Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Taarifa ambayo imestua watu wengi ni hii taarifa ya pamoja iliyotolewa na ubalozi wa Marekani na uingereza nchini, wakilaani vikali vitendo vya ukiukwaji wa haki za msingi wa kibinadamu nchini
Wapo watu wengi sana waliounga mkono tamko hilo na wakieleza kuwa nchi hizo za Magharibi zimechelewa mno kutoa tamko hill na wapo wale watu wanaoitwa "praise and worship team for Magufuli" ambao wanasema mambo ya ndani ya nchi yetu hayapaswi kuingiliwa na mataifa ya kigeni
Siyo siri kuwa kuna ukiukwaji wa hali ya juu wa haki za msingi wa binadamu nchini na wananchi wamepiga kelele sana, lakini ni dhahiri kuwa watawala wetu wameamua kuweka pamba masikioni mwao na kutosikiliza kilio hicho!
Hata hivyo kwa wale wenzetu wanaotetea vitendo hivi vya ukiukwaji wa hali ya juu wa haki za binadamu, ningependa tu kuwauliza kitu kimoja, nyinyi mnaendelea kutetea kwa nguvu zote Rais wetu, lakini je mshajiuliza kuwa Tanzania siyo kisiwa cha kujifanyia mambo yake itakavyo na kuna mikataba mbalimbali ya kimataifa ambayo inakiukwa waziwazi na utawala huu wa awamu ya tano??
Tuchukulie hili suala la mwandishi Kabendera lilivyoshughullkiwa, hivi ndivyo inavyopaswa kushughulikiwa hata kwa sheria zetu za ndani??
Yule mwandishi Kabendera amebebwa usiku wa manane nyumbani kwake na "watu wasiojulikana,"/ambao hawwkutaka hata kujitambulisha, hivi ndiivyo sheria zetu zinavyosema kweli??
Kibaya zaidi ni pale Kamanda Mambosasa alipokiri mwenyewe kuwa Jeshi hilo ndilo linalomshililia mwandishi huyo kituoni kwao na huku likiwa linamhoji kuhusu kile alichokiita kuwa ni uraia wake wenye utata bila kumpa nafasi mtuhumiwa huyo aweze kuleta mwanasheria wake wakati wa mahojiano hayo, je hivi ndivyo sheria zetu za nchi zinavyosema??
Jambo la kushangaza zaidi ni pale walipomburuza mahakamani mwandishi huyo na kumsomea mashitaka ya kubambikiwa kuwa eti amashitakiwa kwa makosa matatu ambayo ni kujiunga na genge la kihalifu, utakatishaji pesa na ukwepaji kodi, makosa yote hayo siyo yale ambayo Kamanda Mambosasa alitueleza watanzania kuwa ndiyo waliyomhoji Kabendera kituoni kwao.
Hivi kwa vitendo kama hivyo vya ukiukwaji wa hali ya juu wa misingi ya kibanadamu, kama dunia haitapaza sauti zao, watakuwa wanaenda kinyume cha ubinadamu
Nimalizie tu post yangu kwa kisema kuwa kitendo cha serikali ya Tanzania kulalamikia kitendo cha ubalozi wa Marekani na Uingereza, kutoa tamko la pamoja kulaani vitendo vya serikali yetu kuminya sheria tulizojiwekea sisi wenyeee, ni sawasawa na majirani wanapoona baba wa mwenye nyumba jirani hao, akifanya vitendo vya "kishenzi" vya kuwacharaza bakora wanawe mara kwa mara na kuvifumbia macho na kusema kuwa havimuhusu kwa kuwa ni vya nyumba jirami
Hakika katika nchi hii kwa hivi sasa hakuna mtu aliye salama hata kidogo, kwa hiyo ni wajibu wa kila mtanzania kupaza sauti yake kwa hali ya juu kabisa ili kuvikomesha vitendo hivyo vya kinyama na vinavyokiuka misingi ya kibinadamu
Tukificha ficha maradhi, mwisho kilio kitatuumbua. OVA
Wapo watu wengi sana waliounga mkono tamko hilo na wakieleza kuwa nchi hizo za Magharibi zimechelewa mno kutoa tamko hill na wapo wale watu wanaoitwa "praise and worship team for Magufuli" ambao wanasema mambo ya ndani ya nchi yetu hayapaswi kuingiliwa na mataifa ya kigeni
Siyo siri kuwa kuna ukiukwaji wa hali ya juu wa haki za msingi wa binadamu nchini na wananchi wamepiga kelele sana, lakini ni dhahiri kuwa watawala wetu wameamua kuweka pamba masikioni mwao na kutosikiliza kilio hicho!
Hata hivyo kwa wale wenzetu wanaotetea vitendo hivi vya ukiukwaji wa hali ya juu wa haki za binadamu, ningependa tu kuwauliza kitu kimoja, nyinyi mnaendelea kutetea kwa nguvu zote Rais wetu, lakini je mshajiuliza kuwa Tanzania siyo kisiwa cha kujifanyia mambo yake itakavyo na kuna mikataba mbalimbali ya kimataifa ambayo inakiukwa waziwazi na utawala huu wa awamu ya tano??
Tuchukulie hili suala la mwandishi Kabendera lilivyoshughullkiwa, hivi ndivyo inavyopaswa kushughulikiwa hata kwa sheria zetu za ndani??
Yule mwandishi Kabendera amebebwa usiku wa manane nyumbani kwake na "watu wasiojulikana,"/ambao hawwkutaka hata kujitambulisha, hivi ndiivyo sheria zetu zinavyosema kweli??
Kibaya zaidi ni pale Kamanda Mambosasa alipokiri mwenyewe kuwa Jeshi hilo ndilo linalomshililia mwandishi huyo kituoni kwao na huku likiwa linamhoji kuhusu kile alichokiita kuwa ni uraia wake wenye utata bila kumpa nafasi mtuhumiwa huyo aweze kuleta mwanasheria wake wakati wa mahojiano hayo, je hivi ndivyo sheria zetu za nchi zinavyosema??
Jambo la kushangaza zaidi ni pale walipomburuza mahakamani mwandishi huyo na kumsomea mashitaka ya kubambikiwa kuwa eti amashitakiwa kwa makosa matatu ambayo ni kujiunga na genge la kihalifu, utakatishaji pesa na ukwepaji kodi, makosa yote hayo siyo yale ambayo Kamanda Mambosasa alitueleza watanzania kuwa ndiyo waliyomhoji Kabendera kituoni kwao.
Hivi kwa vitendo kama hivyo vya ukiukwaji wa hali ya juu wa misingi ya kibanadamu, kama dunia haitapaza sauti zao, watakuwa wanaenda kinyume cha ubinadamu
Nimalizie tu post yangu kwa kisema kuwa kitendo cha serikali ya Tanzania kulalamikia kitendo cha ubalozi wa Marekani na Uingereza, kutoa tamko la pamoja kulaani vitendo vya serikali yetu kuminya sheria tulizojiwekea sisi wenyeee, ni sawasawa na majirani wanapoona baba wa mwenye nyumba jirani hao, akifanya vitendo vya "kishenzi" vya kuwacharaza bakora wanawe mara kwa mara na kuvifumbia macho na kusema kuwa havimuhusu kwa kuwa ni vya nyumba jirami
Hakika katika nchi hii kwa hivi sasa hakuna mtu aliye salama hata kidogo, kwa hiyo ni wajibu wa kila mtanzania kupaza sauti yake kwa hali ya juu kabisa ili kuvikomesha vitendo hivyo vya kinyama na vinavyokiuka misingi ya kibinadamu
Tukificha ficha maradhi, mwisho kilio kitatuumbua. OVA