Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Tafsiri ya neno demokrasia ni kiongozi aliyechaguliwa na watu katika uchaguzi ulio huru na wa haki kwa ajili ya kuwatumikia watu
Tumemsikia wenyewe Rais Magufuli katika ziara yake akiwa huko Kimamba-Kilosa, mkoani Morogoro akiwaambia wakazi wa huko kuwa eti walikosea kumchagua mbunge wao, kwa kuwa walimchagua kwa jazba, bila ya kutafakari na ndiyo sababu inayowapata wakazi wa huko wakose maendeleo!
Ni jambo lililonistua sana niliposikia kauli hiyo kwa kuwa ninajua kuwa mbunge wa Kilosa ni mwanaccm mwenzao, kwa kuwa nilizizoea kauli hizo za Mheshimiwa Rais akizitoa kwenye majimbo waliochagua wabunge wa upinzani
Nika-realize kuwa kumbe kauli aliyowahi itoa Mwalimu Nyerere ni ya kweli tupu kuwa mtu aliyeanza kula nyama ya mtu hataweza acha kuila kamwe!
Ubaguzi aliouanza Jiwe wa kuwabagua wapinzani sasa umeingia kwenye CCM yake!
Nikakumbuka kauli aliyowahi itoa siku chache za nyuma, kuwa matokeo ya kura za maoni za majimbo za CCM si lolote wala chochote safari hii, kwa kuwa itategemea yeye kama Mwenyekiti ameamkaje siku hiyo, kwa kuwa upo uwezekano, hata kama umeshinda kwenye kura za maoni kwenye jimbo lako, lakini Kamati Kuu isilirudishe jina lako kwa kuwa litakuwa limekatwa na bila kutolewa sababu zozote zile
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi kuna haja gani ya kuitisha kura za maoni za CCM, iwapo kumbe inaeleweka, kura hizo si lolote wala chochote, kwani safari hii, Mwenyekiti wa CCM ndiyo "atakayeamua" nani awe mgombea wa ubunge wa jimbo husika?
Dalili zimeshaanza kujitokeza kutokana na hizo ziara za Rais majimboni na "kuwachagulia" wabunge huko majimboni mwao.
Ili tufahamu kuwa Mwenyekiti wetu tayari ana majina yake mfukoni, hebu nijaribu kuwakumbusha namna huyo Mwenyekiti wetu alivyoweza "wachagulia" wabunge kwenye majimbo yao.
Tulimsikia wenyewe Rais wetu akiwaambia wakazi hao wa Kimamba-Kilosa, kuwa "amemu-import" toka Dodoma, Mbunge atakayewafaa, Profesa Palamagamba Kabudi, ili awe Mbunge wao
Akaendeleza hizo "tamaa" zake Rais alipofanya ziara ya mikoa ya Kusini akiwaambia wakazi wa huko, wamchague msanii anayevaa "milegezo" Harmonize awe mbunge wao kwa jimbo la Tandahimba!
Hakuishia hapo, bali alipotembelea jimbo la Kongwa, aliwaomba wakazi wa huko wasikose kumchagua mbunge wao Spika wa Bunge la Jamhuri, Job Ndugai, ingawa kwa "body language" yao wananchi wa huko walionyesha kumkatalia pendekezo lake hilo
Aliendelea "kuwachagulia" wananchi Mbunge wao pale alipotembelea jimbo la Mbeya mjini, akawaomba wakazi wa huko wamchague kuwa mbunge wao, Naibu wa Spika, wa Bunge letu la Jamhuri, Tulia Ackson, kwani yeye anaamini huyo mwanamama, ndiyo "the right choice' kwa wana Mbeya!
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi wanaccm wa majimboni mna haja gani ya kupiga kura za maoni yenu huko majimboni kwenu, kwa kuwachagua wabunge wenu, wakati mnajua kuwa Mwenyekiti wenu tayari ana majina yake "mfukoni" ya wabunge wake anaotaka yeye wawe wabunge wa Bunge lijalo la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Tumemsikia wenyewe Rais Magufuli katika ziara yake akiwa huko Kimamba-Kilosa, mkoani Morogoro akiwaambia wakazi wa huko kuwa eti walikosea kumchagua mbunge wao, kwa kuwa walimchagua kwa jazba, bila ya kutafakari na ndiyo sababu inayowapata wakazi wa huko wakose maendeleo!
Ni jambo lililonistua sana niliposikia kauli hiyo kwa kuwa ninajua kuwa mbunge wa Kilosa ni mwanaccm mwenzao, kwa kuwa nilizizoea kauli hizo za Mheshimiwa Rais akizitoa kwenye majimbo waliochagua wabunge wa upinzani
Nika-realize kuwa kumbe kauli aliyowahi itoa Mwalimu Nyerere ni ya kweli tupu kuwa mtu aliyeanza kula nyama ya mtu hataweza acha kuila kamwe!
Ubaguzi aliouanza Jiwe wa kuwabagua wapinzani sasa umeingia kwenye CCM yake!
Nikakumbuka kauli aliyowahi itoa siku chache za nyuma, kuwa matokeo ya kura za maoni za majimbo za CCM si lolote wala chochote safari hii, kwa kuwa itategemea yeye kama Mwenyekiti ameamkaje siku hiyo, kwa kuwa upo uwezekano, hata kama umeshinda kwenye kura za maoni kwenye jimbo lako, lakini Kamati Kuu isilirudishe jina lako kwa kuwa litakuwa limekatwa na bila kutolewa sababu zozote zile
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi kuna haja gani ya kuitisha kura za maoni za CCM, iwapo kumbe inaeleweka, kura hizo si lolote wala chochote, kwani safari hii, Mwenyekiti wa CCM ndiyo "atakayeamua" nani awe mgombea wa ubunge wa jimbo husika?
Dalili zimeshaanza kujitokeza kutokana na hizo ziara za Rais majimboni na "kuwachagulia" wabunge huko majimboni mwao.
Ili tufahamu kuwa Mwenyekiti wetu tayari ana majina yake mfukoni, hebu nijaribu kuwakumbusha namna huyo Mwenyekiti wetu alivyoweza "wachagulia" wabunge kwenye majimbo yao.
Tulimsikia wenyewe Rais wetu akiwaambia wakazi hao wa Kimamba-Kilosa, kuwa "amemu-import" toka Dodoma, Mbunge atakayewafaa, Profesa Palamagamba Kabudi, ili awe Mbunge wao
Akaendeleza hizo "tamaa" zake Rais alipofanya ziara ya mikoa ya Kusini akiwaambia wakazi wa huko, wamchague msanii anayevaa "milegezo" Harmonize awe mbunge wao kwa jimbo la Tandahimba!
Hakuishia hapo, bali alipotembelea jimbo la Kongwa, aliwaomba wakazi wa huko wasikose kumchagua mbunge wao Spika wa Bunge la Jamhuri, Job Ndugai, ingawa kwa "body language" yao wananchi wa huko walionyesha kumkatalia pendekezo lake hilo
Aliendelea "kuwachagulia" wananchi Mbunge wao pale alipotembelea jimbo la Mbeya mjini, akawaomba wakazi wa huko wamchague kuwa mbunge wao, Naibu wa Spika, wa Bunge letu la Jamhuri, Tulia Ackson, kwani yeye anaamini huyo mwanamama, ndiyo "the right choice' kwa wana Mbeya!
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi wanaccm wa majimboni mna haja gani ya kupiga kura za maoni yenu huko majimboni kwenu, kwa kuwachagua wabunge wenu, wakati mnajua kuwa Mwenyekiti wenu tayari ana majina yake "mfukoni" ya wabunge wake anaotaka yeye wawe wabunge wa Bunge lijalo la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?