Rais Magufuli ametupunguzia mbwembwe na fujo za hawa watu

jsenyinah

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
249
338
WanaJF, wakati mkitafakari weekend yetu inavyoyoyoma,embu tuwaangalie hawa viongozi wetu na fujo zao kwenye awamu hii ya tano.

Vikao,semina, ziara na mengineyo yaliyokuwa yakifanywa na waheshimiwa wetu huko duniani,naona sasa kila kitu hapahapa nchini.Kipindi kile mara oooh Dubai, China, Korea ya kusini, Afrika ya kusino, London na kwingineko. Saiv naona kila kitu Dodoma, makao makuu ya nchi na serikali.

Zamani ilikuwa huko mikoani unapishana na STK nyingiiii barabarani zenye mlingoti wa bendera.Sijui zilikokuwa zikienda.Halafu utakuta tu dereva yupo mwenyewe.

Kwa wale wakazi wa Dodoma walikuwa wanapata taabu sana na fujo za waheshimiwa hasa kipindi cha Bunge,sasaiv kupo shwari,heshima imerudi.

Wote tunaisoma namba.
 
Siku hiz huku mwanza mbwembwe zimebaki kwa watu wawili tu king msukuma na john bina wengine wote chali
 
Kocha anazingua,kuanzia kipa mpaka wings namba 11 wote mabeki,kuanzia dk1 mpaka 90 timu inalinda goli!,...washabiki waisusa timu,kocha hataki ushauri...mwaka huu hii timu Kama haikushuka daraja sijui!...
 
Uongo dhambi jamaa kawabana wapiga dili adi raha na japo na wasiopiga dili pia tumebanwa..
 
Tumezungukwa na Mashamba na Tunakufa na njaa..

Ndio hapo ninapowashangaa watanzania.
Nimebahatika na vijihela na nika nunua Shamba hela 20, ngombe zaidi ya 20 na nini mwenyewe siko nchini. Shamba na ngombe wanateketea, hakuna anao jishughulisha, Lakini hao ndugu zangu waliozoea maisha ya ujanja sasa hivi wana lalamika kila siku maisha magumu. Yaani hata kupanda mchicha na nyanya au mboga hapo wanashindwa,
 
jsenyinah,
Tapeli mkubwa wewe. Unajua wote tunaisoma namba iweje uwadanganye Watanzania wenzako kuwa wauze sungura TZS.36,000/- hadi 65,000/-
Ni Mtanzania gani mwenye uwezo huo kwa sasa ilhali wote tunaisoma namba?
 
Hata huku kitaaaaaaaaa,Heshima imerudi wanapaki magari vijiweni tunapiga nao soga!
 
Back
Top Bottom