Rais Magufuli apinga uzazi wa mpango, asema wananchi wanapotoshwa

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,599
141,416
Rais Magufuli amewataka wananchi wafanye kazi na kwamba uzazi wa mpango ni swala linalotafskarisha.

Amesema baadhi ya nchi huko ulaya zinaujutia mpango huo kwani umezikosesha nguvu kazi.

Rais amesema ameishi Uingereza Kwa mwaka mmoja pia amekaa Ujetumani, Canada, Norway nk hivyo anaelewa vizuri Athari za mpango huo.

Source: TBC



======

Rais Magufuli amepingana na sera ya Serikali yake ya uzazi wa mpango akidai kuwa sera hiyo inapunguza nguvu kazi kwa Taifa

Ameyasema hayo leo Septemba 9, 2018 akiwa mjini Meatu katika mkoa wa Simiyu huku akiongeza kuwa Watanzania waendelee kuzaa lakini wachape kazi ili kukidhi mahitaji ya watoto wao

Amesema ”Najua Waziri wa Afya Ummy Mwalimu hapa angependa kuongelea mambo ya uzazi wa mpango lakini mimi mengine huwa sikubaliani nayo sana, utapangiwaje kuzaa?"

Rais aliendelea kwa kusisitiza kuwa ''Najua kesho watapinga sana lakini ukweli ndio huo watu wamejazwa mawazo ya ajabu, huwezi kuwa Mwanaume kisha ukubali kufungiwa kizazi! Yaani ng'ombe wako umtoe kizazi na wewe tena ukatolewe kizazi? Mimi sikubali''

Aidha, alitolea mfano katika nchi mbalimbali alizowahi kuzitembela akisema “Mimi Ulaya nimekaa, nafahamu madhara ya kutokuzaa, nchi gani sijaenda, Japan nimekaa, Uingereza nimekaa mwaka mzima, Ujerumani nimekaa, Canada nimekaa na nikachaguliwa kuwa 'co-chair' wa mawaziri ardhi duniani, Denmark, Norway, utanidanganya wapi, China nimefika."
 
Kwa nchi zetu za watu weusi hizi, ambazo shughuli kuu ni ukulima wa kienyeji, ufugaji wa kienyeji, uvuvi wa kienyeji, kupikia kwa mkaa na kuni, uchuuzi wa bidhaa za kichina na mitumba ya Ulaya barabarani n.k

kuwa na watu wengi inamaanisha kutakua na kuvamiwa kwa mapori, misitu, samaki kuvuliwa kupita kiasi, vyanzo vya maji kukauka, migogoro ya wakulima na wafugaji na kuongezeka kwa slums mjini (nyumba za uswahilini) na kushindwa kudhibiti uchafu wa miji na matatizo mengine kibao

Sasa hivi haya yaneshaanza kujitokeza Tanzania, Wananchi wanavamia mbuga na mapori hadi serikali inawachomea nyumba, kuvuna mkaa maporini na kupelekea migogoro mingi na mamlaka husika, Wanavyovua samaki hadi wanakaribia kuisha ziwani, na hadi Magufuli mwenyewe anemteua waziri 'kichaa' kudhibiti wavuvi, wakulima na wafugaji wanapigana kisa mashamba, miji yetu pia haijapangiliwa wote tunajua na mengine

Ethiopia na Nigeria ndio nchi za watu weusi zinazoongoza kwa watu wengi.

Na ndio nchi pia zinazoongoza kwa kutoa wahamiaji haramu,

Maisha magumu nchini kwao, ajira hakuna, ardhi pia ni shida ni migogoro isiyoisha, wapo desperate kwenda Ulaya, wengine wamejaa South Africa huko, Waethiopia tunawakamata kwenye malori kila siku, wengine wanafurumushwa Ulaya na Israeli

Hali ikiwa ngumu sana watanzania na sisi tutaanza kuzamia nchi zilizoendelea kupata ajira na maisha bora

Uzazi wa Mpango haumaanishi mtu kutozaa kabisa, unamaanisha kuzaa idadi ya watoto unaowataka na muda unaotaka wewe...

Miaka 50 ijayo vyanzo vya maji, maziwa,misitu na ardhi yenye rutuba ambavyo ndio vitu tunavyovitegemea waafrika ku survive vitakua adimu mno na tutakuwa tunatamani kuzamia Ulaya ama tutaomba hata tutawaliwe tena tu
 
Back
Top Bottom