Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,479
- 30,144
Tulimsikia wenyewe Rais wetu Magufuli wakati akilihutubia Taifa siku chache zilizopita, akituhimiza wananchi tukachape kazi na kuwa tusitishwe na vyombo vya habari vya kibeberu, kwa kuwa ugonjwa wa corona siyo tishio kiasi hicho wanachotuaminisha!
Kwa kweli nilishangazwa sana na maelekezo hayo ya Rais wetu, wakati nchi nyingi, zikiwemo nchi jirani zimechukua hatua ngumu sana, zikiwemo za kuwafungia majumbani, wananchi wao, ili wasitoke
Ninachojiuliza hivi Rais anawezaje kutuhimiza wananchi tukachape kazi, wakati yeye mwenyewe anajua kuwa kazi hizo hazipo, kutokana na wananchi hao kupoteza kazi zao kutokana na ugonjwa huo wa corona?
Hivi Rais hajui kuwa shughuli nyingi za kibiashara zimeathirika sana kutokana na ugonjwa huo?
Hivi Rais hajui kuwa Hoteli nyingi zimefunga biashara na kuwaambia wafanyakazi wao waende majumbani kwao kwenda kupumzika kwa lazima?
Hivi Rais wetu hajui kuwa mashirika mengi ya ndege "yanapumulia mashine" kutokana na mashirika hayo kusitisha huduma zao za usafiri, kwa ajili ya wageni wengi kutoweza kusafiri kutokana na ugonjwa huo wa corona?
Sasa atawahimazaje wafanyakazi hao wakachape kazi, wakati waajiri wao wamewapumzisha kutokana na janga hilo la corona?
Serikali nyingi za nje zishaanza kuwafidia wananchi wao kutokana na madhara makubwa sana waliyoyapata kutokana na jinamizi hili la corona nchini mwao, ikiwemo nchi jirani ya Kenya.
Ningependa nimuulize huyu anayejiita Rais wa wanyonge, je ni lini atawafidia wananchi wake wanyonge, kutokana na madhara makubwa waliyoyapata kutokana na janga hili la corona?
Ni makosa makubwa kwa serikali yetu kuendelea na "business as usual" katika kipindi hiki kigumu sana cha ugonjwa huu wa corona
Maswali yako mengi, lakini itoshe tu kusema, kwa hayo màswali machache niliyoyauliza hivi leo
Kwa kweli nilishangazwa sana na maelekezo hayo ya Rais wetu, wakati nchi nyingi, zikiwemo nchi jirani zimechukua hatua ngumu sana, zikiwemo za kuwafungia majumbani, wananchi wao, ili wasitoke
Ninachojiuliza hivi Rais anawezaje kutuhimiza wananchi tukachape kazi, wakati yeye mwenyewe anajua kuwa kazi hizo hazipo, kutokana na wananchi hao kupoteza kazi zao kutokana na ugonjwa huo wa corona?
Hivi Rais hajui kuwa shughuli nyingi za kibiashara zimeathirika sana kutokana na ugonjwa huo?
Hivi Rais hajui kuwa Hoteli nyingi zimefunga biashara na kuwaambia wafanyakazi wao waende majumbani kwao kwenda kupumzika kwa lazima?
Hivi Rais wetu hajui kuwa mashirika mengi ya ndege "yanapumulia mashine" kutokana na mashirika hayo kusitisha huduma zao za usafiri, kwa ajili ya wageni wengi kutoweza kusafiri kutokana na ugonjwa huo wa corona?
Sasa atawahimazaje wafanyakazi hao wakachape kazi, wakati waajiri wao wamewapumzisha kutokana na janga hilo la corona?
Serikali nyingi za nje zishaanza kuwafidia wananchi wao kutokana na madhara makubwa sana waliyoyapata kutokana na jinamizi hili la corona nchini mwao, ikiwemo nchi jirani ya Kenya.
Ningependa nimuulize huyu anayejiita Rais wa wanyonge, je ni lini atawafidia wananchi wake wanyonge, kutokana na madhara makubwa waliyoyapata kutokana na janga hili la corona?
Ni makosa makubwa kwa serikali yetu kuendelea na "business as usual" katika kipindi hiki kigumu sana cha ugonjwa huu wa corona
Maswali yako mengi, lakini itoshe tu kusema, kwa hayo màswali machache niliyoyauliza hivi leo