Rais Magufuli amteua Charles Kichere kuwa Kamishina Mkuu TRA

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,491
54,884
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amteua Bw. Charles Edward Kichere kuwa Kamishna Mkuu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Kabla ya hapo Bw. Kichere alikuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo na pia amewahi kuwa Mhasibu wa TANROADS. Kufuatia uteuzi huo nafasi ya Naibu Kamishna Mkuu itajazwa baadae.

Kichere anachukua nafasi ya Alphayo Kidata aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu siku ya Alhamisi.
dd4672f782db45e1a72653ae3e85e1ed.jpg
 
Mamlaka ya ukusanyaji kodi TRA ni taasisi nyeti sana kwa maendeleo ya taifa.. Nadhani inatakiwa kuwa na uongozi ambao ni stable ili upange na kutekeleza jukumu lake kwa utaratibu na weledi wa hali ya juu.. Hii kubadilisha uongozi wa juu kila mara kwa maoni yangu, hayaleti tija na wala hayampi nafasi alieteuliwa kupanga mikakati yake ya kuhakikisha kodi inakusanywa kwenye mifumo inayoeleweka..
 
Bavichaa mmebaki watu wa kupandikiza mbegu za udini katika jamii....kwa kuangalia teuzi anazofanya Mheshimiwa Rais Magufuli. Hakika nawahakikishia watanzania tuko sambamba na Rais wetu na hamtashinda.

Awamu ya nne mlikuwa mnaangalia teuzi kwa miwsni ya kidini kwakuwa Rais alikuwa ni muislamu. Sasa awamu ya tano mmeona mtumie ukabila eti 'ukanda uleule'. Kwa taarifa yenu hata wateule wote wawe wazanaki watanzania tunachohitaji ni maendeleo na sio kitu kingine.

Viva Rais Magufuli na serikali yako kwa ujumla.
 
Eti anachapa kazi!!!!
Yaani mshahara wote ule kwa kuteua na kutengua tu?
Hata siku moja ajichanganye shambani asubuhi hadi jioni alime na makamera yammulike!!!!

Mbona mgambo wa bandari anawapiga tafu mara kibao tu!!!!

Au kilimo sio kazi/ajira rasmi.?

Asipokuja shamba kura akaombee huku huko bandarini.
 
Chokaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa mbaya teua tengua.. chokaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa....
 
Back
Top Bottom