Rais Magufuli anakosea kuchukulia upinzani kama maadui badala ya kuwachukulia kama wadau muhimu wa maendeleo

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Tumeshuhudia tokea serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, juhudi kubwa ikifanyika kwa ajili ya kuua upinzani ili nchi ibaki kuwa na mfumo wa chama kimoja

Tumeshuhudia pia wabunge na madiwani wakinunuliwa na kuahidiwa nafasi za "ulaji" iwapo tu wataafiki kujiunga na chama cha CCM kwa kile wenyewe walichokibatiza jina la kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli za kuleta maendeleo hapa nchini

Kutokana na tabia hiyo ya hao wanasiasa "wasaliti" wanaojiunga na CCM tumekuwa tunalazimika kurudia uchaguzi ambao unaligharimu Taifa letu mabilioni ya pesa ambazo zingeweza kufanya shughuli nyingine za maendeleo. Mathalani ujenzi wa madarasa ya shule na hospitali

Lakini kwa bahati mbaya sana priority no 1 ya serikali hii imekuwa siyo tena kujenga madarasa wala hospitali zetu ambazo ziko katika hali mbaya, badala yake ni kuua upinzani nchini!

Kipindi wanachopitia viongozi wa upinzani nchini, hususani wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema ni kipindi kigumu sana ambacho hawajawahi kukipitia tokea mfumo wa vyama vingi nchini urejeshwe nchini kikatiba mwaka 1992

Viongozi kadhaa wa upinzani wamefungwa jela kwa sababu za kisiasa na viongozi wengine wameathirika kutokana na vizuizi wanavyowekewa vya kutofanya siasa na karibu viongozi wote wa chama kikuu cha upinzani cha Chadema wanakabiliwa na kesi mbalimbali za kile kinachoitwa uchochezi kwenye Mahakama zetu

Ninachojaribu kujiuliza ni iweje serikali hii ya awamu ya tano iwachukulie wapinzani maadui wakubwa badala ya kuwachukulia kuwa ni wadau muhimu sana wa maendeleo nchini mwetu??

Na kama kweli kama wapinzani wangekuwa maadui wa maendeleo wangezuiwa kwenye mataifa yaliyostawi sana kimaendekeo mathalani Taifa lenye uchumi namba moja duniani la Marekani, ambalo kwenye Taifa hilo Rais wake Donald Trump anatukanwa waziwazi na wapinzani wa nchi hiyo lakini hawafanywi chochote kwa kuwa Taifa hilo linachukulia kama sehemu ya demokrasia ya kueleza hisia za wananchi kwa ajili ya kuleta maendeleo ya Taifa hilo

Vile vile humu barani Afrika nchi ya Afrika Kusini ambayo ndiyo inayoongoza barani humu kiuchumi, wameimarisha sana demokrasia nchini mwao

Nitoe tu ushauri kwa watawala wetu waiache demokrasia ishamiri nchini kwa kuwa hawana uwezo wa kuua upinzani wa nchi ambao umeota mizizi ndani ya mioyo ya mamilioni ya watanzania

Mungu ibariki Tanzania
 
Wao ndo wameanza kumchukulia kama adui tokea anazindua bunge wakatoka nje hivo hapa naona unaandika utumbo tu
Hivi wewe huoni namna wapinzani wa nchi hii wanavyokuwa treated kama wahaini ndani ya nchi yao??

Badala yake umeliona hilo la kutoka Bungeni kulikofanywa na wabunge wa upinzani??

Umejiuliza ni sababu zipi zilizofanya wabunge wa upinzani kutoka Bungeni??

Ni obvious wanapinga kuburuzwa na Spika Ndugai, ambaye anachukulia uwingi wa wabunge wa CCM kama "fimbo" ya kuwachapia wapinzani
 
Hamna cha kumrembea aachwe afanye atakavyo, ila ataaingoza hii nchi miaka yake mitano. Kisha atatumia madaraka yake kujitangaza tena rais. Baada ya hapo atakaa kushoto na upinzani utadhidi kuimarika. Huu ni mwaka wa 3 wala hajafanikiwa kuua upinzani zaidi ya kuwafanyia hujuma. Huko kwenye box la kura nako watu wamemuonyesha kuwa hawababaiki na mbwembwe zake. Afanye hujuma apendavyo kwa wapinzani wake lakini hana ushawishi kwa watu wengi kama walivyo wapinzani. Hamna haja ya kujikomba kwake maana yeye sio Mungu.
 
Hamna cha kumrembea aachwe afanye atakavyo, ila ataaingoza hii nchi miaka yake mitano. Kisha atatumia madaraka yake kujitangaza tena rais. Baada ya hapo atakaa kushoto na upinzani utadhidi kuimarika. Huu ni mwaka wa 3 wala hajafanikiwa kuua upinzani zaidi ya kuwafanyia hujuma. Huko kwenye box la kura nako watu wamemuonyesha kuwa hawababaiki na mbwembwe zake. Afanye hujuma apendavyo kwa wapinzani wake lakini hana ushawishi kwa watu wengi kama walivyo wapinzani. Hamna haja ya kujikomba kwake maana yeye sio Mungu.
Very true Mkuu Tindo

Huyu jamaa anajidanganya sana kuwa atauua upinzani kwa kuwanunua viongozi wake wasaliti.......

Anaweza akaua upinzani kama "institution" ya Chadema, kwa kuvitumia vyombo vyake vya dola kama Polisi, NEC, Immigration na TRA etc

Lakini anachosahau ni kuwa upinzani halisi upo ndani ya mioyo ya mamilioni ya watanzania!
 
Anahangaika tu huyo.Watu hawamkubali yeye na CCM yake na ndio maana watu hata kupiga kura hawaendi.

Dk.Bashiru juzi kashindwa tu kutamka kuwa CCM imekufa badala yake kazunguzunguka lakini ukweli CCM hii ya Magufuli ndio kabisa ni kero kwa watanzania kuliko CCM yoyote ile ya siku za nyuma.
 
Ulimuonea wapi anafanya hivyo au kumsikia akiyasema?

Upinzani wamejichimbia shimo la futi sita wenyewe kwa siasa za njaa ya kutaka kujaza matumbo yao.. na sasa wanazidi kujifukia.. eeeeeh

Waambie upinzani wafanye siasa zisizo zilivyo sasa.. hawana jipya kabisaaaa.. hawana ujuzi mabomu.. awamu hii bahasha za khakk hakuna eeeeh

Magufuli oyeeeee
 
Ulimuonea wapi anafanya hivyo au kumsikia akiyasema?

Upinzani wamejichimbia shimo la futi sita wenyewe kwa siasa za njaa ya kutaka kujaza matumbo yao.. na sasa wanazidi kujifukia.. eeeeeh

Waambie upinzani wafanye siasa zisizo zilivyo sasa.. hawana jipya kabisaaaa.. hawana ujuzi mabomu.. awamu hii bahasha za khakk hakuna eeeeh

Magufuli oyeeeee
Magufuli oyeee kwa lipi wakati CCM inamfia mikononi mwake?

CCM hii imebaki kuwa chama dola na si chama cha wananchi na ndio maana hata kwenye uchaguzi watu hawajitokezi kwasababu uchaguzi sasa ni kati ya upinzani na dola na si upinzani na CCM.

Hata katibu wenu mkuu, Dk.Bashiru anakiri kuwa mmepoteza "political legitimacy" na alichoshindwa kutamka hadharani ni kusema tu CCM, hasa hii ya Maguli, haikubaliki na wananchi walio wengi.

Endeleeni kuimba Magufuli oyeee huku wananchi wakiimba "Magufuli ziiiii" katika mioyo yao.

Aendelee tu kuwa Raisi wa kujenga miundombinu na si Raisi wa watu ndio atakuja kujua siasa ni watu na chama cha siasa bila watu sio chama cha siasa bali ni taasisi tu kama taasisi zingine.
 
Anahangaika tu huyo.Watu hawamkubali yeye na CCM yake na ndio maana watu hata kupiga kura hawaendi.

Dk.Bashiru juzi kashindwa tu kutamka kuwa CCM imekufa badala yake kazunguzunguka lakini ukweli CCM hii ya Magufuli ndio kabisa ni kero kwa watanzania kuliko CCM yoyote ile ya siku za nyuma.
Ninachokiona Mimi ni CCM kuendelea kututia umasikini kwa kutumia mabilioni ya shilingi katika kurudia chaguzi hizi......

Wakati at the end of the day, upinzani hautakufa nchini na CCM itatuacha katika umasikini wa kutisha..........

Wananchi ndiyo kwanza watakuwa wamejenga ndani ya mioyo yao upinzani wa dhati kabisa!

Kwa kuwa mchezo wanaoucheza hao CCM ni sawasawa na kukimbiza kivuli chako, kwa kuwa kamwe hautakikuta!
 
Anachoweza yeye ni kuliagiza Jeshi "lake" la Polisi liweze kuwabambikia kesi wapinzani wa DHATI nchini za uchochezi, zisizokuwa na kichwa wala miguu..........

Lakini hataweza kuua upinzani na badala yake wapinzani hao watakuja wakiwa MORE STRONGER!
 
Upinzani utahamia ndani ya CCM.
Tumeshuhudia tokea serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, juhudi kubwa ikifanyika kwa ajili ya kuua upinzani ili nchi ibaki kuwa na mfumo wa chama kimoja

Tumeshuhudia pia wabunge na madiwani wakinunuliwa na kuahidiwa nafasi za "ulaji" iwapo tu wataafiki kujiunga na chama cha CCM kwa kile wenyewe walichokibatiza jina la kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli za kuleta maendeleo hapa nchini

Kutokana na tabia hiyo ya hao wanasiasa "wasaliti" wanaojiunga na CCM tumekuwa tunalazimika kurudia uchaguzi ambao unaligharimu Taifa letu mabilioni ya pesa ambazo zingeweza kufanya shughuli nyingine za maendeleo. Mathalani ujenzi wa madarasa ya shule na hospitali

Lakini kwa bahati mbaya sana priority no 1 ya serikali hii imekuwa siyo tena kujenga madarasa wala hospitali zetu ambazo ziko katika hali mbaya, badala yake ni kuua upinzani nchini!

Kipindi wanachopitia viongozi wa upinzani nchini, hususani wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema ni kipindi kigumu sana ambacho hawajawahi kukipitia tokea mfumo wa vyama vingi nchini urejeshwe nchini kikatiba mwaka 1992

Viongozi kadhaa wa upinzani wamefungwa jela kwa sababu za kisiasa na viongozi wengine wameathirika kutokana na vizuizi wanavyowekewa vya kutofanya siasa na karibu viongozi wote wa chama kikuu cha upinzani cha Chadema wanakabiliwa na kesi mbalimbali za kile kinachoitwa uchochezi kwenye Mahakama zetu

Ninachojaribu kujiuliza ni iweje serikali hii ya awamu ya tano iwachukulie wapinzani maadui wakubwa badala ya kuwachukulia kuwa ni wadau muhimu sana wa maendeleo nchini mwetu??

Na kama kweli kama wapinzani wangekuwa maadui wa maendeleo wangezuiwa kwenye mataifa yaliyostawi sana kimaendekeo mathalani Taifa lenye uchumi namba moja duniani la Marekani, ambalo kwenye Taifa hilo Rais wake Donald Trump anatukanwa waziwazi na wapinzani wa nchi hiyo lakini hawafanywi chochote kwa kuwa Taifa hilo linachukulia kama sehemu ya demokrasia ya kueleza hisia za wananchi kwa ajili ya kuleta maendeleo ya Taifa hilo

Vile vile humu barani Afrika nchi ya Afrika Kusini ambayo ndiyo inayoongoza barani humu kiuchumi, wameimarisha sana demokrasia nchini mwao

Nitoe tu ushauri kwa watawala wetu waiache demokrasia ishamiri nchini kwa kuwa hawana uwezo wa kuua upinzani wa nchi ambao umeota mizizi ndani ya mioyo ya mamilioni ya watanzania

Mungu ibariki Tanzania
 
Hamna cha kumrembea aachwe afanye atakavyo, ila ataaingoza hii nchi miaka yake mitano. Kisha atatumia madaraka yake kujitangaza tena rais. Baada ya hapo atakaa kushoto na upinzani utadhidi kuimarika. Huu ni mwaka wa 3 wala hajafanikiwa kuua upinzani zaidi ya kuwafanyia hujuma. Huko kwenye box la kura nako watu wamemuonyesha kuwa hawababaiki na mbwembwe zake. Afanye hujuma apendavyo kwa wapinzani wake lakini hana ushawishi kwa watu wengi kama walivyo wapinzani. Hamna haja ya kujikomba kwake maana yeye sio Mungu.
Upinzani unakufa mdo mdo, mwaka wa tatu upinzani unazidi dhoofika mbayaa.
Endeleeni kukana.
 
Juhudi kubwa inatumika ili kuonesha kwamba anakubalika wakati kiuhalisia jamaa hakubaliki na mtu yeyote yule hata mtoto mchanga anamkataa huu ni ukweli mchungu unaomuuma sana jamaaa
The opposite is true.
Hakuna rais anaekubalika kama magufuli
 
Upinzani huu ambao ni chaka la mafisadi hauna budi kufa ...Magufuli hawezi kujenga urafiki na wala rushwa,wakwepa kodi na wauza ngada.
 
Upinzani huu ambao ni chaka la mafisadi hauna budi kufa ...Magufuli hawezi kujenga urafiki na wala rushwa,wakwepa kodi na wauza ngada.
Kama kweli upinzani unakufa una haja gani ya kujaza vikosi vya askari kwenye vituo vya kupigia kura unadhani nchi hii iko vitani??

Kama upinzani unakufa RC wa Dar aliwezaje kuwapongeza maskari wake baada ya uchaguzi wa Ukonga kwa kuwawezesha CCM kupata ushindi wa kishindo??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom