Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,007
- 9,873
Watakaowasilisha Hati zao za Utambulisho kwa Mamlaka hii leo ni
1. Bw. David William Concar, Uingereza
2. Bw. Muhammad Saleem, Pakistan
3. Bw. Didier Chassot, Uswisi ( Switzerland).
Maneno ya Balozi wa Uingereza
Mara baada ya kutoka kukabidhi hati ya Ubalozi balozi amesema anatumaini uchaguzi utakuwa huru na haki na utamalizika salama. Aliulizwa namna anavyoweza kuuzungumzia uchumi wa Tz amesema badi anajifunza lakini anaona sio mbaya kwa kuweka umeme kwenye vijiji na kujenga miundombinu kama barabara
Balozi wa Pakistan, amesema Tanzania ni nchi nzuri sio tu kwa sekta ya utalii bali pia kwa uwekezaji na sayansi, amesema ametembelea maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Kilimanjaro, nk na ameona ni nchi inayovutia sana