoani Manyara wakati akielekea Dodoma Kikazi ambapo Dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo amelazwa katika hospital ya Mkoa iliyopo mjini Babati akipatiwa matibabu baada ya kunusurika.
Marehemu Kwitega alipoteza maisha hapo Jana katika eneo la Mdorii Mkoani Manyara wakati akielekea Dodoma Kikazi ambapo Dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo amelazwa katika hospital ya Mkoa iliyopo mjini Babati akipatiwa matibabu baada ya kunusurika.