Rais Magufuli amtaka mfanyabiashara Mo Dewji kujali wafanyakazi wake kama anavyofanya kwenye timu ya mpira

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,267
Rais Magufuli amtaka Mo Dewji kujali maslahi ya wafanyakazi wake kama Anavyoijali Simba

Rais Magufuli amemtaka Mfanyabishara Mohamed Dewji (Mo Dewji), kuhakikisha anajali maslahi ya wafanyakazi wake kama anavyofanya katika Timu ya mpira wa miguu ya Simba Sports Club ambapo amemsihi kwamba wafanyakazi hao nao wanastahili kupata maslahi yao.

Rais magufuli amesema ivho leo Alhamisi Agosti 1, alipokuwa akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Kiwanda cha Kusaga Nafaka cha 21st Century Food and Packaging, kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam, kinachomilikiwa na mfanyabiashara huyo.

“Mohamed Dewji ninakupongeza sana katika hili na ninakuomba uwajali wananchi wanaofanya kazi hapa hasa maslahi yao kwahiyo unapokuwa unaangalia maslahi ya Simba uangalie pia masilahi ya wafanyakazi wa 21st century food and packaging,” amesema.

Aidha ameiataka Kampuni ya Metl Group iliyopo chini ya mfanyabishara huyo kuachana na utaratibu walionao wa kuagiza ngano kutoka nje ya nchi na badala yake kuanza kulima ngano nchini kwani kwa kufanya hivyo itasawadia Watanzania wanaohitaji ajira.

“Ninatoa wito kwa Kampuni ya Metl Group chini ya Mohamed Dewji, nilipokuwa ninapewa maelekezo nmeambiwa mahindi yanatoka Tanzania ambayo yanatengenezwa tani 300 kwa siku lakini ngano inayotengeneza tani 1400 kwa siku inaagizwa kutoka nje hii tuibadilishe,” amesema.

“Katika maisha yangu nilikua ninafahamu kulikuwa na mashamba makubwa sana ya ngano kule Manyara lakini sasa hivi hayatumiki na kuna wakati wawekezaji wakijaribu wanachomewa moto sasa nitoe wito hata kwa Kampuni yako muanze kulima ngano kwani mtakuwa mmesaidia Watanzania wengi,” amesema.

Mhe. Rais Magufuli amefungua kiwanda cha kusaga unga wa mahindi na ngano cha 21st Century Food Packaging chenye uwezo wa kusaga tani 1,500 kwa siku.
▪Mo aahidi kumuunga mkono Mhe. Rais Magufuli kwa kuwekeza shil Bil 860 utakaozalisha ajira 100,000 ifikapo mwaka 2025


1564671085254.jpeg
 
Vyura mmeshaanza majungu yenu? Naona uungwaji mkono wa mzee kilomoni umeisha sasa? Aya nendeni kwenye wiki ya wananchi.

alafu mumwombe ndugu Rostam awe mwekezaji wenu kama alivyo Mohamedi kwa simba. Maendeleo hayana vyama.
 
Mo bana, eti atawekeza tshs Bil. 860, hii si kweli, asicheze na akili zetu, atawekeza labda tshs 100 bil alafu atasema bil 800 huyu..
Mbona umepinga Bil.860.Aseme mwenye pesa anayewekeza wewe usiyejua chochote kuhusu uwekezaji huu upinge?Mbona hujapinga ajira ya watu laki moja?Uwekezaji huo ni muda mrefu mpaka 2025.
Ujahili ni ujinga. Yaani mtu anampangia mwenye pesa kiasi cha kuwekeza.
 
Rais Magufuli amtaka Mo Dewji kujali maslahi ya wafanyakazi wake kama Anavyoijali Simba

Rais Magufuli amemtaka Mfanyabishara Mohamed Dewji (Mo Dewji), kuhakikisha anajali maslahi ya wafanyakazi wake kama anavyofanya katika Timu ya mpira wa miguu ya Simba Sports Club ambapo amemsihi kwamba wafanyakazi hao nao wanastahili kupata maslahi yao.

Rais magufuli amesema ivho leo Alhamisi Agosti 1, alipokuwa akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Kiwanda cha Kusaga Nafaka cha 21st Century Food and Packaging, kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam, kinachomilikiwa na mfanyabiashara huyo.

“Mohamed Dewji ninakupongeza sana katika hili na ninakuomba uwajali wananchi wanaofanya kazi hapa hasa maslahi yao kwahiyo unapokuwa unaangalia maslahi ya Simba uangalie pia masilahi ya wafanyakazi wa 21st century food and packaging,” amesema.

Aidha ameiataka Kampuni ya Metl Group iliyopo chini ya mfanyabishara huyo kuachana na utaratibu walionao wa kuagiza ngano kutoka nje ya nchi na badala yake kuanza kulima ngano nchini kwani kwa kufanya hivyo itasawadia Watanzania wanaohitaji ajira.

“Ninatoa wito kwa Kampuni ya Metl Group chini ya Mohamed Dewji, nilipokuwa ninapewa maelekezo nmeambiwa mahindi yanatoka Tanzania ambayo yanatengenezwa tani 300 kwa siku lakini ngano inayotengeneza tani 1400 kwa siku inaagizwa kutoka nje hii tuibadilishe,” amesema.

“Katika maisha yangu nilikua ninafahamu kulikuwa na mashamba makubwa sana ya ngano kule Manyara lakini sasa hivi hayatumiki na kuna wakati wawekezaji wakijaribu wanachomewa moto sasa nitoe wito hata kwa Kampuni yako muanze kulima ngano kwani mtakuwa mmesaidia Watanzania wengi,” amesema.

Mhe. Rais Magufuli amefungua kiwanda cha kusaga unga wa mahindi na ngano cha 21st Century Food Packaging chenye uwezo wa kusaga tani 1,500 kwa siku.
▪Mo aahidi kumuunga mkono Mhe. Rais Magufuli kwa kuwekeza shil Bil 860 utakaozalisha ajira 100,000 ifikapo mwaka 2025
View attachment 1169472

Mbona serikali imeshindwa kuwajali wafanyakazi wake?
 
Katika Kampuni zinazolipa vibaya hapa Tanzania nadhani huyu anaongoza, dogo moja kamaliza kadigrii kake mshahara kapewe laki tatu na nusu kwa cheo cha meneja. Nikamwambia acha usenge kaacha sahizi yupo sehemu take home yake 900,000.
Kwani alilazimishwa kufanya kazi? si aliomba mwenyewe?
 
Mbona serikali imeshindwa kuwajali wafanyakazi wake?
Bora umeniwahi. Nilitaka kuandika kitu ambacho kingenisababishia ban ya milele.

Huu unaenda mwaka wa tano tangu aingie madarakani lakini hajawahi hata saa moja kuwafikiria watumishi wa umma. Anachofikiria yeye ni vitisho tu na mikwara ya jogoo.
 
Rais Magufuli amtaka Mo Dewji kujali maslahi ya wafanyakazi wake kama Anavyoijali Simba

Rais Magufuli amemtaka Mfanyabishara Mohamed Dewji (Mo Dewji), kuhakikisha anajali maslahi ya wafanyakazi wake kama anavyofanya katika Timu ya mpira wa miguu ya Simba Sports Club ambapo amemsihi kwamba wafanyakazi hao nao wanastahili kupata maslahi yao.

Rais magufuli amesema ivho leo Alhamisi Agosti 1, alipokuwa akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Kiwanda cha Kusaga Nafaka cha 21st Century Food and Packaging, kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam, kinachomilikiwa na mfanyabiashara huyo.

“Mohamed Dewji ninakupongeza sana katika hili na ninakuomba uwajali wananchi wanaofanya kazi hapa hasa maslahi yao kwahiyo unapokuwa unaangalia maslahi ya Simba uangalie pia masilahi ya wafanyakazi wa 21st century food and packaging,” amesema.

Aidha ameiataka Kampuni ya Metl Group iliyopo chini ya mfanyabishara huyo kuachana na utaratibu walionao wa kuagiza ngano kutoka nje ya nchi na badala yake kuanza kulima ngano nchini kwani kwa kufanya hivyo itasawadia Watanzania wanaohitaji ajira.

“Ninatoa wito kwa Kampuni ya Metl Group chini ya Mohamed Dewji, nilipokuwa ninapewa maelekezo nmeambiwa mahindi yanatoka Tanzania ambayo yanatengenezwa tani 300 kwa siku lakini ngano inayotengeneza tani 1400 kwa siku inaagizwa kutoka nje hii tuibadilishe,” amesema.

“Katika maisha yangu nilikua ninafahamu kulikuwa na mashamba makubwa sana ya ngano kule Manyara lakini sasa hivi hayatumiki na kuna wakati wawekezaji wakijaribu wanachomewa moto sasa nitoe wito hata kwa Kampuni yako muanze kulima ngano kwani mtakuwa mmesaidia Watanzania wengi,” amesema.

Mhe. Rais Magufuli amefungua kiwanda cha kusaga unga wa mahindi na ngano cha 21st Century Food Packaging chenye uwezo wa kusaga tani 1,500 kwa siku.
▪Mo aahidi kumuunga mkono Mhe. Rais Magufuli kwa kuwekeza shil Bil 860 utakaozalisha ajira 100,000 ifikapo mwaka 2025
View attachment 1169472
Anawanyonya sana wafanyakazi wake MO,machoni pa umma anaonekana mwema ila viwandani kwake hatari tupu.

Mhindi mhindi tu,japo Serikali nayo inachangia kwa kutofuatilia maslahi ya wananchi wake na vyama vya wafanyakazi vipo kwaajili ya mei mosi
 
Barrick si mwekezaji wa ndani. Tungekuwa tunawatendea na tuwawekea wawekezaji na wafanyabiashara wa ndani mazingira mazuri yenye kuhamasisha uwekezaji kama tunavyowafanyia wale wa nje nna uhakika hali ingekuwa tofauti.
 
Bora umeniwahi. Nilitaka kuandika kitu ambacho kingenisababishia ban ya milele.

Huu unaenda mwaka wa tano tangu aingie madarakani lakini hajawahi hata saa moja kuwafikiria watumishi wa umma. Anachofikiria yeye ni vitisho tu na mikwara ya jogoo.

Kwa wale wakristo, wanahitwa wanasheria.
Luke 11:46 New International Version (NIV)
Jesus replied, “And you experts in the law, woe to you, because you load people down with burdens they can hardly carry, and you yourselves will not lift one finger to help them.

Luke 11:46:
Akasema, Nanyi wana-sheria, ole wenu, kwa sababu mwawatwika watu mizigo isiyochukulika, wala ninyi wenyewe hamwigusi mizigo hiyo hata kwa kimoja cha vidole vyenu.
 
Back
Top Bottom