Rais Magufuli anapokiri "hapa kazi tu" imeshindwa kuleta uzalishaji(maendeleo)kwa miaka miwili,je anakosea wapi?

papaa musofe

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
842
1,475
Kwa Mara ya kwanza nimemsikia Rais John Pombe Magufuli akikiri kwamba tangu aingie madarakani takribani miaka miwili iliyopita,ameshindwa kuhakikisha Sera zake zinazaa matunda (uzalishaji)na maendeleo kwa taifa

Hali hii ya kupungua kwa ukuaji wa uchumi(uzalishaji)umemfanya ashindwe hata kulipa stahiki za wafanyakazi ikiwemo kuongeza mishahara na au increment

Kabla ya kipindi chake,JK alikuwa akiongeza mishahara na kuilipa pia bila kubabaika,hii ilimaanisha kwamba awamu ya nne ilikuwa na Sera zilizofanya uchumi ukue na kuzalisha mali iliyofanya taifa lijikimu

Je Magufuli anakwama wapi kulielekeza taifa katika Sera zitakazofanya uzalishaji uongezeke? Ni kwa nini uzalishaji umepungua?

Tunapanga bajeti zetu sawasawa kwa kuangalia sekta zinazozalisha na hivyo kuziongezea nguvu na raslimali fedha na utaalamu? JK na Mkapa walielekeza raslimali katika sekta zipi ambazo ziliwafanya waendeshe nchi kwa kurelax,wakulima wakipata pembejeo,wafanyakazi wakilipwa mishahara na kupata nyongeza,barabara zikajengwa,Taasisi imara zikaundwa kama Sumatra,Tanroad,Ewura,miradi ya maji ikafanyika,misingi ya biashara ikawa imara na taifa likaaminika

Kwa nini JPM anakwama? Anajifunza nini kutoka kwa watangulizi wake kuhusu uendeshaji wa uchumi ambao ulisimama imara kwa takribani miaka 20?

Hii falsafa ya hapa kazi tu ilichambuliwa kisayansi,maana tangu mkoloni hajaja tulikuwa tunafanya kazi,pamoja na kufanya kazi bado taifa hili ni masikini,anamaanisha kufanya kazi kwa maguvu tu kama wabeba zege?

Hapa kazi tu kwa mkulima inamaanisha alime tu?lakini si miaka yote tunalima?! Hapa kazi tu kwa dereva wa mabasi,si miaka yote anaendesha magari!? Hapa kazi tu kwa muhasibu,si miaka yote anatunza hesabu!? Hapa kazi tu kwa injinia,si miaka yote anafanya uinjinia wake!? Hapa kazi tu kwa mwandishi wa habari,si miaka yote anafanya uandishi wa habari!?

Je hii falsafa ya hapa kazi tu ni ngeni?ina maana hapo zamani tulikuwa hatufanyi kazi?nchi hii angeikuta ilivyo kama tulikuwa hatufanyi kazi? Na kwa nini tangu aanze kuimba hapa kazi tu ndio uzalishaji umeshuka
 
Tehetehe!

Uchumi ni kama jua,huwezi kulificha,ni kama kikohozi,kaanza taratibu kukubaliana na wana JF,uchumi umekwama
Kwanza atafakari,sekta zipi zinaongeza huo uzalishaji na kwenye bajeti anaziangalia vipi pamoja na mazingira yanayozizunguka
 
Kwa akili zake navyozijua ipo siku ataomba aachie ngazi, maana tangu aingie madarakani hakuna unafuu wowote wa maisha Na kiuchumi uliopatikana!! Kila kona ya nchi hii ni kilio!!! Sasa kapigilia msumari kwenye jeneza la watumishi kuwa hakuna nyongeza ya mshahara!!! At the same time anatazamia aone ufanisi na uzalishaji ukikuwa makazini na viwandani!!! Huyu jamaa naona bado yuko usingizini akiota ndoto labda Akifanikiwa ataamka 2020.
 
Kwa akili zake navyozijua ipo siku ataomba aachie ngazi, maana tangu aingie madarakani hakuna unafuu wowote wa maisha Na kiuchumi uliopatikana!! Kila kona ya nchi hii ni kilio!!! Sasa kapigilia msumari kwenye jeneza la watumishi kuwa hakuna nyongeza ya mshahara!!! At the same time anatazamia aone ufanisi na uzalishaji ukikuwa makazini na viwandani!!! Huyu jamaa naona bado yuko usingizini akiota ndoto labda Akifanikiwa ataamka 2020.
Akae na mawaziri wake wamuelekeze sekta zinazozalisha ni zipi na wachambue kwa nini zimedumaa katika awamu hii
 
Hapa kazi tu ni kauli ya kisiasa tu kama zile zingine za Maisha bora kwa kila Mtanzania Nchi inabidi iwe na vision imara na isimamiwe,, sio kila Mtawala anakuja na mawazo yake bila strategic plan zozote mwisho wa siku ni failure kama taifa tunaingia tutakuwa tunapiga marktime kila miaka kumi .Yule alikuwa na kilimo kwanza akafeli, huyu kaja na hapa kazi tu na viwanda naye akiendelea hivi atafeli vile vile.. Sasa Hapa kazi tu so what! Kipi kipya tutapata tofauti na miaka mingine , Haya tumuombe tu labda Mungu atampa maono mapya
 
Hapa kazi tu ni kauli ya kisiasa tu kama zile zingine za Maisha bora kwa kila Mtanzania Nchi inabidi iwe na vision imara na isimamiwe,, sio kila Mtawala anakuja na mawazo yake bila strategic plan zozote mwisho wa siku ni failure kama taifa tunaingia tutakuwa tunapiga marktime kila miaka kumi .Yule alikuwa na kilimo kwanza akafeli, huyu kaja na hapa kazi tu na viwanda naye akiendelea hivi atafeli vile vile.. Sasa Hapa kazi tu so what! Kipi kipya tutapata tofauti na miaka mingine , Haya tumuombe tu labda Mungu atampa maono mapya
Kila mtu anakuja na staili yake ya kuongoza nchi,tumekuwa shamba la majaribio
 
Hapa kazi tu ni kauli ya kisiasa tu kama zile zingine za Maisha bora kwa kila Mtanzania Nchi inabidi iwe na vision imara na isimamiwe,, sio kila Mtawala anakuja na mawazo yake bila strategic plan zozote mwisho wa siku ni failure kama taifa tunaingia tutakuwa tunapiga marktime kila miaka kumi .Yule alikuwa na kilimo kwanza akafeli, huyu kaja na hapa kazi tu na viwanda naye akiendelea hivi atafeli vile vile.. Sasa Hapa kazi tu so what! Kipi kipya tutapata tofauti na miaka mingine , Haya tumuombe tu labda Mungu atampa maono mapya
Mkuu mbona hiyo iko too obvious. hakuna haja ya kuzunguka zunguka!!

Kama kilimo kwanza kimetushinda tutawezaje Viwanda kwanza!!
 
Mkuu mbona hiyo iko too obvious. hakuna haja ya kuzunguka zunguka!!

Kama kilimo kwanza kimetushinda tutawezaje Viwanda kwanza!!
Viwanda vinapata malighafi nyingi kwenye Kilimo,sheria ya historia ilishapanga kwamba lazima Kilimo kiimarike ndipo uwaze kusindika ziada,sasa hata Kilimo cha chakula tu hatujaweza

Ni sawa na "kuyabemenda maendeleo" ni sawa na kuwa na maendeleo njiti(watoto wanaozaliwa kabla ya muda) ambayo hayadumu

Nyerere alitaka kuiruka sheria ya historia inayosema jamii lazima ipitie kwenye ubepari ndipo iende kwenye ujamaa,tena ubepari ukomae kabisa na utaenda kwenye ujamaa sio kwa matamko,bali jamii yenyewe itajiongoza bila kusubiri mwanasiasa,Mzee Nyerere hakusubiri ubepari ukue na ukome,kairusha nchi sarakasi mpaka kwenye ujamaa,

Sheria ya historia ikamgomea,ujamaa ukagoma,jamii yenyewe ikarudi hatua iliyotakiwa kupitia,ubepari ambao tunao

Kuirusha nchi hatua hizo imeleta hasara kubwa ya mamia kama si maelfu ya trilioni
 
Hameni nchi wenzenu marekani wanazamia Canada kumkimbia Trump na nyie zamieni msumbiji wala hakuna atakayewazuia.
Akili yako nyembamba haijajua methali. Ukipewa challenge ya maneno unatoa bunduki au unatafakari kabla ya kulopoka?
 
Viwanda vinapata malighafi nyingi kwenye Kilimo,sheria ya historia ilishapanga kwamba lazima Kilimo kiimarike ndipo uwaze kusindika ziada,sasa hata Kilimo cha chakula tu hatujaweza

Ni sawa na "kuyabemenda maendeleo" ni sawa na kuwa na maendeleo njiti(watoto wanaozaliwa kabla ya muda) ambayo hayadumu

Nyerere alitaka kuiruka sheria ya historia inayosema jamii lazima ipitie kwenye ubepari ndipo iende kwenye ujamaa,tena ubepari ukomae kabisa na utaenda kwenye ujamaa sio kwa matamko,bali jamii yenyewe itajiongoza bila kusubiri mwanasiasa,Mzee Nyerere hakusubiri ubepari ukue na ukome,kairusha nchi sarakasi mpaka kwenye ujamaa,

Sheria ya historia ikamgomea,ujamaa ukagoma,jamii yenyewe ikarudi hatua iliyotakiwa kupitia,ubepari ambao tunao

Kuirusha nchi hatua hizo imeleta hasara kubwa ya mamia kama si maelfu ya trilioni
Yaani Mkulu angenda kwanza kuangalia mafail ya KILIMO kwanza kujua tulikosea wapi ili alekebishe kabla ya kuja na hii sera ya viwanda!!
 
Back
Top Bottom